Maaskofu wasusia mwaliko wa JK

Maaskofu wana lao jingine, hii issue ya impartiality haina nguvu, kwa sababu mtu unaweza kuwa impartial na ukaenda kushiriki katika vikao vya wagombea wote. Kwani watu wote wanaoenda katika mikutano ya Kikwete ni CCM ? Wote watampigia kura? Wote wanaoenda kwenye mikutano ya Slaa ni CHADEMA ? Wote watampigia kura ? Hakuna watu wanaokwenda kwenye mikutano yote ?

Swala la futari, "kufuturu" na mtu haina maana ni lazima uwe umefunga, mbona watanzania tulioishi kwa ujirani na indeed undugu na kuoleana kati ya wakristo na waislam tunaona kila siku waislam wanaalika wakristo katika futari ? Mbona tunajua kwamba ukarimu kwa waislam ni jambo la thawabu kama ulivyo kwa wakristo ?

Kwa hiyo, swala la impartiality halipo, wangempenda wangeweza kwenda na kusema wako open kwenda kwa mgombea yoyote.Kanisa halikatai mtu. Swala la kufuturu halipo, kufuturu na mtu si lazima uwe muislam, na wala si lazima hata ufunge.

Sasa baada ya kuona kwamba hayo mawili si issues, tujiulize, kwa nini maaskofu wanakataa kukutana na Kikwete ?
 
Sasa baada ya kuona kwamba hayo mawili si issues, tujiulize, kwa nini maaskofu wanakataa kukutana na Kikwete ?

Mkuu, majibu wanayo ila nao wameamua kujibu hili suala la mwaliko kisiasa maana wamegundua wanahangaika na wanasiasa. Ni kwa sisi sasa kujaribu hisia zetu kujua sababu
 
Hatuko kwenye somo la lugha hapa. Nenda TUKI au BAKITA kama unataka kiswahili fasaha

JF always tupo katika somo la lugha, ukipigwa fimbo ya kifimbocheza kubali makosa. Ukianza kukubali kuboronga lugha kidogo pole pole tutajikuta kila mtu anaongea lugha yake kama tupo katika mnara wa Babeli.
 
Labda hamuwajui hao wanaojiita Maaskofu; Mbeya inaongoza kwa kuwa na Maaskofu wengi na wengi wao ni walaji tu. Hawana ubavu wa kukataa mwaliko wa JK.

Hawa watakuwa wachache ambao wanamchukia JK au wako upande wa Dr. Slaa na wanajaribu kutumia dini kuonyesha JK hakubaliki Mbeya. Hawa ni watu wa mungu, kwanini waogope kutaja majina yao? Mwandishi hataji jina lake na hao Maaskofu wake nao hawataji majina yao. Angalau Wakatoliki bado wana miiko kwenye dini zao, lakini hizi dini zingine ambazo zimejaa Mbeya yaani ni balaa tupu.

Habari zingine zinalengo la kuwadanganya Watanzania badala ya kutoa habari. Wakati huu wa uchaguzi tutasikia mengi sana.

Hizi habari zimeandikwa na Mwananchi na hawa jamaa wana bifu na kampenia ya JK tangu wagombane kule Bukoba, nimekuwa nikifuatilia headlines zao tangu wiki iliyopita na hakuna ubishi kwamba wachagua upande wa ku-kampenia.
 
Hizi habari zimeandikwa na Mwananchi na hawa jamaa wana bifu na kampenia ya JK tangu wagombane kule Bukoba, nimekuwa nikifuatilia headlines zao tangu wiki iliyopita na hakuna ubishi kwamba wachagua upande wa ku-kampenia.

Wenzetu wa magharibi wamefikia nafasi hata magazeti yanajulikana mirengo yake. Ukisoma The New York Times unajua kabisa ni gazeti la ma liberals, Wall Street Journal ni gazeti la conservatives. Wakati wa uchaguzi magazeti yanatoa endorsement wazi wazi, lakini hili haliwafanyi wa relax katika kutafuta objectivity na halimaanishi kwamba watataka kuweka bias za kijinga katika news coverage (op-ed pieces are a whole different ballgame though)

Kwa hiyo mimi binafsi sijali sana kama gazeti lina mrengo fulani, as long as hiyo bias inajulikana (Nasoma both NYT na WSJ, OK, OK, mainly NYT, I am not a rich Jew ogling the market). Ninachojali zaidi ya hii bias / mrengo ni kwamba, je gazeti linasema kweli ?
 
