Mabilioni yakusanywa kumwangusha Kikwete

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,007
Mabilioni yakusanywa kumwangusha Kikwete

Na Saed Kubenea

MwanaHALISI~Maslahi ya Taifa Mbele

RAIS Jakaya Kikwete atahitaji kutumia nguvu mara tatu kukabiliana na “genge” linalotaka kumzuia kugombea urais kwa kipindi cha pili, MwanaHALISI limeelezwa.

Taarifa zilizopatika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki zilisema, wanaotaka kumzuia Kikwete kugombea urais kwa kipindi cha pili, wamepanga kutumia, na tayari wamekusanya Sh. 2.5 bilioni kwa shughuli hiyo.

“Hizi si fedha kidogo. Lazima CCM ijipange kutumia mara tatu zaidi (Sh. 7.5 bilioni) kama inataka Kikwete apite,” ameeleza mpasha habari.

Fedha za wanaompinga Kikwete zinalenga kununulia magari, pikipiki, baisikeli, sare – suruali, fulana, khanga na kapelo; mabango na vipeperushi.

Nyingine zimepangwa kutumika katika ununuzi wa mafuta kwa ajili ya magari, posho za wapigadebe na “takrima” kwa wabunge ambao wataamua kuwaunga mkono kwa kuchomoka kwenye mkondo mkuu wa CCM.

Wiki iliyopita, aliyekuwa mwenyekiti wa mkoa wa Dar es Salaam, Hemed Mkali, aliliambia gazeti la NIPASHE kuwa lazima kila juhudi ifanywe “kuzima mahangaiko ya wanaotaka kugombea urais” mwaka 2010 vinginevyo CCM itaangamia.

Mkali alikuwa akisisitiza hoja ya wastaafu wa CCM ambao siku moja kabla ya kauli yake walitahadharisha mgawanyiko ndani ya chama chao, wakisema utatokana na kugombea urais mwaka kesho.

Viongozi wengine waliotoa rai ya kuvunja “mahangaiko ya kugombea urais” ni aliyekuwa mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma, Pancreas Ndejembi, aliyekuwa mwenyekiti wa mkoa wa Iringa, Tasil Mgoda na aliyekuwa mwenyekiti wa mkoa wa Pwani, Jumanne Mangala.

Akizungumza na MwanaHALISI kwa njia ya simu juzi Jumatatu, Mkali alisema yeye na wenzake wanajua wanachosema na kwamba hawakukurupuka.

Alipotakiwa kueleza kwa undani msingi wa madai yao kuhusu waliomo kwenye mhangaiko wa urais, kwanza Mkali alisita na baadaye alieleza:

“Tunawafahamu. Wapo watu wengi. Wengine ni viongozi wa juu serikalini na ndani ya chama. Wengine ni ‘marafiki zake’ wa karibu,” alieleza Mkali.

Alipobanwa kueleza maana ya “rafiki zake,” na huyo hasa ni nani, Mkali alisema kwa sauti ya kubembeleza, “Ndugu yangu, sasa hivi niko Rufiji; si usubiri nirudi Dar es Salaam ili tuongee?”

Taarifa zaidi zinasema Mkali na wenzake, baada ya kuongea na waandishi wa habari juu ya dukuduku lao, walikwenda nyumbani kwa kiongozi mmoja mstaafu na kumweleza kuwa walikuwa na ushahidi tosha juu ya kile walichokuwa wakisema.

Haijafahamika iwapo wastaafu waliagizwa na baadhi ya viongozi wa CCM au serikali ili kuvunja ukimya juu ya kinachoendelea; lakini kwa nafasi yao ya sasa hawakutegemewa kuwa na maslahi ya kuwafanya kuwa mstari wa mbele.

Wiki moja kabla ya wastaafu kuvunja kimya, makamu mwenyekiti mstaafu na mjumbe wa kudumu wa Kamati Kuu ya CCM, John Samwel Malecela alisema wanaotaka kuchuana na Kikwete kutoka ndani ya chama hicho wanajisumbua.

