Mabomu Arusha: Mtazamo wangu

Mabomu Arusha: Mtazamo wangu

Daima tutaendelea kutafuta maadui nje yetu kumbe adui yumo miongoni mwetu. Kama alivyosema waziri mkuu wa zamani, mtu ambaye ameingia mamlakani kwa kutumia kalamu kuwavunja adui zake, atatumia risasi kubaki madarakani.
Ninyi endeleeni kutafuta adui wa nje lakini sisi wengine tumeshajua adui ni nani.
 
POLISI ni watumiwa no.1 kisha CCM ni mtuhumiwa no.2 na Lukuvi na Serikali yao ni watumiwa no.3 Ukisikiliza kauli ya Lukuvi,Nape na Mwigulu Lawama zote wanazielekeza kwa CHADEMA,Kwanini? maana wao ndio wenye dola intelegensea yao inawaona CHADEMA tu kwa kuwa wanazidi kupata NGUVU na kukubalika kwa wananchi kila iitwapo leo? Mtoto aliyepigwa risasi anasema ni POLISI kampiga,mama aliyethubutu kumnyoshea kidole aliyerusha bomu ili akamatwe inasemekana alipigwa risasi.Sasa Kwanini TUSISADIKI KUWA POLISI,CCM NA SERIKALI NDIO WAPANGAJI WAKUU WA MLIPUKO HUU? Kwa makini kabisa nikiwa na Akili timamu mchoro huu umepangwa kwa makusudi na SERIKALI ya CCM ikiwatumiwa POLISI ili UCHAGUZI usifanyikekwa kata 4 za jiji la Arusha ili CCM waendelee kuiba kwa raha zao. CCM MKUBALI KUSHINDWA ARUSHA KAMA NIKULEMEWA CCM MKO HOI BIN TAABANI.
 
Acha 2gombane kama majogoo wakat vifaranga hawanashida ya kumjua baba yao.
 
ulichoandika kwenye uzi huu ni sahihi na kina mashiko zaidi,kuliko hicho wanachong'ang'ania wao.Kumbuka bomu la kanisani watu walichangia kwa nguvu zote kwamba ni waislamu.Baadhi ya magazeti yakanukuu kwamba mrusha bomu alikuwa amevaa kanzu na kilemba.Walipokuja kukamatwa waliohusika joto lilipungua.Wale waropokaji wakakaa kimya.Kwa hiyo hata hili tayari wapo wale ambao hawataki kuambiwa kingine isipokuwa waambiwe fulani ndo muhusika.Ni upuuzi na hakuna ushahidi wa kuthibitisha hicho wanachosema.Hawa wanaosema fulani anahusika ndo wachonganishi wa amani ya tz.Wanasiasa uchwara nao wanachangia vurugu na kuharibu amani ya nchi,wanaropoka sana tena bila ushahidi
basi, kama kweli hili suala limefanywa na polisi wetu wa tanzania, kuna sababu zote wananchi kuingia mitaani kwa amani kushinikiza livunjwe! kauli za wengi lazima zitakuwa na mashiko! kwa sababu hiyo, nami naanza kufuatilia mtiririko huu wa polisi kurusha risasi na bomu. mungu ainusru tanzania.
 
kaka gemu ya kucheza na akili ama fahamu,mind controling issue.ila chadema iwe makini na maneno wayaongeayo kwani vita kuu ni yakunasa akili hususani sisi mbumbu tusiojiuliza kwanini.lema kahusishwa na mabomu kisa kauli,nauna mchezo ule wa ngeli ugaidi!
Masaa 21 yaliyopita · Like
 
Haya ni mawazo dhaifu sana, sisi ndio soko la pili kwa ukubwa kwa kenya na mpaka wa namanga ndio unapitishia hizo bidhaa zao sasa wakiharibu Arusha watapitisha wapi bidhaa zao? wanapitishia pia rawa material toka tanzania arusha, KQ ndizo zinaleta watalii wengi TZ na wengi wanaelekea Arusha. Haiingii akilini hata kidogo Wakenya wafanye huu upumbavu. Wakenya wanafanya juhudi kujenga uchumi wao kama kawaida yao na sisi tunaendelea kupiga domo na kuwatetea serikali dhaifu. Unda tume huru na yenye uwezo ituambiwa hawa ni akina nani then tujue mbichi na mbivu hawataki wanaishia kutoa povu kama mbwa mwenye kichaa halafu baadhi yetu tunadanganyika kwa huu upuuzi.

