Mdude_Nyagali
Member
- Dec 11, 2022
- 60
- 1,237
Mabadiliko kutoka π½ππππΏπππ π½πππππ ππππππππ - π½π½π mpaka kuwa π½ππππΏπππ π½πΌπππ ππππππππ- π½π½π. TUMEPIGWA BILIONI 13.
Kwa mujibu wa wizara ya Kilimo chini ya waziri @HusseinBashe ni kwamba serikali inatumia milion 16.4 kufadhili shamba la hekta moja kwenye mradi wa Building a Better Tomorrow kwa kifupi BBT. Gharama hizi hazina uhalisia wowote kwa mtu anayejua kilimo au mkulima yoyote. Na kama zingekuwa na uhalisia kwamba mkulima anaweza kutumia milioni 16 kuandaa shamba la hekta moja ambayo ni sawa na ekari mbili basi nchi hii hakuna ambaye angemudu gharama hizo.
Fikiria unalima nini kwenye shamba la hekta moja ambalo maandalizi yake mpaka kupanda mbegu yanagharimu milioni 16? Unalima dhahabu kwenye hilo shamba? Au unalima almasi? Ama tanzanite? Maana haiwezekani shamba lililoandaliwa kwa milion 16 upande mahindi, Mpunga au ulezi halafu utegemee mtaji wako milioni 16 kurudi achilia mbali kupata faida.
Naomba kujitolea mfano mwenyewe maana ni mkulima. Msimu wa kilimo uliopita nimelima ekari 2 na kidogo ambazo sawa na hekta moja na nilivuna tani 3 au gunia 30 za kg 100. Nilikodi shamba kwa laki moja. Vibarua wakanilimia kwa ng'ombe kwa shilingi laki moja. Gharama za mbegu, madawa ya kuuwa wadudu na kukausha nyasi pamoja na mbolea nikatumia laki tano. Kuvuna na kupukuchua pamoja na mifuko ya kuwekea mahindi nimetumia laki tatu. Jumla ya gharama nilizotumia ni milion 1. Nimeuza mahindi hayo December 2022 kwa milion 2 na nusu baada ya kuuza kwa kg Tsh. 800 hukohuko shambani. Hivyo faida ukawa ni milioni 1.5.
Sasa tukirudi kwa Bwana Bashe na wizara yake ya kilimo kwa hekta 1 au ekari 2 na kidogo bajeti yao ni kama ifutavyo:
Hapo sijajumlisha gharama za upimaji ardhi na hati miliki ambayo wameweka ni milion 2. Na hapo pia nina mashaka kama hizo ndio bei halisi za kupimia ardhi kwa hekta. Anyway tuachane na mambo ya hati miliki turudi kwenye topic yetu.
Mimi ni miongoni mwa watu ambao naunga mkono wakulima kuinuliwa hasa vijana. Mradi wa Building a Better Tomorrow au BBT lengo kuu lilikuwa ni kuinua kilimo kupitia vijana. Lakini kwa mchanganuo unaonekana ni π©ππππ πππ π©ππππ π»πππππππ - π©π©π» na kwamba mradi huu umesukwa kimkakati kuwatumia vijana kufanya ufisadi wa mabilioni. Pengine ndio maana vijana walio wengi kama sio wote waliobebwa au kupewa fursa katika mradi huo hawajui chochote kuhusu kilimo na hawajawahi kulima. Ni wakati sasa wa CAG kwenda kufanya ukaguzi katika mradi huo.
Hawa watu ambao Rais Samia aliwapa ruhusa ya kula kulingana na urefu wa kamba zao imefika mahari sasa wanataka kukata mpaka kamba ili waitafune nchi yote ibaki na mashimo. Kuna wingu zito la ufisadi kuanzia wizarani mpaka nje ya wizara ukiachilia mbali fisadi mmoja mkongwe kupewa tenda ya kusambaza mbolea katika mradi huo.
Imekuwa ngumu sana kumtenga bwana Bashe na ufisadi kwa sababu ya watu waliomlea na kumkuza katika siasa ambao kwa kiasi kikubwa wananuka ufisadi wa nchi hii. Bado nina file zake nazipitia kupata uhakika. Miongoni mwa file hizo zinahusisha baadhi ya viwanda kikiweno kiwanda cha Mbolea ya minjingu somewhere.
Kwa mazingira haya tusitegemee kama kutakuwa na uwajibikaji wowote kwa sababu wazazi wa kisiasa wa Bashe ambao wanazo kashfa nzito nchi hii wameshinda vita dhidi ya mafisadi wa Sukuma Gang ambao nao walitesa kwa miaka mitano.
Cha muhimu sasa bila kujali tofauti ya vyama vyetu na dini zetu tuungane kudai #KatibaMpya ili angarau tuokoe chenji na maliasili zilizobakia nchi hii. Tofauti na hapo tutapigwa mnada nchi hii pengine tutakosa mpaka sehemu ya kuishi.