Aliwaambia waandishi wa habari, nyumbani kwake Sea View, Dar es Salaam kuwa mgombea wa CCM mwaka 2010 ni Jakaya Mrisho Kikwete.

Kauli ya Malecela na zile za wenyeviti wa mikoa wastaafu, haziwezi kuwa mlolongo wa porojo mitaani bali majibu kwa kile ambacho kinachemka ndani ya nyoyo na vikao vya siri vya wanachama na viongozi.

Gazeti hili liliandika Oktoba mwaka jana kuwa kulikuwa na njama za kumg’oa Kikwete. Lilifungiwa kwa siku 90 kwa madai ya wizara ya habari kwa akile kilichoitwa kufanya “uchochezi.”

Toleo Na. 118 la MwanaHALISI liliandika kuwa watuhumiwa wa ufisadi nchini walikuwa wamejipanga kumg’;oa Rais Kukwete ili asigombee urais mwaka 2010.

Gazeti lilinukuu taarifa zilizosema wapinzani wa Kikwete walikuwa wanataka kumfanya awe “One-Term President” – rais wa kipindi kimoja, lengo likiwa kumwadhibu kwa kile kilichoitwa kuwasahau wenzake na kutowatetea walipoingia katika matatizo.

Tangu hapo, vyombo vya habari mbalimbali, yakiwemo magazeti ya serikali na CCM, vimeandika juu ya njama za “kumzuia Kikwete kugombea urais” Oktoba mwaka kesho.

Mbunge wa Maswa ambaye alijitosa katika kinyang’anyiro cha urais mwaka 2005 na kushindwa katika hatua za awali, John Shibuda tayari ametangaza kumpinga Kikwete katika uchaguzi mwakani.
 
..bora tungeelezwa Kikwete alitumia billioni ngapi kuutafuta Uraisi from 95 mpaka 05 alipoupata.

..vilevile Kikwete ana mpango wa kutumia billioni ngapi kutetea nafasi yake 2010?
 
Hao wanaotaka kumpinga Kikwete naombea waendelee na dhamira yao hiyohiyo mpaka mwisho tuone kina Malecela watakuwa na ubavu wa kuwazuia.Waache waparuane na kama kugawanyika sisi walalahoi tunasema hewala!
 
Hao wote wanajuana na umeshasikia ni marafiki zake .....sisi tukae kimya??maana watatuwekea fmgombea fisadi au anewabeba mafisadi....kwa kweli kama BWM angekuwa uwezo kuwazuia mtandao...na kuweka mtu wake nadani nchi ingetawalika.mm-la sababu mtandao una nguvu kubwa na pesa....awa jamaa watatuchagulia rais for the next 20 yrs....
 
Upinzani ya ccm unaweza kuja pale tu wachache wataona inawezekana wakauchukua uraisi! Bado navuta pumzi na subira, mpaka hapo nitakapoona majina ya wagombea ndani ya ccm
 
Kitu ambacho kimefichwa katika habari hii ni kuwa je ni akina nani hasa?

1. Je ni mafisadi kama ambavyo kubenea ameshawahi kueleza huko nyuma??
2. Je ni watu safi ambao wanataka mabadiliko ndani ya CCM?

Taarifa kama hii inabidi iwe na closer look, kwani mara nyingi nimeshuhudia watu wakisema mafisadi wana njama ya kumwondoa JK , wakati in other hand ni mbinu ya kumfanya Kikwete aendelee na madaraka, kwa kuwadanganya watanzania kuwa JK ni masfi na anawapinga mafisadi, wakati yeye na mafisadi ni baba mmoja na mama mmoja!

Kubenea may be sijaelewa taarifa yako, lakini acha nichukiwe, kwa hali ya uangalifu sana umekuwa ukimfagilia kikwete, watu wameona na rumors za kuwa hilo gazeti ni la JK, liko kuwakomoa makundi mengine ya mafisadi wakati wao wenyewe ni mafisadi!

by the way kesi yako imeishaje, polisi haijawapata tu waliokumwagia tindikali?????
 
Waberoya,
Ukiisoma taarifa kwa makini na fedha walizokwishakusanya jibu litakuwa moja tu: ni mafisadi ambao wanaona mwenzao Kikwete amewatupa au kuwatema. Hii si dalili njema kwa nchi.
 