Wenzetu wa magharibi wamefikia nafasi hata magazeti yanajulikana mirengo yake. Ukisoma The New York Times unajua kabisa ni gazeti la ma liberals, Wall Street Journal ni gazeti la conservatives. Wakati wa uchaguzi magazeti yanatoa endorsement wazi wazi, lakini hili haliwafanyi wa relax katika kutafuta objectivity na halimaanishi kwamba watataka kuweka bias za kijinga katika news coverage (op-ed pieces are a whole different ballgame though)

Kwa hiyo mimi binafsi sijali sana kama gazeti lina mrengo fulani, as long as hiyo bias inajulikana (Nasoma both NYT na WSJ, OK, OK, mainly NYT, I am not a rich Jew ogling the market). Ninachojali zaidi ya hii bias / mrengo ni kwamba, je gazeti linasema kweli ?
Kiranga kujua kama gazeti linasema kweli ni vizuri kutafiti ukweli wa habari hii tokea Mbeya.

Itakuwa ni kichekesho kuikataa simply kwa sababu tu imeandikwa na Mwananchi. Mwenye habari iliyo na ukweli zaidi ya huu atujuze maana wamenukuu hata watu kwa majina kuwa waliwa interview. Ubishi wa ukweli wa habari sasa hapa una sababu gani?
 
Maaskofu wasusia mwaliko wa JK

Maaskofu na wachungaji hao walimgomea Rais Kikwete Septemba Mosi, mwaka huu wakati wa ziara yake mkoani Mbeya.

Viongozi hao wa dini walisema Kikwete ni sawa na wagombea wengine wa urais wanaostahili kupatiwa haki sawa.

maaskofu na wachungaji wa dini mbalimbali takribani 40 walisema kwa nini tualikwe kwa futuru sisi ambao hatuko kwenye mfungo?

Wameugomea mwaliko huo na kuufananisha na rushwa

Askofu wa Kanisa la Pentekoste Evangelisti, Zebadia Mwanyerere Mwakatage alisema kitendo cha kualikwa na rais akiwa mgombea hakikustahili.

Mwakatage alisema Kikwete anatumia kofia yake akijua kuwa yeye ni mgombea sawa na wengine.

Hapo kwenye bluu wanasisitiza hawadanganyiki kwa rushwa ya chakula na wanasititiza Kikwete ni sawa na wagombea wengine na vivyo hasitahili kupendelewa.
 
Ni pigo kubwa kweli kweli kwa JK kutoka kwa maaskofu hawa. Ni kubwa kweli kweli. Jk afahamu kwamba mialiko ya namna hii wakati wa kampeni ni unethical, inaweza kutafsiriwa vibaya, lakini yeye huwa hajui mambo hayo. Kweli ana washauri!

Inaonekana hawandanganyiki.
 
Kila mahesabu JK anayopiga kura hazitoshi! kuchakachua itakuwa nooma! waislamu na wakristo matatani duh! sasa anataka kuomba nguvu ya makanisa? au ni nini haswa kilichomsibu private citzen to be bwana JK
2010 hatudanganyiki
 
Tatizo hapa JF wengi hamjui historia za watu na sehemu wanazoishi,kwa watu wa mkoa wa Mbeya mambo ya kijinga au kuwaburuza hawataki na huwa hawafichi mambo ,hawana unafiki wa kusema kijiko ni koleo na koleo ni kijiko,kama kijiko basi ni kijiko.Tatizo la siasa za mbeya lina mizizi miaka mingi na halijaanzia kwa Kikwete tu bali Kikwete ni kama kaongeza chumvi kwenye mboga kwa kumweka mtu kuwa mkuu wa mkoa ambaye alishindwa ubunge katika wilaya zilizopo kwenye mkoa aouongoza hii kweli ni dharau kwa wenyeji wa mkoa,pia mkuu huyo wa mkoa anachofanya ni hapo Mbeya ni kuendeleza chuki na watu wamelalamika kwa Kikwete lakini wapi,huenda sijui kama kumbukumbu zangu zimepotea sijui kama wapo basi ni wachache wakuu wa mikoa ambao toka Kikwete alipowateua kwa mara ya kwanza hawajahamishwa,kwa mkuu wa mkoa wa mbeya hajawahi hamishwa toka miaka mitano alipoteuliwa na wananchi wakilalamika zaidi ndio Kikwete anaweka pamba masikioni,sasa na wananchi nao wana njia zao za kuonyesha kupingaHONGERENI MAASKOFU WA MBEYA KWA KUGOMEA FUTARI,futari nini kwani
 
Kumbe na wewe hauelewi, huo uzi hauzungumzii ndoa ya Dr. Slaa, unazungumzia wizi wa wake za watu wa Dr. Slaa.
Mbeya ni kama Nigeria kila kona kuna kanisa.hawa wanaojiita maaskofu ni waimba kwaya.maaskofu wanajulikana vizuri.wataje majina yao tuwajue.ni kundi la Mr.Sugu Hili.
 
