Mabraza wa Kariakoo na dili zao

Hii kubwa sana brother, wachache sana tunaokuelewa.
 
huu utoto peleka Facebook.
 
huu utoto peleka Facebook.
 
Dah hii ni Extra Miles Bruh ... Nimewakumbuka ma bro wa TMK, tembea Tandika yote ile tena shuka mpaka Yombo huko Relini, Mnanda daily Mtaani tena hapo Mateja Kibaoooo

Rip all of em
 
Dah kitambo kile keep in resting bro Afizi yosso , MUBABA we always pray for you na tunakusubiri kitaa .

No pain no sweet , downtown kitambo , ushua na maisha ya ushua ni vitu tofauti ila jamii inaamini yasiyoaminika _ rest easy Lemutuz nakukumbuka dingi

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
 
NAENDELEA........!!!!
Nilikua kimya kidogo sababu nilikua kwa wabangubangu huko nafuatilia dili flani afu tukadakwa na masoja wahuni waliopinda balaa wa FARDC katika road block ya barabarani kati ya mji wa Lellwa na Kamombo wakitudhania sisi ni wahalifu tunawauzia silaha banyamulenge,silaha za kutokea Uganda au tunanunua madini ya vikundi vya waasi na kuyavusha ziwa Tanganyika mpaka Burundi.
Ikabidi tukae ngomeni.......mpaka pale wadau walipokuja kututolea dhamana
NAPOMAANISHA DHAMANA NI KWAMBA WADAU WALIVAMIA NGOME NA KUZICHAPA MCHANA KWEUPE WAKIDAI WANAWATAKA WASWAHILI WAO ESPECIALLY MIMI WALIEKUA WANANIITA KALULU MTOTO YA ZANZBAR 🤣🤣🤣 NA LILIKUA SHAMBULIZI LA SUPRISE SO IKABIDI TUACHIWE HURU MAANA MASOJA WALIKIMBIA NA KUTELEKEZA KAMBI AMBAYO ILIKUA KAMA KITUO KIDOGO CHA KUKAGULIA MAGARI BARABARANI KATI YA MJI WA LWELLA NA KAMOMBO BASI WADAU WAKATUTOA KINGUVU SISI NA WASHIRIKA WAO WENGINE WALIOKAMATWA KIPINDI HICHO*
Ila wale manjagu wahuni wa FARDC walitupukutisha mzigo wote wa mawe tuliopewa kuupeleka BURUNDI kimagendo kwa kuuvusha ziwani....na mpaka mda huu nipo na ugomvi na MWANANGU NDAGARA....maana alidai mm nina roho nyepesi sana ndio maana wale wanoko wa FARDC wamechukua mawe yetu......SASA NIPO SEHEMU SALAMA NIMETULIA ngoja niwape story kidogo...!!!
Kuna braza wetu mmoja wa kuitwa. ""NDAGARA""" yeye amezaliwa katika mji mmoja wa mpakani mwa DRC na Burundi ambao unaitwa MIDUHA....anaishi Nairobi alikuja masikani na dili la kuchukua mawe kinyemela kutoka DRC na kuyavusha Burundi....afu baada ya hapo""YANAUZIKA BILA KUKATWA KODI""".
Braza akasema ni issue ya wiki tatu tu tunamaliza kila kitu....mchawi pesa ya mtaji tu...
Akasema ameshawapanga watu wake Burundi na DRC na mizigo wanayo.....kwahiyo ni sisi tu...twende MIDUHA au tumtumie hela amalize kila kitu.......TUKAPIGIANA HESABU ZINAHITAJIKA MILIONI 60 ZA KIBONGO.....KWA KUANZIA AMBAZO ZITAZAA MILIONI 314 KAMA MZIGO UKIVUSHWA SALAMA BURUNDI......!!!
Kama mnavyojua ndugu yenu napenda hela.....afu hapa nilipo nimepigika na mwaka ndio unaanza.....nikaona hii fursa ngoja nichungulie........
Kama kweli unaweka milioni 60 na unapata 314 ndani ya wiki tatu.....basi mchawi mtaji...ngoja mtaji utafutwe hata kwa kukopa.
Hapa town sisi watoto wa mjini hatuna hela.....ila hela ya kula sio issue na hela za kukopa sio issue wala kupata asset za kuweka bondi sio issue"""""MAANA TUNAAMINIKA""".
Unajua TANZANIA kuna watu wana hela ila kama hawakujui hawawezi kukukopesha sababu pesa nyingi zinapitia mlango wa nyuma kuingia mifukoni mwa watu....
Safari hii nikawacheki wahindi mabraza zangu wa migodini huko kwa wasukuma""BIG UP BRAZA PATEL""" ....nikampa mchongo wanikope hela afu bondi nawaachia gari na trekta la kulimia vikae yadi mpaka hela itakapoanza kurudi.