Kitu ambacho kimefichwa katika habari hii ni kuwa je ni akina nani hasa?

1. Je ni mafisadi kama ambavyo kubenea ameshawahi kueleza huko nyuma??
2. Je ni watu safi ambao wanataka mabadiliko ndani ya CCM?


Waberoya, kwa maoni yangu walio safi ndani ya CCM ni wachache sana na hawana ubavu wowote ndani ya chama hicho maana chama kimeshashikwa na mafisadi. Sasa mafisadi wanapambana wenyewe kwa wenyewe. Inasemekana kuanzia jana kulikuwa na vikao vya juu vya CCM ambavyo vitaendelea hadi J'tatu, kwa maoni yangu hakutakuwa na jipya lenye maana yoyote bali ni USANII MTUPU!!!
 
Naona Kubenea hapa naye ni jitihada ya kuuza gazeti lake kwa kuweka habari ambayo si ajabu haina ukweli kabisa.

Siamini kabisa kuna kundi la maana ndani ya CCM linataka kumpinga JK hapo 2010.

Kinachoendelea sasa ni watu kuandika mambo kwa hisia na kwasababu hawawajibiki kutoa ushahidi basi wanaendeleza lile lile gumzo la kwenye vijiwe.

Ni mambo yale yale ya mwaka 2005 kwamba Malecela kachukua pesa Iran, kabadili dini nk. Baadaye ikaja onekana ulikuwa utumbo mtupu.

Tusubiri hiyo 2010 na tuone kama hizi habari zina ukweli wowote zaidi ya kuweka vichwa vya habari ambavyo ni rahisi kuuzika mitaani.

Kwa anayejua jinsi CCM wanavyochagua rais, sioni kwa vipi mtu anayetaka kushinda urais anaweza kumshinda JK kwenye kamati kuu ya CCM?

Nawasifu thisday kwa kuwa muda wote wanatanguliza facts kabla ya kuja na conclusions, tofauti na haya magazeti mengine ambayo yanajenga hoja kwa foundation mbovu kabisa.

2010 si mbali na tutajua tu.
 
Siamini kabisa kuna kundi la maana ndani ya CCM linataka kumpinga JK hapo 2010.

Kwa hiyo unataka kutwambia kwamba wale waliojiita "Wazee wa Chama" walikurupuka tu walipotoa kauli kwamba "atakayempinga Kikwete 2010 atakiona"? Unataka kutwambia kwamba Chiligati, Msekwa na Malecela nao walikurupuka pale walipotoa kauli kwamba 2010 ni Kikwete tu maana wana Utamaduni wao wa kuachiana Rais akae vipindi viwili?

Kwa maoni yangu nadhani wanajua nini kinaendelea dhidi ya Kikwete ndiyo maana ikabidi waanze kumpigia debe la nguvu Kikwete, vinginevyo hawakuwa na sababu zozote za kutoa kauli zile.
 
Hao wote wanajuana na umeshasikia ni marafiki zake .....sisi tukae kimya??maana watatuwekea fmgombea fisadi au anewabeba mafisadi....kwa kweli kama BWM angekuwa uwezo kuwazuia mtandao...na kuweka mtu wake nadani nchi ingetawalika.mm-la sababu mtandao una nguvu kubwa na pesa....awa jamaa watatuchagulia rais for the next 20 yrs....
The Kikwete veterans have systematically discovered that every flaw associated in the public mind with their hero turns out to be a defining trait of BWM's regime. I am not a trained psychologist, but some form of projection seems to be at work in the present climate of public opinion, direct defenses of Kikwete have limited appeal, so the Kikwetean's mainly argue by implication.
 
Mabilioni yakusanywa kumwangusha Kikwete

Na Saed Kubenea

MwanaHALISI~Maslahi ya Taifa Mbele

RAIS Jakaya Kikwete atahitaji kutumia nguvu mara tatu kukabiliana na “genge” linalotaka kumzuia kugombea urais kwa kipindi cha pili, MwanaHALISI limeelezwa.

