Madabwada
JF-Expert Member
- May 8, 2009
- 541
- 314
Na Joseph Sabinus
Tanzania Daima
KANISA Katoliki nchini limeibuka tena na kutoa waraka kwa waamini wake kuhusu namna bora ya kushiriki uchaguzi mkuu ujao na safari hii likitoa maswali mazito kwa wagombea ambayo waumini wao wanapaswa kuyazingatia.
Waraka huo umo kwenye ujumbe wa Kwaresima wa mwaka huu, walioutoa hivi karibuni na kusainiwa na maaskofu wa majimbo yote 31 nchini, wakiongozwa na dhamira kuu isemayo Ninyi ni Chumvi ya Dunia (Mt 5:13).
Kama tunavyofahamu, nchi yetu iko katika mchakato wa uchaguzi mkuu, utakaofanyika Oktoba 2010. Uchaguzi huo utatupatia viongozi wapya: madiwani, wabunge na rais wa nchi yetu.
Uchaguzi huo ni tukio la kijamii na vile vile ni tukio la kisiasa. Ni tukio ambalo Wakristo wote wanapaswa kushiriki kama wajibu wao. Historia yatwambia kwamba, ushiriki wa Wakristo katika mambo ya ulimwengu umekuwa wa namna tofauti katika kipindi cha zaidi ya miaka 2000, ilisomeka sehemu ya waraka huo.
Kwa mujibu wa waraka huo wenye kurasa 30, namna moja ya Wakristo kushiriki katika masuala ya kiulimwengu ni kwa njia ya kushiriki katika masuala ya kisiasa kwa kuwa wanaposhiriki katika masuala ya kisiasa wanatimiza wajibu wa kiraia.
Katika ujumbe huo wa Kwaresma mwaka huu, maaskofu hao wanasema uchaguzi huo ni tukio la kijamii na la kisiasa, hivyo Wakristo wote hawana budi kushiriki kikamilifu ili kutimiza wajibu wao.
Kwa upande wa wagombea watakaojitokeza kuwania nafasi mbalimbali za uongozi, waraka huo umewataka kujiuliza wanataka kuwafanyia nini Watanzania ili wawe na maisha bora yanayompendeza Mwenyezi Mungu.
Tunaomba sana na kuwasihi wale wote wanaogombea katika nafasi hizo za uongozi wafikiri na kutafakari kwa makini ni kitu gani kimewasukuma ili kuchukua hatua hiyo? Wanataka kwa moyo wao wote kuwatumikia Watanzania ili kila mtu katika jamii yetu apate hadhi yake ya kiutu ambayo ni stahili yake? ulihoji waraka huo.
Aidha, maaskofu hao wamewataka wagombea wote kujiuliza kama kweli wana nia ya dhati ya kuwasaidia Watanzania ili kila mtu apatiwe mahitaji msingi ya kumwezesha kuishi maisha yanayomstahili mwanadamu, pamoja na kuwa tayari kuzifanya rasilimali za nchi yetu kuwa kwa ajili ya manufaa ya wote.
Wakati tunawahimiza waamini wote kushiriki katika zoezi zima la uchaguzi, tunaomba vile vile wale watakaoshiriki katika kuchagua, wawahoji na wapime udhati wa nia ya wagombea kwa kufuata vigezo vya hadhi ya utu wa mwanadamu na tunu za kimaadili.
Kamwe msichague mtu kwa sababu ya shinikizo, wala kwa sababu ya rushwa, au ubaguzi wowote ule kwani kwa kufanya hivyo mtakuwa mnakosea mbele ya Mungu. Muwachague viongozi mkiwa mmeongozwa na dhamiri safi mbele ya Mungu na hivyo muwachague viongozi ambao wataliongoza taifa hili kwa kujali maslahi ya wote na ambao watatusaidia kujenga jamii yenye upendo, umoja, haki na amani, inasomeka sehemu ya waraka huo.
Maaskofu hao wamesisitiza kuwa, kamwe binadamu hawezi kutenganishwa na Mungu na wala siasa haiwezi kutenganishwa na maadili.