π΄π ππ π π΅ππππππ π π ππ πΊπππ ππ π΅ππππ
Kwa mujibu wa wizara ya Kilimo chini ya waziri @HusseinBashe ni kwamba serikali inatumia milion 16.4 kufadhili shamba la hekta moja kwenye mradi wa Building a Better Tomorrow kwa kifupi BBT. Gharama hizi hazina uhalisia wowote kwa mtu anayejua kilimo au mkulima yoyote. Na kama zingekuwa na uhalisia kwamba mkulima anaweza kutumia milioni 16 kuandaa shamba la hekta moja ambayo ni sawa na ekari mbili basi nchi hii hakuna ambaye angemudu gharama hizo.
Fikiria unalima nini kwenye shamba la hekta moja ambalo maandalizi yake mpaka kupanda mbegu yanagharimu milioni 16? Unalima dhahabu kwenye hilo shamba? Au unalima almasi? Ama tanzanite? Maana haiwezekani shamba lililoandaliwa kwa milion 16 upande mahindi, Mpunga au ulezi halafu utegemee mtaji wako milioni 16 kurudi achilia mbali kupata faida.
Naomba kujitolea mfano mwenyewe maana ni mkulima. Msimu wa kilimo uliopita nimelima ekari 2 na kidogo ambazo sawa na hekta moja na nilivuna tani 3 au gunia 30 za kg 100. Nilikodi shamba kwa laki moja. Vibarua wakanilimia kwa ng'ombe kwa shilingi laki moja. Gharama za mbegu, madawa ya kuuwa wadudu na kukausha nyasi pamoja na mbolea nikatumia laki tano. Kuvuna na kupukuchua pamoja na mifuko ya kuwekea mahindi nimetumia laki tatu. Jumla ya gharama nilizotumia ni milion 1. Nimeuza mahindi hayo December 2022 kwa milion 2 na nusu baada ya kuuza kwa kg Tsh. 800 hukohuko shambani. Hivyo faida ukawa ni milioni 1.5.
Sasa tukirudi kwa Bwana Bashe na wizara yake ya kilimo kwa hekta 1 au ekari 2 na kidogo bajeti yao ni kama ifutavyo:
- Kulima shamba Tsh. 4,250,000/
- Kumwagilia Tsh. 7,500,000/
- Kupima afya ya udongo Tsh. 2,500,000/
- Mbolea Tsh. 1,750,000/
- Viuatilifu Tsh. 375,000/
- Mbegu Tsh. 112,000/-
Hapo sijajumlisha gharama za upimaji ardhi na hati miliki ambayo wameweka ni milion 2. Na hapo pia nina mashaka kama hizo ndio bei halisi za kupimia ardhi kwa hekta. Anyway tuachane na mambo ya hati miliki turudi kwenye topic yetu.
Mimi ni miongoni mwa watu ambao naunga mkono wakulima kuinuliwa hasa vijana. Mradi wa Building a Better Tomorrow au BBT lengo kuu lilikuwa ni kuinua kilimo kupitia vijana. Lakini kwa mchanganuo unaonekana ni π©ππππ πππ π©ππππ π»πππππππ - π©π©π» na kwamba mradi huu umesukwa kimkakati kuwatumia vijana kufanya ufisadi wa mabilioni. Pengine ndio maana vijana walio wengi kama sio wote waliobebwa au kupewa fursa katika mradi huo hawajui chochote kuhusu kilimo na hawajawahi kulima. Ni wakati sasa wa CAG kwenda kufanya ukaguzi katika mradi huo.
Hawa watu ambao Rais Samia aliwapa ruhusa ya kula kulingana na urefu wa kamba zao imefika mahari sasa wanataka kukata mpaka kamba ili waitafune nchi yote ibaki na mashimo. Kuna wingu zito la ufisadi kuanzia wizarani mpaka nje ya wizara ukiachilia mbali fisadi mmoja mkongwe kupewa tenda ya kusambaza mbolea katika mradi huo.
Imekuwa ngumu sana kumtenga bwana Bashe na ufisadi kwa sababu ya watu waliomlea na kumkuza katika siasa ambao kwa kiasi kikubwa wananuka ufisadi wa nchi hii. Bado nina file zake nazipitia kupata uhakika. Miongoni mwa file hizo zinahusisha baadhi ya viwanda kikiweno kiwanda cha Mbolea ya minjingu somewhere.
Kwa mazingira haya tusitegemee kama kutakuwa na uwajibikaji wowote kwa sababu wazazi wa kisiasa wa Bashe ambao wanazo kashfa nzito nchi hii wameshinda vita dhidi ya mafisadi wa Sukuma Gang ambao nao walitesa kwa miaka mitano.
Cha muhimu sasa bila kujali tofauti ya vyama vyetu na dini zetu tuungane kudai #KatibaMpya ili angarau tuokoe chenji na maliasili zilizobakia nchi hii. Tofauti na hapo tutapigwa mnada nchi hii pengine tutakosa mpaka sehemu ya kuishi.
π΄π ππ π π΅ππππππ π π ππ πΊπππ ππ π΅ππππ