issenye
JF-Expert Member
- Feb 2, 2011
- 3,795
- 5,255
Kipi kizuri, ulale morogoro kisha ufike salama kesho yake au uruhusiwe kusafiri usiku halafu uvamiwe na majambazi, au kupata ajali usiku, (kumbuka usiku ndio wakati gari za mizigo zinasafiri pia madereva wanakuwa wamechoka)Wanajamvi, imekuwa ni jambo la kawaida kwa mabasi kutoka Mwanza Tukuyu Songea Mwanza Kigoma kuzuiliwa Morogoro.
Pamoja na nia nzuri ya usalama lakini abiria wanateseka sana hasa ukizingatia kipindi hiki gharama za maisha Imekuwa juu.
Jana nilikuwa mhanga baada ya kukwama mji kasoro bahari nikitokea Mwanza.
Nadhani sasa wadau ni wakati muafaka wa kufuta safari za moja kwa moja kutoka katika hiyo mikoa ili abiria ajue kabisa kwamba atalala njiani.
Nawasilisha wakuu kwa mawazo yenu ju ya jambo hili.