Mabasi kutoka mikoa ya mbali kulala Morogoro

Mabasi kutoka mikoa ya mbali kulala Morogoro

Nkungulume

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2015
Posts
2,987
Reaction score
1,210
Wanajamvi, imekuwa ni jambo la kawaida kwa mabasi kutoka Mwanza Tukuyu Songea Mwanza Kigoma kuzuiliwa Morogoro.

Pamoja na nia nzuri ya usalama lakini abiria wanateseka sana hasa ukizingatia kipindi hiki gharama za maisha Imekuwa juu.

Jana nilikuwa mhanga baada ya kukwama mji kasoro bahari nikitokea Mwanza.

Nadhani sasa wadau ni wakati muafaka wa kufuta safari za moja kwa moja kutoka katika hiyo mikoa ili abiria ajue kabisa kwamba atalala njiani.

Nawasilisha wakuu kwa mawazo yenu ju ya jambo hili.
 
Poleni sana,kwahyo hua hamuogi kabisa?mtafanana hivi hivi.pollen sana
 
Wana jamvi imekuwa ni jambo la kawaida kwa mabasi kutoka Mwanza Tukuyu Songea Mwanza Kigoma kuzuiliwa Morogoro.

Pamoja na nia nzuri ya usalama lakini abiria wanateseka sana hasa ukizingatia kipindi hiki gharama za maisha Imekuwa juu.
Jana nilikuwa mhanga baada ya kukwama mji kasoro bahari nikitokea Mwanza.
Nadhani sasa wadau ni wakati muafaka wa kufuta safari za moja kwa moja kutoka katika hiyo mikoa ili abiria ajue kabisa kwamba atalala njiani.

Nawakilisha wakuu kwa mawazo yenu ju ya jambo hili.
Labda mlichelewa kufika Moro, sio lazima kulala.
 
Wana jamvi imekuwa ni jambo la kawaida kwa mabasi kutoka Mwanza Tukuyu Songea Mwanza Kigoma kuzuiliwa Morogoro.

Pamoja na nia nzuri ya usalama lakini abiria wanateseka sana hasa ukizingatia kipindi hiki gharama za maisha Imekuwa juu.
Jana nilikuwa mhanga baada ya kukwama mji kasoro bahari nikitokea Mwanza.
Nadhani sasa wadau ni wakati muafaka wa kufuta safari za moja kwa moja kutoka katika hiyo mikoa ili abiria ajue kabisa kwamba atalala njiani.

Nawakilisha wakuu kwa mawazo yenu ju ya jambo hili.
Lipo sawa tu.

Wanapunguza ajali, bora uteseke kwa kulala barabarani kuliko kwenda mwendo kasi na kuhatarisha maisha.
 
Lipo sawa tu.

Wanapunguza ajali, bora uteseke kwa kulala barabarani kuliko kwenda mwendo kasi na kuhatarisha maisha.
Yah! Huwa inasaidia kuwafanya madereva wapimzike kidogo kuliko kulazimisha kufika mwisho wa siku ajali zinazidi kutumaliza, nadhan si jambo baya kwa upande wangu.
 
Huu no upuuzi tu wa kitanzania, huwezi kutengeneza 24hrs economy kwa kulaza watu njiani, polisi wafanye kazi yao waweke road blocks kila baada ya umbali fulani, nchi ya amani ya nchi hii na barabara zilivyoboreshwa kuwaambia watu walale njiani ni kudharau intelligence ya watanzania inamaanisha hawawezi kujisimamia kuanzia serikali yenyewe hadi watumia Barabara.
 
Acha walale tu, maana abiria na abiria wao wote hawajielewi, gari zinakimbizwa sana likishaanza giza abiria wapo kimya ila gari ikipata ajari ndio wanaanza kupiga kelele dereva alikuwa anakimbia sana
 
Ni wazo zuri ila kama mtanzania mwenzangu nakukumbusha tu, hatuna mikoa inaitwa Tukuyu na Songea. Siku nyingine tafuta majina sahihi ya mikoa na hii si kwa faida yako tu, bali kwa walio bado kwenye elimu msingi
Safi sana, Tukuyu ipo Mbeya na Songea ipo Ruvuma
 
Wanajamvi, imekuwa ni jambo la kawaida kwa mabasi kutoka Mwanza Tukuyu Songea Mwanza Kigoma kuzuiliwa Morogoro.

Pamoja na nia nzuri ya usalama lakini abiria wanateseka sana hasa ukizingatia kipindi hiki gharama za maisha Imekuwa juu.

Jana nilikuwa mhanga baada ya kukwama mji kasoro bahari nikitokea Mwanza.

Nadhani sasa wadau ni wakati muafaka wa kufuta safari za moja kwa moja kutoka katika hiyo mikoa ili abiria ajue kabisa kwamba atalala njiani.

Nawasilisha wakuu kwa mawazo yenu ju ya jambo hili.


Kwani ni lazima ushuke kwenye basi? Hauwezi kulala humo humo?
 
Back
Top Bottom