Kalunya
JF-Expert Member
- Oct 5, 2021
- 13,324
- 18,478
Vijijini kwetu kuni bure au gesi bei juu kuliko kuni na mkaa.Sekta kibao ziko wazi mfano gesi ya kupikia nilikuwa Ghana vijijini watu kusiko na barabara wanapeleka mitungi kwa punda sababu magari ya kampuni za gesi hayafiki kule !!! Wamejiongeza .Hapa kwetu gesi biashara mwisho miji mikubwa .Jeshi laweza ishika miji midogo karibu na kambi zao wakaweka maduka ya bei jumla ya majiko ya gesi ya kupikia wakawapa biashara bodaboda wakachukua maduka hayo jirani na kambi na kwenda kuuza rejareja huko ndani ndani vijijini kwa walimu,wakulima,nk kwa kuwapelekea majumbani au kujifungulia viduka vidogo vijijini vya maduka ya Gesi
Kampuni za gesi bado hazijawafikia watu wote kampuni za gesi zaweza pia mikataba ya kibiashara na JWTZ wao wana nagari yawezayo fika popote porini kwenye wateja
Kampuni za gesi ya kupikia zichukue hii kama opportunity ya kufikisha bidhaa zao remote areas kusikofikika na magari yao
Kama soda na bia zinafika KILA kijiji sembuse gas.
Bodaboda zimefungua vijiji.
Zamani hadi ufike kijijini unatumia wiki kufika.
Uhitaji wa gas vijijini si Mkubwa kuliko mijini usafiri sio tatizo.