Tukahesabiana siku 60 bila riba
WANA FAMILIA HATUTOZANI RIBA
Hela ikapatikana ikawekwa kibindoni sehemu salama ambayo mimi niliyekopwa na mkopeshaji tunaijua afu ndio nikakaa mezani kusikiliza hilo dili.....maana lilivutia.
NDAGARA: Mpango upo hivi...ni kwamba kule DRC hasa maeneo ya KIVU KUSINI hasa miji ya LUBENGA,KASABA,MALUNGU,KAHOLOLO, KILEMBWE NA TULAMBO....kuna mawe ya kumwaga ni sisi kununua tu na kuyavushia ITARA au KAKAMBA na kuyauzia MIDUHA kwa wadau wa kununua mawe.....kila kitu kipo under control.....na biashara ikiwa nzuri tutahamishia makazi BUJUMBURA kwa mda ili tupige hela..!!!
MIMI: Mkuu hii dili unachosema nakuelewa ila sasa kuna risk kubwa...afu mtaji wakuanzia milioni 60 tena za kukopa ni mdogo mno,......afu hapo hatujaweka gharama za usafiri na mambo mengine ya kibiashara...
MIMI: Kwanini tusijipe wiki mbili twende kigoma afu tuvuke ziwa tuingie burundi then tufuatilie soko sisi wenyewe kwa kutazama na sio kuambiwa.....MAANA MANENO YA KUAMBIWA CHANGANYA NA YAKO.
NDAGARA: Dogo sikia unachosema mimi nakuelewa.....wewe tafuta milioni sitini ya mtaji wako na mimi nina pesa ya mtaji wangu milioni sitini.
Hatutoingia kwenye biashara mpaka tufanye uchunguzi....ili tuone maneno niliyoambiwa ni kweli....
Gharama za kwenda safari yetu ya kuchunguza nadhani itatugharimu milioni mbili za kitanzania kila mmoja......sababu kule Burundi mimi ni nyumbani....na nina wadau wengi kwahiyo kwa kule gharama hazitokuwepo.
*NDAGARA ALIPOSEMA WADAU ALIMAANISHA WAASI WA MSITUNI KULE KONGO AMBAO WANATAFUTA MASOKO MAZURI YA KUUZIA MADINI YAO....SABABU HAWATAKI KUWAUZIA WANYARWANDA NA WAGANDA WAKIDAI WANAWAPUNJA MGAO
NDAGARA alinificha mengi ili nimpe kampani ila niliyajua nilipofika BURUNDI na kukutana na wazee wa kazi.....!!!!
Kesho yake asubuhi
Ndagara katoka Nairobi kaja dar afu tukakaa chini na kupangiana mipango ya kwenda kuchungulia fursa na ikiwa nzuri tunajitosa hivyo hivyo kila mtu na mtaji wa kukopa....
Mimi nikamcheki braza PATEL na kumwambia zile siku 60 asizihesabu maana bado sijaanza hiyo biashara rasmi,na kama ni biashara ya uhakika nitamuingiza na yeye aongeze mtaji.....ngoja nikaichungulie kwanza.....na katika zile milioni 60....tutoe milioni mbili za safari afu zingine akae nazo kwanza mpaka mimi nikiona biashara ipoje ndio nimwambie.
Na zile bondi zangu arudishie wadau wangu wakae nazo zisikae yard tena,sababu biashara bado kuanza.
Mimi naingia kigoma mara moja....kisha navuka ziwa naingia Burundi kibishi kuchungulia fursa na kukutana na wadau wa huko.
Jamaa yangu Ndagara kanihakikishia hao wadau wana mizigo ya kutosha ila tatizo ni wanunuzi tu wa kimagendo wa kuaminika na wao.
Fasta nikakamata gari mpaka kahama....pale kahama nikakamata gari mpaka Nyakanazi.....pale Nyakanazi nikakamata gari mpaka Kakonko......Kibondo........Kasulu.... then nipo town Kigoma ....mji wenye kumbukumbu nyingi na mimi since 1996............!!!
Ndagara tunakutana Kigoma mjini mitaa ya Mwanga afu tunakaa chini kupanga mpango kazi wa kukutana na wadau wenye mzigo....na namna ya kuvuka ziwa kimya kimya mpaka upande wa Burundi.....either tushukie mji wa KABEZI au GITAZA .....kule juu Bujumbura wachawi wengi ni noma!!!!
KUMBUKA SIKUJUA WADAU KAMA NI WABABE WA VITA HUKO DRC WATU WALIOPINDA BALAA*
Kaa chonjo nije nikupe kilichoendelea huko maana vita wewe visikie tu ila usiombe vikukute....!!!
ITAENDELEA................!!!!
 