Hili ndilo jambo ambalo Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ambaye mchakato wa kumtangaza Mwenyeheri unaendelea, alitufundisha kwamba siasa lazima ijengwe katika misingi imara ya kanuni thabiti za kimaadili zinazopaswa kuwa ndiyo mhimili wa maisha katika jamii, walisema maaskofu hao.
Walisisitiza kuwa katika kipindi hiki ambacho nchi ipo katika mfumo wa vyama vingi vya siasa, waumini wana haki ya kujiunga na kushiriki katika kuchagua ama kuchaguliwa ili kutimiza wajibu wao.
Walisisitiza kuwa hali hii ya kuwapa uwezo na haki ya kushiriki uchaguzi kupitia vyama mbalimbali vya siasa, haiwezi kuchanganywa na hali ya kushindwa kutambua na kuchagua kanuni za kimaadili na tunu za msingi zinazojali hadhi ya utu wa binadamu.
Wamekwenda mbali na kusema kuwa, demokrasia ya kweli ambayo uchaguzi ni sehemu tu ya kielelezo chake, itafaulu endapo tu itajengwa juu ya uelewa sahihi wa nafsi ya binadamu.
Walitahadharisha kuwa ushiriki wa Wakristo katika siasa na hasa katika uchaguzi ujao, haupaswi kuipuuzia kanuni hii vinginevyo ushuhuda wa imani ya Kikristo ulimwenguni na muungano unaopaswa kuwepo kati ya yale ambayo Wakristo wanayaamini na maisha yao ya kawaida hautakuwepo.
Huenda badala ya kuwa chumvi inayokoleza katika jamii, mara nyingine mmekuwa kama chumvi isiyo na ladha kwa kuwa chanzo cha uozo katika jamii. Au wakati fulani na katika mazingira fulani mmekuwa ndiyo chanzo cha kueneza ubinafsi, uchu wa madaraka na hata wa mali? walisema maaskofu hao katika waraka huo.
Miezi kadhaa iliyopita, maaskofu Wakatoliki hao walitoa waraka wa kichungaji uliovuta hisia za wengi ukiwa unatoa elimu kwa waamini wake juu ya namna ya kushiriki katika uchaguzi mkuu ujao na kuwapata viongozi bora kwa njia sahihi.
nb: wanajamvi .... aliyenao aturushie jamvini pls ...
Tanzania Daima
KANISA Katoliki nchini limeibuka tena na kutoa waraka kwa waamini wake kuhusu namna bora ya kushiriki uchaguzi mkuu ujao na safari hii likitoa maswali mazito kwa wagombea ambayo waumini wao wanapaswa kuyazingatia.
Waraka huo umo kwenye ujumbe wa Kwaresima wa mwaka huu, walioutoa hivi karibuni na kusainiwa na maaskofu wa majimbo yote 31 nchini, wakiongozwa na dhamira kuu isemayo Ninyi ni Chumvi ya Dunia (Mt 5:13).
Kama tunavyofahamu, nchi yetu iko katika mchakato wa uchaguzi mkuu, utakaofanyika Oktoba 2010. Uchaguzi huo utatupatia viongozi wapya: madiwani, wabunge na rais wa nchi yetu.
Uchaguzi huo ni tukio la kijamii na vile vile ni tukio la kisiasa. Ni tukio ambalo Wakristo wote wanapaswa kushiriki kama wajibu wao. Historia yatwambia kwamba, ushiriki wa Wakristo katika mambo ya ulimwengu umekuwa wa namna tofauti katika kipindi cha zaidi ya miaka 2000, ilisomeka sehemu ya waraka huo.
Kwa mujibu wa waraka huo wenye kurasa 30, namna moja ya Wakristo kushiriki katika masuala ya kiulimwengu ni kwa njia ya kushiriki katika masuala ya kisiasa kwa kuwa wanaposhiriki katika masuala ya kisiasa wanatimiza wajibu wa kiraia.
Katika ujumbe huo wa Kwaresma mwaka huu, maaskofu hao wanasema uchaguzi huo ni tukio la kijamii na la kisiasa, hivyo Wakristo wote hawana budi kushiriki kikamilifu ili kutimiza wajibu wao.
Kwa upande wa wagombea watakaojitokeza kuwania nafasi mbalimbali za uongozi, waraka huo umewataka kujiuliza wanataka kuwafanyia nini Watanzania ili wawe na maisha bora yanayompendeza Mwenyezi Mungu.