Jukumu la kwanza la serikali ni kupatia raia wake usalama. Swai la kujiuliza mara nyingi huzuia maandamano eti kwasababu kunaupungufu wa askari kulinda usalama, ss jana hao polisi kwann hawakuweza kuzuia mdhara yasitokee?
unampiga risasi asiye na hatia eti anazui kumshika mwalifu kwann usimpige huyo mwalifu anayetoroka kwanza?
Aibuu kuu kwa serikali!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Inawezekana kabisa mtoa mada anasema ukweli,japo sababu za hao wakenya isiwe sahihi.Mimi hainiingii akilini,Askari aliyevaa sare,mchana,atupe bomu la kuua watu na kujeruhi wengine Sabini???????????,Kama ilikuwa lazima awe polisi kwanini asiwe Askari kanzu??????,kwanini asitumie gari la kiraia,inamaana walitaka kujitambulisha kuwa wao polisi ndio waliouwa??????haiingii akilini wakuu????
 
Manyerere,
Kwanza kabisa niseme inapofikia mahali wananchi wakawaida wana speculate ujue hapo kuna serious intelligence failure.

Huko nyuma Tanzania ilikuwa inaogopwa sana kwa intelligence yake ndio maana tuliweza kuwa salama licha ya Mreno na Kaburu kutupumulia.

Hata hapa ndani ilikuwa rahisi sana kwa wahalifu kubainika mara moja na motive ya uhalifu wao.

Ukiangalia sasa hivi tuna viporo vya mambo mengi yasiyo na majibu.
1. Suala la Mwakyembe kutaka kuuawawa kwa ushahidi wa majina na vyombo husika umetupa majibu gani?
2. Suala la Ulimboka, Mwangosi, Kibanda yana majibu gani? Tena la ulimboka akasemwa ni Mkenya yameishia wapi?
3. Suala la mengi kuwekewa madawa limeishia wapi?
4. Suala la Olaisiti kanisani hakuna jibu!

Lakini pia fikiria kwanini Arusha waliuawa watu waliokwenda kwenye mkutano siku za nyuma kabla ya tukio hili?
Je, Igunga nako Polisi walipoua tutasemaje au kule Iringa ambako Mwangosi alitolewa roho na askari wetu nako tumtafute mchawi kutoka Zambia?

Ninachotaka kusema hapa ni kuwa tusitafute sababu za ku-justify short coming zetu.
Hata kama yupo adui tatizo sio adui, tatizo ni intelligence failure kubwa sana kuliko wakati wowote wa uhuru wetu.

Endapo tungekuwa na jibu moja kati ya hayo niliyosema basi tungeweza kuangaza pembeni.
Hilo silo na hivyo tatizo ni letu wala sidhani Kenya wanahusika.
Wanahusika vipi wakati padre kapigwa risasi,. sheikh kamwagiwa tindikali na hakuna aliyewajibika?

Kama serikali haijui tatizo lipo wapi basi hilo ndilo tatizo na wala si mabomu.
Nchi hii yenye miaka 50 na iliyopita katika nyakati ngumu kushindwa kujua nani wako nyuma ya hili ni intelligence failure ya kutisha na hatari kubwa sana.

Kama serikali yenye intelligence unit zote imesimama mbele na kutoa ushuhuda kama ule wa sinema ya Kova, ule wa Lukuvi na Ule wa Mulugo unategemea kitu gani.

Manyerere haya hayakuanza leo, intelligence failure imeshindwa kuanzia Dowans, Meremeta, Richmond,Pesa za radar,green so and so on. Leo tudhani kuwa failure za intelligence yetu ni matokeo ya Wakenya! I can't buy that.

Kipi ambacho unaweza kutuwekea hapa kama kazi ya intelligence katika miaka 8 iliyopita zaidi ya kupiga mabomu wapinzani wa siasa.