Blood unatisha winga kichizi

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
 
INAENDELEA......!!!!
Mpango kazi ulikua hivi........kutokea kigoma kuna jamaa atatuvusha ziwa tanganyika upande wa Tanzania mpaka katikati ya ziwa mpakani mwa burundi na DRC muelekeo wa kuelekea bandari bubu ya mji mdogo wa Kabezi Burundi.....ambapo katikati ya mpaka wa ziwa kati ya Burundi na DRC tutapokelewa na jamaa watakaotufaulisha mpaka nchi kavu upande wa burundi katika huo mji mdogo wa Kabezi.
Yote hayo ni katika kukwepa doria za boti za wanajeshi na maharamia wanaowaibia wavuvi na wafanyabiashara ziwani,maana usalama ziwani wakati mwingine sio wa uhakika.
Kutokea pale mji mdogo wa Kabezi ni kupanda bodaboda kuitafuta Mujejuru then kuingia Bujumbura downtown.
Pale Bujumbura hakuna kukaaa sana ni kukutana na wadau wa kikongo,ambao ndio watakaotuvusha boda to boda kupitia Miduha au Musaga kuingia kwa wakongomani huko kivu ya kusini kupitia mipaka isiyo rasimi kukwepa wanajeshi wa Burundi mpakani,wanaowawinda waasi wanaoipinga serikali ya Burundi.
Mpango kazi ukaendelea hivi....!!!
Ukishaingia kwa wakongomani huko kivu ya Kusini.....kuna kupokelewa na wadau ambao watatuunganisha na wadau wenye mali....ila sasa wadau wenyewe wanakaa mbali na mji....i mean wadau wenyewe wanakaa maporini na ni watu wa kuhamahama.
Na sifa kubwa ya maeneo ya kivu ya kusini ni barabara mbovu kupitika na usalama usio wa uhakika kutokana na vikundi vya waasi visivyo rasmi na magenge ya wahalifu.
Kati ya miji ya Kasongo na Fizi na kule kaskazini kwenye mji wa Kitenge....hapo katikati ndio wadau walikua wanaleta mizigo yao kutokea Kivu kaskazini.
Barabara ni mbovu na ni lazima wapitie barabara za vichochoroni na maporini kuwakwepa askari wa FARDC na vikundi vya waasi na wahalifu...Mwanzoni ilikua rahisi kuyavushia Rwanda au Uganda ila sasa waasi wa kinyarwanda na kihutu ndio wamekua kikwazo na pia bei za wanyarwanda na waganda wadau walikua wanaona kua wanapunjwa kimaslahi.....ikawabidi wadau watafute ruti nyingine kupitia Burundi.
MIDUHA BURUNDI:
Ukiwa pale Miduha basi wadau kwanza wanakuuliza kua"""Je papaa unaweza kulushika fango fango""""
Fango fango hapo wanamaanisha AKA 47 iliyovunjwa kitako na kuongezewa magazine mbili kila upande!!
Vile vile wanakuuliza je papaa unaweza kufumusha""Embe""'....hapo wanamaanisha unaweza kurusha guruneti!!!
Watakuuliza pia je papaa unaweza kuvuya kumumaji?????
Hapo wanamaaanisha kua je unaweza kuogelea.
Wanakuuliza yote hayo ili kama hujui kuogelea au kutumia hivyo vitu ufundishwe..
Na ukumbuke kipindi hicho umeingia Burundi kimagumashi na unapaswa kuingia DRC kimagumashi ili kuufuata mzigo kuutazama na kujihakikishia hiyo fursa
Soko la mzigo i mean black market lipo Burundi....maana kuna wadau kibao wa kikongo na kikenya wananunua mzigo kwa bei rahisi ila wanaogopa kuvuka na kuingia kule Kivu ya kusini au Kivu ya kaskazini kwa sababu za kiusalama.
Mzee kama hujui unapewa mafunzo kidogo kuhusu hivyo vitu hapo juu nilivyovielezea then unajiandaa kwa safari ya msituni....na unapewa code name....""Mine was KALULU""".....!!!
Mzee kwanza hilo Fango fango ni zito karibia kilo tano kasoro ukichanganya na magazine zake......pia limeundwa kienyeji kulenga shabaha ni mpaka uwe mzoefu nalo.....ila linatoa bonge la sauti mpaka kero likifyatua risasi.
Embe ni yale maguruneti ya kienyeji ambayo ukikosea kidogo tu kuwasha baruti basi ujue yanakulipukia wewe mwenyewe ulielishika.
