Maandamano ya wananchi kumuunga mkono Spika Ndugai

Maandamano ya wananchi kumuunga mkono Spika Ndugai

Kipindi wapinzani wanaambiwa wakiandamana watapigwa mpaka wachakae mlikua mnachekelea.

Sasa ni zamu yenu kupigwa mpaka mchakae.

Andamaneni mkione cha moto [emoji2]

Mungu wetu ni mwaminifu sana, hujibu kila jambo kwa wakati wake [emoji120]
Sisi sio wapinzani au chama cha siasa, kuhusu kupigwa tulishajiaandaa na hiyo hali endapo ikitokea Ila haya ni maandamano ya amani, hivyo tunahitaji amani kwenye maandamano yetu
 
Wananchi wapi mkuu? [emoji23][emoji23][emoji23]

Sikia, kuna mambo mengi sana yakuwapeleka watz barabarani tena yanayogusa maisha yao moja kwa moja hilo la Ndugai ni cha mtoto! Lakini watu wako kimya wamelizika tu, sembuse hilo la Ndugai?

Acha watz waitwe watz
 
Maandamano yapo kikatiba, hivyo ni vyema maandamano yaandaliwe kwa kufuata kanuni na taratibu zilizopo. Naunga mkono 100% maandamano hayo
 
Hivi alishindwa nini kujiuzulu bila kuomba msamaha?
Alitakiwa kuonyesha msimamo kwa alichokiongea bila kuomba msamaha. Kuomba msamaha ndiyo kosa kubwa zaidi maana inaonyesha alichoongea akina ukweli. Alafu mbaya zaidi unamwomba msamaha mtu asiyejua maana ya msamaha Wala kusamehe. Na asiyesamehe.
 
Tanzania hii nani atapoteza muda kuandamana, mtu aache kuitafutia familia yake chakula mezani aende kuandamana na kupigwa virungu
Mkuu utajikuta mwenyewe huko jangwani na pale pana mafuriko mvua ikija utasombwa na maji utajikuta uko mto wami huko ,kisa nini, ndugai?!
Watanzania wameshachoshwa na hizi sarakasi za serikali sasa, Kwa taarifa yako hii taarifa imeshasambaa Kwa machinga wote, bodaboda, na wananchi wengi wa kawaida.
Ninyi wanufaika wa mifumo ya kinyonyaji ya serikali hii hatuwahitaji.
 
Shujaa gani anakana alichosema. Tena unalia nimekosa Sana Mimi mnisamehe. Shujaa anapambana mpaka mwisho. Ajifunze kwa kina mbowe ambao wako tayari kufia jela bila kuomba msamaha.
Hoja sio Ndugai, hoja ni kwamba kushikilia msimamo wa kuondoa huo mseto wa hayo matozo, umeme, mikopo n.k
 
Ndugai ameshatuwakilisha wananchi, ni mda wetu wananchi kuandamana Kwa kumuunga mkono.
Ndugai ni shujaa
Niandamane kwa ajili ya Ndugai mangapi kayapitisha? baada ya kuona awamu hii imempa kisogo anataka tumuone wa maana upande wangu hapana kaita wangapi wakajiekeza kwenye kamati ya maadili ya bunge kwa kusema ukweli? Mliowakilishwa andamaneni mkifika maeneo yangu nitawapeni maji ya kunywa muendelee na safari
 
Niseme Kwa kifupi kwamba, Ndugai alitoa mawazo kuhusu mikopo ya nchi na tozo kuwakilisha kilio cha wananchi wengi, ila nasikitika kwamba ccm wameshinikiza ajiuzuru Kwa maslahi ya chama Chao.

Jambo kama hilo ni hatari Kwa watu wengine wenye mawazo mbadala katika kusemea matatizo ya wananchi wa hali ya chini.

Hivyo watanzania ni vyema tukaandamana kumuunga mkono Mh Ndugai Kwa uthubutu ule wa kuweza kuzungumzia matatizo ya wananchi wa hali ya chini, Pia kuwapa moyo watu wengine wenye mawazo mbadala kuzungumzia matatizo ya wananchi wa hali ya chini
Mawazo ya wananchi yalizungumziwa barabarani wakati mjengo upo,
Tuandamane kama sehemu ya shukrani kutoka huyu mgonjwa aliyepitisha sheria kandamizi
 
Back
Top Bottom