DOKEZO Mabosi wa Benki ya CRDB Tawi la Gongo la Mboto someni kero hii ya wafanyakazi wenu

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Najua nikitoa hapa kero yangu hapa Jukwaa la Fichua Uovu, kero yangu itafika kwa wahusika.

Kero yetu/yangu kubwa ni kwa Wahudumu wa CRDB Tawi la Gongo la Mboto lililopo pale Mzambarauni Kiukweli, Dar es Salaam, wale wahudumu ni wasumbufu na wanakera mno.

Nitoe kisa kimoja, Jumanne ya Novemba 28, 2023 nilienda pale kuchukua kadi yangu mpya baada ya kupoteza ya zamani,

nilitumiwa SMS tarehe 25 Nov kwamba kadi ipo tayari nikachukue pale.

Basi nikaomba ruhusa kazini kwamba nitachelewa kufika kwa saa kadhaa, nikaahidi hadi saa nne Asubuhi.

Nilifika mapema Benki na kulazimika kusubiri wafungue, ulipofika muda wao wa kufungua hakuna hata mpangilio mzuri unaotuongoza wateja, haijulikani usimame wapi, wahudumu wanashindwa hata kuwapanga wateja.

Ilipofika zamu yangu nikawaeleza shida kilichonipeleka pale, wakauliza nilipata SMS, nikawaambia ndio na kuwaonesha.

Basi mhudumu mmoja akaingia ndani kutafuta kadi, alikaa huko kuanzia saa mbili hadi saa tano hakutoka, wakati huo mimi nimeaga kazini kuwa saa nne nitaingia wa kuwa nilijua ni suala la kwenda kuchukua kadi tu.

Basi nikaondoka bila huduma, kiukweli huduma ya pale hovyo sana wahusika wajue hilo.
 
Najua nikitoa hapa kero yangu hapa Jukwaa la Fichua Uovu, kero yangu itafika kwa wahusika.

Kero yetu/yangu kubwa ni kwa Wahudumu wa CRDB Tawi la Gongo la Mboto lililopo pale Mzambarauni Kiukweli, Dar es Salaam, wale wahudumu ni wasumbufu na wanakera mno.

Nitoe kisa kimoja, Jumanne ya Novemba 28, 2023 nilienda pale kuchukua kadi yangu mpya baada ya kupoteza ya zamani,

nilitumiwa SMS tarehe 25 Nov kwamba kadi ipo tayari nikachukue pale.

Basi nikaomba ruhusa kazini kwamba nitachelewa kufika kwa saa kadhaa, nikaahidi hadi saa nne Asubuhi.

Nilifika mapema Benki na kulazimika kusubiri wafungue, ulipofika muda wao wa kufungua hakuna hata mpangilio mzuri unaotuongoza wateja, haijulikani usimame wapi, wahudumu wanashindwa hata kuwapanga wateja.

Ilipofika zamu yangu nikawaeleza shida kilichonipeleka pale, wakauliza nilipata SMS, nikawaambia ndio na kuwaonesha.

Basi mhudumu mmoja akaingia ndani kutafuta kadi, alikaa huko kuanzia saa mbili hadi saa tano hakutoka, wakati huo mimi nimeaga kazini kuwa saa nne nitaingia wa kuwa nilijua ni suala la kwenda kuchukua kadi tu.

Basi nikaondoka bila huduma, kiukweli huduma ya pale hovyo sana wahusika wajue hilo.
Nendeni bank zenye wateja wachache,hao CRDB wameshazidiwa na idadi ya wateja wa kuwahudumia,hakuna ufanisi tena wala kusikilizwa
 
Yaani hii bank siku hizi ni kama matawi yote yana shida. Unaweza kuta kuna madirisha ya tellers 4 au 5 lkn mhudumu ni mmoja tu
Mkuu tuwalaumu CRDB lakini kwa uzoefu wangu hapa Tanzania Benki zote ni za hovyo sana, tena sana.. Wamezidiana tu kiwango cha Uhovyo..

Zote customer care zao zina mashaka.. Sorry to say!
 
Ukienda Kibaha utafunga na hiyo akaunti kabisa.CRDB ni benk ya hovyo sana.Nilikuwa na hisa huko wakanisumbua na mikopo yao niliamua kuuza hizo hisa na sitakuja kutumia huduma zao milele.

Sent from my TECNO B1f using JamiiForums mobile app
Mkuu uliuzaje Hisa?mimi ninazo NMB Bank na mwaka huu Juni nilipata gawio la Tsh. 545,000,naamini 2024 gawio litafika 700,000,nataka niuze Hisa zangu NMB,naomba muongozo
 
Back
Top Bottom