Vilevile mavazi ya kuvaa ni nguo za kiraia na mabuti ya mvua na makoti ya mvua...njia nzima mnapita porini hakuna kupita barabarani,na mkikutana na jeshi la FARDC au vikundi vya wahalifu wa BAKOMBA au WABANGUBANGU IYEMA au WAKATO KOMBE au WAKONGOLO hakuna kuuliza ni kushambuliana tu....maana na wao ni wezi...wakiwakuta na mzigo wanawanyanganya kibabe.
Nipo na bro Ndagara tunapewa somo na mwisho tukaulizwa je mpo tayari kuvuka boda kwenda kucheki mzigo.
Mpo tayari kuua ikibidi???
Mpo tayari kuuawa ikibidi???
Mpo tayari kukabiliana na lolote ikibidi???
Mambo yakienda vizuri ni safari ya wiki moja,ila mambo yakienda vibaya mnaweza kukaa huko miezi miwili mpaka mitatu.
Je mpo tayari?????
Wadau wakajitambulisha kua wao ni MAKEMBA BUNENE hakuna mtu anayewatawala au kuweka sheria juu yao....wao ni kikundi huru cha underground militia force supported by them self to protect their own business interest.
MAKEMBA BUNENE MILITIAS:
Jamaa wamepinda balaa,kwanza wapo wengi na wapo very organized na issue kwao sio madaraka bali kulinda maslahi ya biashara zao.Na wana vikundi vya kijeshi wenyewe wanaviita LA GUIERRA ambavyo vinalinda site zao za machimbo....ndio walikua wanatafuta masoko mbadala ya mzigo yao.....hasa soko haramu(Black market) la kenya .Na wana silaha za kivita na wapo very organized huko misituni ila wapo very low key huwaoni popote hata kwenye politics za DRC.Na kila kikundi cha waasi kwao ni adui na majeshi ya serikali kwao ni adui.MAKEMBA BUNENE kwa nje wanaonekana raia wa kawaida na wanavuka mpaka kihalali kuingia Burundi kama wajasiriamali wa kawaida wanaojitafutia mkate wao wa kila siku
LA GUIERRA:
Hawa ni special force,s waliojizatiti kwa silaha bora za kijeshi na sijui wanazinunua wapi.Walichokosa ni magari ya deraya tu na vifaru na mzinga.Ila kwa silaha zingine wapo vizuri tu na wana stock za kutosha.....na hawavai mavazi ya kijeshi bali wanavaa kiraia kwa namna wanayojya wao katika kutambuana hawavai mavazi ya kijeshi na hio ndio code yao kubwa.
Ukiwaona kwa nje ni raia kabisa ila kwa ndani ni wahalifu sugu walioshindikana na kwao ni mwiko kujihusisha na siasa.....wao wanajihusisha na biashara zao na kulinda masilahi yao ya kibiashara katika eneo la kivu ya kusini na kivu ya kaskazini.
Wadau wakatuuliza je mpo tayari tuwapeleke mkaone kwanza shughuli zetu zinavyofanyika?????
Sisi sababu tunataka kwenda kutazama mizigo basi haraka haraka tukajibu kua tupo tayari kwa safari wala hakuna shida.
Ilikua saa nne asubuhi,basi wakatuambie mle kwanza ugali kabla ya kuanza safari ya kuvuka boda kuingia DRC.....na sikujua kwanini wakitusisitiza tule kwanza kabla ya kuanza safari ya kutoka pale Miduha na kuvuka boda kuingia upande wa pili wa mji wa Kitenge kwa kupitia kati ya mji wa Bukavu na Uvira ila sio kwenye mipaka rasimj bali njia za vichochoroni ambako hali za usalama ni za kutatanisha kwa asilimia 100%.
Mimi na Ndagara tukatoka chemba kidogo na kuanza kuulizana vitu.
MIMI: Bro wewe mwenyeji hapa Miduha,,,,je tuvuke huko tukachungulie fursa???????
NDAGARA: Sikiza dogo nisingetoka Nairobi na kuja Dar then Kigoma then huku kama sina tumaini na hizi fursa.
Twende tukachungulie tuone hizi fursa zipoje sawa bwana mdogo.
MIMI: Vipi kuhusu risk zake bro???
NDAGARA: Acha uoga dogo utajiri hautafutwi kirahisi.....utaogopaje wakati tupo na wazee wa kaza""Makemba bunene"""acha uoga......tatizo lenu watanzania waoga sana nyie 🤣🤣🤣
MIMI: Sawa bro hakuna shida ila duuuh kama hapa mpakani pako hivi.. sijui huko upande wa pili pakoje.
Basi tukawarudia wadau na kuwaambia kua tupo tayari kwa safari...ngoja tuweke mambo yetu sawa.Wakajibu sawa wanatusubiri ila wakatusisitiza lazima tule kwanza ugali wa kutosha kabla ya kuondoka Miduha.
ITAENDELEA..........!!!!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…