Taarifa zilizopatika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki zilisema, wanaotaka kumzuia Kikwete kugombea urais kwa kipindi cha pili, wamepanga kutumia, na tayari wamekusanya Sh. 2.5 bilioni kwa shughuli hiyo.

“Hizi si fedha kidogo. Lazima CCM ijipange kutumia mara tatu zaidi (Sh. 7.5 bilioni) kama inataka Kikwete apite,” ameeleza mpasha habari.

Fedha za wanaompinga Kikwete zinalenga kununulia magari, pikipiki, baisikeli, sare – suruali, fulana, khanga na kapelo; mabango na vipeperushi.

Nyingine zimepangwa kutumika katika ununuzi wa mafuta kwa ajili ya magari, posho za wapigadebe na “takrima” kwa wabunge ambao wataamua kuwaunga mkono kwa kuchomoka kwenye mkondo mkuu wa CCM.

Wiki iliyopita, aliyekuwa mwenyekiti wa mkoa wa Dar es Salaam, Hemed Mkali, aliliambia gazeti la NIPASHE kuwa lazima kila juhudi ifanywe “kuzima mahangaiko ya wanaotaka kugombea urais” mwaka 2010 vinginevyo CCM itaangamia.

Mkali alikuwa akisisitiza hoja ya wastaafu wa CCM ambao siku moja kabla ya kauli yake walitahadharisha mgawanyiko ndani ya chama chao, wakisema utatokana na kugombea urais mwaka kesho.

Viongozi wengine waliotoa rai ya kuvunja “mahangaiko ya kugombea urais” ni aliyekuwa mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma, Pancreas Ndejembi, aliyekuwa mwenyekiti wa mkoa wa Iringa, Tasil Mgoda na aliyekuwa mwenyekiti wa mkoa wa Pwani, Jumanne Mangala.

Akizungumza na MwanaHALISI kwa njia ya simu juzi Jumatatu, Mkali alisema yeye na wenzake wanajua wanachosema na kwamba hawakukurupuka.

Alipotakiwa kueleza kwa undani msingi wa madai yao kuhusu waliomo kwenye mhangaiko wa urais, kwanza Mkali alisita na baadaye alieleza:

“Tunawafahamu. Wapo watu wengi. Wengine ni viongozi wa juu serikalini na ndani ya chama. Wengine ni ‘marafiki zake’ wa karibu,” alieleza Mkali.

Alipobanwa kueleza maana ya “rafiki zake,” na huyo hasa ni nani, Mkali alisema kwa sauti ya kubembeleza, “Ndugu yangu, sasa hivi niko Rufiji; si usubiri nirudi Dar es Salaam ili tuongee?”

Taarifa zaidi zinasema Mkali na wenzake, baada ya kuongea na waandishi wa habari juu ya dukuduku lao, walikwenda nyumbani kwa kiongozi mmoja mstaafu na kumweleza kuwa walikuwa na ushahidi tosha juu ya kile walichokuwa wakisema.

Haijafahamika iwapo wastaafu waliagizwa na baadhi ya viongozi wa CCM au serikali ili kuvunja ukimya juu ya kinachoendelea; lakini kwa nafasi yao ya sasa hawakutegemewa kuwa na maslahi ya kuwafanya kuwa mstari wa mbele.

Wiki moja kabla ya wastaafu kuvunja kimya, makamu mwenyekiti mstaafu na mjumbe wa kudumu wa Kamati Kuu ya CCM, John Samwel Malecela alisema wanaotaka kuchuana na Kikwete kutoka ndani ya chama hicho wanajisumbua.

Aliwaambia waandishi wa habari, nyumbani kwake Sea View, Dar es Salaam kuwa mgombea wa CCM mwaka 2010 ni Jakaya Mrisho Kikwete.

Kauli ya Malecela na zile za wenyeviti wa mikoa wastaafu, haziwezi kuwa mlolongo wa porojo mitaani bali majibu kwa kile ambacho kinachemka ndani ya nyoyo na vikao vya siri vya wanachama na viongozi.