Tusiondoe jicho kwenye ukweli, hii ni intelligence failure inayosabababishwa na weak leadership ya nchi hii.
The buck stops wiith JK na ingekuwa kwa wenzetu intelligenece failure inatosha kabisa kumpunzisha mwenye dhamana.

cc. JokaKuu, Manyerere Jackton
 
Jaribio lolote la kuwatuhumu wakenya kuwa wamehusika kulipua mabomu Arusha ni kujaribu kuonyesha baadhi yetu tulivyochoka kushughulisha vichwa vyetu.
Waliokuwepo uwanjani soweto wameshuhudia kuwa polisi ndio walirusha bomu, ndio walipiga hovyo risasi za moto na hivyo kuua na kujeruhi watu, hata mtoto mdogo ameshuhudia kuwa alipigwa risasi na poolisi.
Manyerere Jackton usdhani watu wamelala hapa kwamba unaweza kuwalisha mzoga kirahisi. Jipange uje kivingine kwani kastika hili ccm wanahusika zaidi ya asilimia mia moja!
 
Last edited by a moderator:
Hakuna lolote la wakenya hapo. Wewe manyerere jackton unajulikana kwa kulamba viatu vya lowasa.

Suala hapo ni CCM kutoamini wala kukubali kwamba jiji la Arusha kuwa chini ya serikali ya Chadema.
 
Kwa kweli uchambuzi huu ni makini hii naikubali ndiyo akili pevu.kubwa sasa ni watanzania tuwe na mtizamo wa mbali ili tuweze kuidumisha Amani tuliyo nayo kwani ikishaondoka kuirudisha siyo rahisi
 
ooops....u need to shapen ur analytical skills.
 
Inawezekana kabisa mtoa mada anasema ukweli,japo sababu za hao wakenya isiwe sahihi.Mimi hainiingii akilini,Askari aliyevaa sare,mchana,atupe bomu la kuua watu na kujeruhi wengine Sabini???????????,Kama ilikuwa lazima awe polisi kwanini asiwe Askari kanzu??????,kwanini asitumie gari la kiraia,inamaana walitaka kujitambulisha kuwa wao polisi ndio waliouwa??????haiingii akilini wakuu????
mechi uliyoiona ni rahisi kuifanyia tathimini kuliko mechi uliyosimuliwa sasa tabu waliosimuliwa wanajifanya mabingwa wa tadhimini,Mimi ningeomba tujirekeze kwa nn polisi waliua kwa namna ile
 
kutambua elimu ya mtu ni rahisi tu. moja ya mbinu ni pale mtu anapoamua kumshambulia mwingine bila kujielekeza kwenye hoja. jamhuri linasomwa na watu makini wanaohangaisha vichwa ktk kufikiri. halina wasomaji wa mihemko na jazba. wenye akili wote kwenye matukio ya arusha lazima wake na 5W's + 1H katika kupata nani mhusika. kunishambulia kwa mtazamo wangu ni kuonyesha jazba na majibu ya mkato. jadili hoja, basi.

Manyerere so kwamba umeshambuliwa ila ni kwamba wewe umetoa uzi ambao ni hydra headed na kuruhusu kuwa exposed kiasi kwamba anyone can interpret you in picture you are or you are not. Umejikita kwenye hisia na kuacha kuangalia udhaifu wetu kama Watanzania. You are ignoring some facts that have architect frictions among Tanzanians who knew nothing but peace, neighborhood, fraternity and the likes. Wakenya ndio wametuma baadhi yab Watanzania kuua albino ili wapate utajiri, kuua vikongwe kwa kisingizio cha uchawi, pot wenzako wauawe na kemikali kutokana na maji ya mto Teheti wakati serkali ipo, polisi waue wafanya biashara ya madini wa Mahene, Kenya walimuua Mwangozi, Kenya walimteka Kibanda, Kenya waliwatuma Nape, Mwigulu na Wassira kuwachagulia Wachaga kuwa chama chao ni CDM. Wakenya wamewatuma CCM kusema CDM Chama cha Wakristo tena Wakatholick? Wakenya wameituma serikali kujenga majengo kama madarasa na kuyasajiri kama sekondari lakini wakazinyima mahabara, maktaba, walimu, vitabu na vitendea kazi nyingine? Wakenya walitutuma kuingia mikataba ya kilaghai? Wakenya wanatutuma kuharibu mazingira? Wewe unatoka mpakani mwa Kenya na Tanzania. Ukitoka Kenya ni kijani kibichi pamoja na miti mingi na ukivuka Tanzania Sirari ni nyasi tu miti hakuna, Namnaga kuja Aruaha vivyohivyo, kule IMO na Horiri vivyo hivyo na zaidi soma makala za Mbwambo kuhusu uharibifu wa mazingira. Sasa kama haya madhaifu yanasababishwa na Wakenya naona Tanzania haipashwi kuwepo na shule tuliyosomeshwa haina maana. Kwa kweli uzi wako ni tusi kwa Watanzania kana kwamba hawana bongo. Uzi wako unafaa kufichwa mbali na watoto
 
