babu na mjukuu
JF-Expert Member
- Jun 23, 2016
- 3,949
- 6,752
Acha dharau kwa watu wa Mbeya. Ina maana wana dhiki sana hadi wapoteze muda wao kwa elfu 3!?View attachment 1052612
Wengi wamekuwa wakijiuliza inakuwaje wananchi wa Mbeya , mkoa ambao Tangu Rais achaguliwe hajawahi kukanyaga , Mkoa unaoongoza kwa ajali za kutisha za magari kutokana na uduni wa barabara baada ya wenye mamlaka kujiapiza kutoziboresha ili kuwakomesha wananchi walioikataa ccm kidemokrasia eti wananchi waandamane kuunga mkono juhudi ?
Ukweli ni huu hapa , maandamano yale yaliwezeshwa kwa watu kupewa fedha taslimu , watu wamelipwa kuanzia elfu 3 , 5 , hadi elfu 10 kulingana na hadhi ya muhusika , malipo yalisimamiwa na watendaji wa vijiji na wajumbe wa nyumba 10 , bado haijafahamika kilikotoka kitita hicho ( tunaendelea kufukunyua ) , sare nyingi mpya za ccm ziligawiwa , angalieni vizuri mavazi ya waandamanaji , pamoja na wafanyakazi kutishwa wasipoandamana lakini pia walilipwa posho kwa viwango tofauti kulingana na hadhi .
Watu wanajiuliza kuna kipi kilichofanyika hadi watu wa Mbeya waandamane , mbona Chato hakujawahi kufanyika maandamano kama hayo pamoja na neema ya uwanja wa ndege waliojengewa ? Ama hakika propaganda za ccm ni rahisi mno kuzing'amua.
SIRI IMEFICHUKA
Hizi dharau zenu ndio sababu ya hilo lichama lenu linakufu
Sent using Jamii Forums mobile app