Tunaomba sana na kuwasihi wale wote wanaogombea katika nafasi hizo za uongozi wafikiri na kutafakari kwa makini ni kitu gani kimewasukuma ili kuchukua hatua hiyo? Wanataka kwa moyo wao wote kuwatumikia Watanzania ili kila mtu katika jamii yetu apate hadhi yake ya kiutu ambayo ni stahili yake? ulihoji waraka huo.
Aidha, maaskofu hao wamewataka wagombea wote kujiuliza kama kweli wana nia ya dhati ya kuwasaidia Watanzania ili kila mtu apatiwe mahitaji msingi ya kumwezesha kuishi maisha yanayomstahili mwanadamu, pamoja na kuwa tayari kuzifanya rasilimali za nchi yetu kuwa kwa ajili ya manufaa ya wote.
Wakati tunawahimiza waamini wote kushiriki katika zoezi zima la uchaguzi, tunaomba vile vile wale watakaoshiriki katika kuchagua, wawahoji na wapime udhati wa nia ya wagombea kwa kufuata vigezo vya hadhi ya utu wa mwanadamu na tunu za kimaadili.
Kamwe msichague mtu kwa sababu ya shinikizo, wala kwa sababu ya rushwa, au ubaguzi wowote ule kwani kwa kufanya hivyo mtakuwa mnakosea mbele ya Mungu. Muwachague viongozi mkiwa mmeongozwa na dhamiri safi mbele ya Mungu na hivyo muwachague viongozi ambao wataliongoza taifa hili kwa kujali maslahi ya wote na ambao watatusaidia kujenga jamii yenye upendo, umoja, haki na amani, inasomeka sehemu ya waraka huo.
Maaskofu hao wamesisitiza kuwa, kamwe binadamu hawezi kutenganishwa na Mungu na wala siasa haiwezi kutenganishwa na maadili.
Hili ndilo jambo ambalo Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ambaye mchakato wa kumtangaza Mwenyeheri unaendelea, alitufundisha kwamba siasa lazima ijengwe katika misingi imara ya kanuni thabiti za kimaadili zinazopaswa kuwa ndiyo mhimili wa maisha katika jamii, walisema maaskofu hao.
Walisisitiza kuwa katika kipindi hiki ambacho nchi ipo katika mfumo wa vyama vingi vya siasa, waumini wana haki ya kujiunga na kushiriki katika kuchagua ama kuchaguliwa ili kutimiza wajibu wao.
Walisisitiza kuwa hali hii ya kuwapa uwezo na haki ya kushiriki uchaguzi kupitia vyama mbalimbali vya siasa, haiwezi kuchanganywa na hali ya kushindwa kutambua na kuchagua kanuni za kimaadili na tunu za msingi zinazojali hadhi ya utu wa binadamu.
Wamekwenda mbali na kusema kuwa, demokrasia ya kweli ambayo uchaguzi ni sehemu tu ya kielelezo chake, itafaulu endapo tu itajengwa juu ya uelewa sahihi wa nafsi ya binadamu.
Walitahadharisha kuwa ushiriki wa Wakristo katika siasa na hasa katika uchaguzi ujao, haupaswi kuipuuzia kanuni hii vinginevyo ushuhuda wa imani ya Kikristo ulimwenguni na muungano unaopaswa kuwepo kati ya yale ambayo Wakristo wanayaamini na maisha yao ya kawaida hautakuwepo.
Huenda badala ya kuwa chumvi inayokoleza katika jamii, mara nyingine mmekuwa kama chumvi isiyo na ladha kwa kuwa chanzo cha uozo katika jamii. Au wakati fulani na katika mazingira fulani mmekuwa ndiyo chanzo cha kueneza ubinafsi, uchu wa madaraka na hata wa mali? walisema maaskofu hao katika waraka huo.
Miezi kadhaa iliyopita, maaskofu Wakatoliki hao walitoa waraka wa kichungaji uliovuta hisia za wengi ukiwa unatoa elimu kwa waamini wake juu ya namna ya kushiriki katika uchaguzi mkuu ujao na kuwapata viongozi bora kwa njia sahihi.
nb: wanajamvi .... aliyenao aturushie jamvini pls ...