Kwenye hili Manyerere nakusihi rudi darasani, hili halihitaji akili kubwa kulijua, mtoto ameisha shuhudia hivi, polisi ndio waliompiga risasi, matamshi ya akina Mwigulu na Mwampamba yote yanaonesha hawa jamaa walikua wamejipanga, kama unaunganisha issues za humu, unga na ile iliotoka jana humu, kua magamba hawataki kiti cha meya wa jiji la Arusha kwenda upinzani, so hata hiyo tarehe iliotangazwa, uchaguzi hautafanyika. Kwenye hili ccm na serikali hawawezi kukwepa lawama, lakini mwisho njaomba niseme hivi, kwa umri wako kaka na uzoefu wako wa kua mwanahabari wa muda mrefu, je kuna uhalifu wowote uliowahi kufanyika hapa nchi usiohusisha serikali na wahalifu hao wasikamatwe? Ngoja nikukumbushe kidogo, wizi wa pesa za iliokua Beural De change ya NBC ya zama hizo, Sarah Simbaulanga mwaka 1987, siku 3 tu baadae alikamatwa London Uingereza (Technology ya wakati huo ilikua chini sana na still walimkamata) linganisha na issue ya EPA with this technology we have, nenda tukio la kuauwa kwa RPC wa MWanza juzi, ndani ya siku 18 tayari wote waliohusika walikamatwa, linganisha na issue ya kuuawa kwa pot wako David Mwangosi na sarakasi za polisi (Assume kusingekua na picha za mnato na video) Nenda na tukio la Mwakyembe "sumu" yake and lingenisha na walichokisema akina DCI Manumba?

Naomba ku-conglude hivi, kama polisi hawahusiki, kukamata wahusika ni kazi ya wiki 1 tu, ukiona danadana, weka akili kichwani, kaka, hivi macho na ujasiri wa Nape jana na alichokua akikiongea, mbona saikolojia ilimwonesha kabisa kwamba anacho kiongea sicho anachokiamini? hata hili mzee wangu hukuona!?

Nice reminiscence...
Any comment mr Jackpot?
 
Manyerere,
This is too low my brother. Huu muda ulioutumia kuwaza na kuandika hii post, ungeutumia kuwaza na kuwazua namna ambayo ungelisaidia gazeti unaloliongoza kupanda kwa Ads na Circulation.

Analysis hovyo kabisa hii
 
Mkuu Manyerere Unachosema chaweza kuwa kweli ila tatizo kubwa linalochanganya watu ni weredi wa polisi kufanya kazi yake, hebu ona kwa mfano mabomu ya leo yana tija gani?? au tuseme polisi wanatumiwa na waKenya!!! Angalia kauli za ccm chama tawala ni upuuzi mtupu, watu wanakufa na amani inatoweka wakubwa wako busy na siasa!!!!!!!!!!! It is so sad, Miaksa imekuwa mingi hatujaona hata kesi moja wahusika wakikamatwa basi tukubali kuwa polisi na ccm wameamua kuisaliti nchi ikiwa mawazo yako ni ya kweli!!!!!!!!!!!!! ni hayo tu
 
Manyerere unajitahidi kuokoa jahazi lililokwisha zama na shehena ya unga!! Kwa.mara nyingine boss wako Lowassa ameingizwa king na wahuni mahasimu wenzake ndani ya CCM. Maneno ya pembeni ni kwamba wanataka kumwangushia jumba bovu(mauaji ya juzi).

Mmeshindwa kumshauri mapema,sasa mambo yameharibika unakuja na stori za kijinga! Nimekudharau sana!
 
Ukweli wa mambo ni huu hapa: Tusitafute mchawi hata kidogo!! Wala tusiwalaumu polisi wetu. Polisi ni kama mbwa tu wanaotimiza amri ya kuuma!!! Mwenye mbwa ndiye anayefahamu kisa na mkasa wa mbwa wake kuuma! Kikwete ndiye mratibu wa shughuli zote za mabomu makanisani na katika mikutano ya kisiasa pamoja na mauaji na utesaji unaoendelea sasa katika Tanzania!!! Huu ndio ukweli. Full stop!! Mwenye masikio ya kusikia na asikie!
 
Back
Top Bottom