Gazeti hili liliandika Oktoba mwaka jana kuwa kulikuwa na njama za kumg’oa Kikwete. Lilifungiwa kwa siku 90 kwa madai ya wizara ya habari kwa akile kilichoitwa kufanya “uchochezi.”

Toleo Na. 118 la MwanaHALISI liliandika kuwa watuhumiwa wa ufisadi nchini walikuwa wamejipanga kumg’;oa Rais Kukwete ili asigombee urais mwaka 2010.

Gazeti lilinukuu taarifa zilizosema wapinzani wa Kikwete walikuwa wanataka kumfanya awe “One-Term President” – rais wa kipindi kimoja, lengo likiwa kumwadhibu kwa kile kilichoitwa kuwasahau wenzake na kutowatetea walipoingia katika matatizo.

Tangu hapo, vyombo vya habari mbalimbali, yakiwemo magazeti ya serikali na CCM, vimeandika juu ya njama za “kumzuia Kikwete kugombea urais” Oktoba mwaka kesho.

Mbunge wa Maswa ambaye alijitosa katika kinyang’anyiro cha urais mwaka 2005 na kushindwa katika hatua za awali, John Shibuda tayari ametangaza kumpinga Kikwete katika uchaguzi mwakani.

Sababu kuu ya kumuangusaha Mh. Kikwete ni kuwasahau na kutowatetea mafisadi!:eek: Hii kali kuliko.

Kama hakuna sababu sioni vipi hivyo vichuruku 2.5 bilioni vitaweza kumuangusha Mh. Kikwete.

Narudia, hakuna mwenye sababu kuu!
 
Kwa hiyo unataka kutwambia kwamba wale waliojiita "Wazee wa Chama" walikurupuka tu walipotoa kauli kwamba "atakayempinga Kikwete 2010 atakiona"? Unataka kutwambia kwamba Chiligati, Msekwa na Malecela nao walikurupuka pale walipotoa kauli kwamba 2010 ni Kikwete tu maana wana Utamaduni wao wa kuachiana Rais akae vipindi viwili?

Kwa maoni yangu nadhani wanajua nini kinaendelea dhidi ya Kikwete ndiyo maana ikabidi waanze kumpigia debe la nguvu Kikwete, vinginevyo hawakuwa na sababu zozote za kutoa kauli zile.

Wazee wa chama waliposema Mkapa aendelee 2000 kwani kulitokea mtu wa kumpinga? Au hamna hata kumbukumbu nini kilitokea kabla ya uchaguzi wa 2000 ndani ya CCM?

Naamini haya maneno yanaenezwa na watu ambao hawajui CCM inavyofanya mambo yake au magazeti ambayo yanataka kuuza habari.
 
Mabilioni yakusanywa kumwangusha Kikwete

Na Saed Kubenea

MwanaHALISI~Maslahi ya Taifa Mbele

RAIS Jakaya Kikwete atahitaji kutumia nguvu mara tatu kukabiliana na “genge” linalotaka kumzuia kugombea urais kwa kipindi cha pili, MwanaHALISI limeelezwa.

Taarifa zilizopatika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki zilisema, wanaotaka kumzuia Kikwete kugombea urais kwa kipindi cha pili, wamepanga kutumia, na tayari wamekusanya Sh. 2.5 bilioni kwa shughuli hiyo.

“Hizi si fedha kidogo. Lazima CCM ijipange kutumia mara tatu zaidi (Sh. 7.5 bilioni) kama inataka Kikwete apite,” ameeleza mpasha habari.

Fedha za wanaompinga Kikwete zinalenga kununulia magari, pikipiki, baisikeli, sare – suruali, fulana, khanga na kapelo; mabango na vipeperushi.

Nyingine zimepangwa kutumika katika ununuzi wa mafuta kwa ajili ya magari, posho za wapigadebe na “takrima” kwa wabunge ambao wataamua kuwaunga mkono kwa kuchomoka kwenye mkondo mkuu wa CCM.

Wiki iliyopita, aliyekuwa mwenyekiti wa mkoa wa Dar es Salaam, Hemed Mkali, aliliambia gazeti la NIPASHE kuwa lazima kila juhudi ifanywe “kuzima mahangaiko ya wanaotaka kugombea urais” mwaka 2010 vinginevyo CCM itaangamia.

