Mabati ya ALAF yako overated sana

Mabati ya ALAF yako overated sana

Binafsi mm nalikubali bati la ALAF na ndilo nililoezekea nyumba na nilienda kuchukuwa kiwandani kwa vipimo nilivyokuwa navihitaji, asikwambie mtu bati lina miaka minne kasoro lakini utaliona chafu kipindi cha kiangazi kama lina vumbi hivi sasa ngoja mvua inyeshe utadhani ngozi ya nyoka mweusi🙂🙂🙂

Nimeezekea versetile rangi Chacoal grey! Nilipata na wasaa wa kuingia kiwandani asikwambie mtu material yanavyobadilishwa kuwa bati ni hatari na sheet inazungushwa umbali mrefu kabla ya kuanza kukatwa na mbaya zaidi nikaambiwa hicho kiwanda kilikuwa cha serikali enzi za Nyerere!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Nikahuzunika.
 
Kuna njia nyingi sana zakufanya utafiti,kwakifupi jamaa amefikia hatua yakuezeka sasa kwastory anazozipata kila mmoja anasifia ALAF kwaiyo yy amekuja kivingine ili apate uhakika zaid ya anachokisikia mtaani ili aweze kuchukua maamuz sahihi. Big up mkuu you're great thinker
 
Mleta maada ni muuongo sana, Alafu ni level za juu, huwezi linganisha na wengine.
Mm nimebahatika kutumia bati zao na pia za kapuni zingine, mpaka sasa nabaki na Alafu
 
ALAF wapo vzr mkuu kinachowasumbua wengi nigarama zao ila nivyema ujichange uchukue kitu chakueleweka kuliko kuchukua zabei rahisi thn mwakan tu unarud kuanzisha uzi wakushauriwa rangi nzur yakupaka kwene Bati
 
we!!we!!! labda hujawahi kujenga, na kama hujawahi kujenga hujatembelea kwenye majengo ya watu ukaona jinsi mabati ya kampuni nyingine yalivyopauka kama ngozi ya kenge? asikudanganye mtu kwa bongo bati ni ALAF tu
Mkuuu umemaliza kila kitu, anakuja na stori za vijiwe vya kahawa anataka tumwamini.
 
Inategemea na kampuni,kuna jamaa yangu alipaua na bati za kampuni 1 ya wachina inaitwa eagle,unaenda mwaka wa 3 bati ziko vile vile,jirani yake alipaua na alaf,ngoja niishie hapa kwa leo
Si kweli ndugu angalia mabati ya kampuni zingine yanavyo pauka paa linakuwa na mabakamabaka ndani ya mwaka mmoja tu.
 
Sidhani kama umefanya utafiti, ALAF wapo vizuri sana kulinganisha na products nyingi sana za mabati. Angalia nyumba zilizopauliwa kwa products za ALAF compare na zile za kampuni zingine, nakupa mwaka mmoja tu wa kufanya research yako, then njoo na jibu hapa.

Kuna Dragon, Sunshare, Simba..etc. fanya utafiti kidogo.
 
Jaman vp kuhusu SUNSHARE nayo je yanalingana na ALAF????
Wapo vizuri japo sidhani kama wanafika level ya ALAF. Ikipita miaka mitatu nitajua kama wapo sawa au vipi, ni mwaka wa pili na sijaona tatizo kwenye ubora wao.
 
Hapo kwa Simba Sc. Naunga mkono hoja. Teh Teh Teh.
Vitu vingi mkuu vipo over rated yaan mpaka unashangaa sifa zote zile kumbe hali halisi ndio hii? Papuchi ipo over rated Simba SC ipo over rate n.k n.k
 
Binafsi mm nalikubali bati la ALAF na ndilo nililoezekea nyumba na nilienda kuchukuwa kiwandani kwa vipimo nilivyokuwa navihitaji, asikwambie mtu bati lina miaka minne kasoro lakini utaliona chafu kipindi cha kiangazi kama lina vumbi hivi sasa ngoja mvua inyeshe utadhani ngozi ya nyoka mweusi🙂🙂🙂 Nimeezekea versetile rangi Chacoal grey! Nilipata na wasaa wa kuingia kiwandani asikwambie mtu material yanavyobadilishwa kuwa bati ni hatari na sheet inazungushwa umbali mrefu kabla ya kuanza kukatwa na mbaya zaidi nikaambiwa hicho kiwanda kilikuwa cha serikali enzi za Nyerere!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Nikahuzunika.
Bati kuzungushwa mbali mrefu siyo issue, ni suala LA Technology mkuu.
 
Si kweli ndugu angalia mabati ya kampuni zingine yanavyo pauka paa linakuwa na mabakamabaka ndani ya mwaka mmoja tu.
Inategemea 'sheet' ya bati ambayo inakuwa kwenye 'roller' wamechukulia nchi gani;India,china ,Africa kusini n.k hawa wenye viwanda wanachokifanya ni kuweka mikunjo na kukata saizi wanayotaka.kuhusu rangi,uimara n.k inategemea huko nje walikochukulia hizo 'sheet'
 
Embu leteni variaties ya bati na garama zake. Binafsi natafakari ains gani za bati nikayotumia kuezekea lakin unafuu wa bei kuzingatiwa
 
Back
Top Bottom