Maaskofu wana lao jingine, hii issue ya impartiality haina nguvu, kwa sababu mtu unaweza kuwa impartial na ukaenda kushiriki katika vikao vya wagombea wote. Kwani watu wote wanaoenda katika mikutano ya Kikwete ni CCM ? Wote watampigia kura? Wote wanaoenda kwenye mikutano ya Slaa ni CHADEMA ? Wote watampigia kura ? Hakuna watu wanaokwenda kwenye mikutano yote ?

Swala la futari, "kufuturu" na mtu haina maana ni lazima uwe umefunga, mbona watanzania tulioishi kwa ujirani na indeed undugu na kuoleana kati ya wakristo na waislam tunaona kila siku waislam wanaalika wakristo katika futari ? Mbona tunajua kwamba ukarimu kwa waislam ni jambo la thawabu kama ulivyo kwa wakristo ?

Kwa hiyo, swala la impartiality halipo, wangempenda wangeweza kwenda na kusema wako open kwenda kwa mgombea yoyote.Kanisa halikatai mtu. Swala la kufuturu halipo, kufuturu na mtu si lazima uwe muislam, na wala si lazima hata ufunge.

Sasa baada ya kuona kwamba hayo mawili si issues, tujiulize, kwa nini maaskofu wanakataa kukutana na Kikwete ?
=======

Kiranga
Tatizo si impartiality tu. Dr. Slaa akienda Mbeya akaandaa chakula cha jioni na kuwaalika wakaenda, itakuwa nongwa. Dr. akifika Mwanza airport akakuta viongozi wa dini wamejipanga kumsalimu itakuwa nongwa kwa CCM. Kiongozi mmoja amenitonya kuwa Dr. alipokuwa amelazwa Moi, alifika kumjulia hali, matokeo yake alitumiwa na waheshimiwa wanaotoka Kanisa lake jioni kuambiwa kuwa Mkulu amesikitishwa na kitendo hicho.

Kwa CCM kutumia viongozi wa dini kama Mama Rwakatare ni sawa, lakini wapinzani hawaruhisiwi!
 
wakigoma wao haina maana waumini wote hawataichagua CCM, kama ingekuwa hivo basi , ukimwi usingekuwepo, wizi na uhalifu usingekuwepo wajaribu kujitutumua TU hamna lolote!..:becky::becky:
 


Mufti Mkuu Sheikh Simba akemea wanaotaka kutumia udini na pesa (kuanzia dk 4:01 ya video clip) kupata vyeo vya kiutawala ktk kipindi hiki cha kampeni kuelekea uchaguzi Oktoba 2010.
 
Last edited by a moderator:
na commenta za wachangiaji huko kwenye gazeti ni hizi, inaonekana wakristo mwaka huu unataka kuufanya huu uchaguzi wa wakristo na waislam(ila nnaamini si wakristo wote wenye mawazo mgando kama haya)

Mtu wa Pwani, na wewe Bwana, unashindwa kutofautisha JF na hao wanaotoa maoni kwenye magazeti! Kwanza hii comment ya kwanza, kama wafahamu maaskofu wanavyojikweza, haiwezekani kabisa, askofu aandike sms! Itakuwa muujiza ninavyowafahamu, hata wachungaji na mapadri wengi wanajikuza sana.

Mimi ningekuheshimu sana ungebakia kwenye comments za JF- the Thinkers!
 
My take is at least there are few of us who can take the bull by its horn. Saying 'no' to a President isn't that easy. I am glad at least for the reasons expressed. Sio tu unaitiwa chakula unakimbilia bila kujua kwa nini! Au unaitwa njoo ukagawiwe fulana au vyandalua usijiulize mbona leo! Nawapa pongezi hawa, walau wametufundisha kufikiria kabla ya kutenda! Kama wamefanya hivyo kiunafiki basi naye Mungu atawaadhibu, Mungu hadanganyiki!
 
wakigoma wao haina maana waumini wote hawataichagua CCM, kama ingekuwa hivo basi , ukimwi usingekuwepo, wizi na uhalifu usingekuwepo wajaribu kujitutumua TU hamna lolote!..:becky::becky:

Mawazo haya hapo juu yanaendelea kuthibitisha maoni ya maaskofu kuwa chakula cha Kikwete kiliandaliwa kama rushwa kwa ajili ya kupatiwa kura.
 
Maaskofu hatuzitaki KURA ZENU!!! Na bado ushindi utakuwa kishindo mwaka huu...:becky::becky:!

Za maaskofu hamzitaki, za waumini hamzitaki za wafanyakazi hamzitaki, za ....hamzitaki sasa kura za CCM zitatoka sayari ya Masi?
 
Back
Top Bottom