Mkali alikuwa akisisitiza hoja ya wastaafu wa CCM ambao siku moja kabla ya kauli yake walitahadharisha mgawanyiko ndani ya chama chao, wakisema utatokana na kugombea urais mwaka kesho.

Viongozi wengine waliotoa rai ya kuvunja “mahangaiko ya kugombea urais” ni aliyekuwa mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma, Pancreas Ndejembi, aliyekuwa mwenyekiti wa mkoa wa Iringa, Tasil Mgoda na aliyekuwa mwenyekiti wa mkoa wa Pwani, Jumanne Mangala.

Akizungumza na MwanaHALISI kwa njia ya simu juzi Jumatatu, Mkali alisema yeye na wenzake wanajua wanachosema na kwamba hawakukurupuka.

Alipotakiwa kueleza kwa undani msingi wa madai yao kuhusu waliomo kwenye mhangaiko wa urais, kwanza Mkali alisita na baadaye alieleza:

“Tunawafahamu. Wapo watu wengi. Wengine ni viongozi wa juu serikalini na ndani ya chama. Wengine ni ‘marafiki zake’ wa karibu,” alieleza Mkali.

Alipobanwa kueleza maana ya “rafiki zake,” na huyo hasa ni nani, Mkali alisema kwa sauti ya kubembeleza, “Ndugu yangu, sasa hivi niko Rufiji; si usubiri nirudi Dar es Salaam ili tuongee?”

Taarifa zaidi zinasema Mkali na wenzake, baada ya kuongea na waandishi wa habari juu ya dukuduku lao, walikwenda nyumbani kwa kiongozi mmoja mstaafu na kumweleza kuwa walikuwa na ushahidi tosha juu ya kile walichokuwa wakisema.

Haijafahamika iwapo wastaafu waliagizwa na baadhi ya viongozi wa CCM au serikali ili kuvunja ukimya juu ya kinachoendelea; lakini kwa nafasi yao ya sasa hawakutegemewa kuwa na maslahi ya kuwafanya kuwa mstari wa mbele.

Wiki moja kabla ya wastaafu kuvunja kimya, makamu mwenyekiti mstaafu na mjumbe wa kudumu wa Kamati Kuu ya CCM, John Samwel Malecela alisema wanaotaka kuchuana na Kikwete kutoka ndani ya chama hicho wanajisumbua.

Aliwaambia waandishi wa habari, nyumbani kwake Sea View, Dar es Salaam kuwa mgombea wa CCM mwaka 2010 ni Jakaya Mrisho Kikwete.

Kauli ya Malecela na zile za wenyeviti wa mikoa wastaafu, haziwezi kuwa mlolongo wa porojo mitaani bali majibu kwa kile ambacho kinachemka ndani ya nyoyo na vikao vya siri vya wanachama na viongozi.

Gazeti hili liliandika Oktoba mwaka jana kuwa kulikuwa na njama za kumg’oa Kikwete. Lilifungiwa kwa siku 90 kwa madai ya wizara ya habari kwa akile kilichoitwa kufanya “uchochezi.”

Toleo Na. 118 la MwanaHALISI liliandika kuwa watuhumiwa wa ufisadi nchini walikuwa wamejipanga kumg’;oa Rais Kukwete ili asigombee urais mwaka 2010.

Gazeti lilinukuu taarifa zilizosema wapinzani wa Kikwete walikuwa wanataka kumfanya awe “One-Term President” – rais wa kipindi kimoja, lengo likiwa kumwadhibu kwa kile kilichoitwa kuwasahau wenzake na kutowatetea walipoingia katika matatizo.

Tangu hapo, vyombo vya habari mbalimbali, yakiwemo magazeti ya serikali na CCM, vimeandika juu ya njama za “kumzuia Kikwete kugombea urais” Oktoba mwaka kesho.

Mbunge wa Maswa ambaye alijitosa katika kinyang’anyiro cha urais mwaka 2005 na kushindwa katika hatua za awali, John Shibuda tayari ametangaza kumpinga Kikwete katika uchaguzi mwakani.

Wale wazee kumbe wanajibizana na watu. Safari hii hawana EPA?
 
Wazee wa chama waliposema Mkapa aendelee 2000 kwani kulitokea mtu wa kumpinga? Au hamna hata kumbukumbu nini kilitokea kabla ya uchaguzi wa 2000 ndani ya CCM?

Naamini haya maneno yanaenezwa na watu ambao hawajui CCM inavyofanya mambo yake au magazeti ambayo yanataka kuuza habari.

2000 hatukusikia kauli kutoka kwa "Wazee wa Chama" ya "atakayempinga Mkapa 2000 atakiona" lakini mwaka huu tumeisikia ya kuhusiana na Kikwete na nina hakika kabisa kwamba "Wazee wa Chama" wasingekurupuka tu from nowhere na kutoa kauli ambayo inaelekea ilikuwa inamlenga kumtisha mtu mmoja ndani ya CCM au kundi la Watu ndani ya CCM. Pia 2000 hatukusikia kauli za 'Ni Mkapa tu 2000'

Kuna kitu chini kwa chini ndiyo maana kauli hizi zinatolewa, haiwezekani kauli hizi zitolewe bila sababu yoyote maana siku zote panapofuka moshi hapakosi.....
 
Mwaka 2010 ni wananchi kuamua kama wanamtaka JK au, haina haja ya JK kuogopa wapinzania kama anajiamini maana kama hana tatizo hana sababu ya kuogopa kwani wananchi watamchagua.

Wajibu wa JF na vyombo vya habari vingine ni kuakikisha kuwa wananchi wanatumia nafasi yao ya kula vizuri na kuwapa viongozi wazuri
 
Hamna lolote. Hii ni kuuza magazeti tuu ama watu wanajenga hoja zisizo na miguu wala kichwa. Najua wale wazee wa Zipompapompa sasa hivi wanajipanga kwaaajili ya 2015 ndio maana vikao haviishi ila sasa kinachowaumiza kichwa ni kwamba JK atamkabidhi nani kati yao maana anaweza kuwatosa wote vile vile.
 
Dalili moja kubwa ya kufikia mwisho wa mfumo Dume kama wa CCM ni kuzaliwa kwa mapambano ya ndani kwa ndani.
Kipimo kile kile walozoea kuwapimia wakulima na wafanyakazi wa Tanzania sasa watapimiana wenyewe na kulazimishana kunywa.

Zoezi hili tunaliombea lidumu hadi mwisho wa ukomo wa utawala wao wa Kimaruk.
 
Waberoya,
Ukiisoma taarifa kwa makini na fedha walizokwishakusanya jibu litakuwa moja tu: ni mafisadi ambao wanaona mwenzao Kikwete amewatupa au kuwatema. Hii si dalili njema kwa nchi.

Mtu akitupwa nje ya mduara wa Kikwete ni Adui wa nchi??

Waliomo ndani ya mduara wa MH huyu ni watu Safi?

Kikwete mwenyewe ni safi??

CCM ni safi?

Kundi lipi katika hayo mawili ni safi?

Hitimisho kwamba hii si dalili nzuri kwa nchi umellifikiaje?

Ni kwa sababu ya kitendo cha Muungwana kukatiziwa muda wake wa kukaa Ikulu??

Ni kweli CCM ikitoweka uwepo wa nchi uko mashakani au waliozoea kunyonga watashindwa kula vya kuchinja????
 
Hitimisho kwamba hii si dalili nzuri kwa nchi umellifikiaje?

Madilu, hapa mimi naspeculate naweza kabisa nisiwe sahihi. Nadhani Jasusi aliandika vile kwa sababu wakati wa mapambano ndani ya makundi yaliyopo ndani ya CCM yakiendelea nchi itakuwa haina uongozi kama tunavyoona sasa. Nguvu zote na mabilioni ya pesa yatakuwa yamehamishiwa katika mapambano hayo makali na kila kundi likitaka kuibuka na ushindi ili waweze kuweka mgombea wao 2010.
 
Back
Top Bottom