Maandamano ya CHADEMA Arusha: Mabomu yarindima, raia wauawa na viongozi wakamatwa

yani hawa watu ni tigo haswa!wametuibia kura tumenyamaza then wanataka waendelee kututia vidole machoni!nina hasira nao plse moshi kesho tuingie barabarani kama noma na iwe noma!
 
Mungu yuko nawe dr. salaaa na CDM. Watanzania tunawaombea na hata siku moja majambazi hawatashinda nguvu ya umma
 
Chadema haitafuti haki, haki ipi mnayoitafuta na mlionyimwa? mmedai katiba, hewala. Mnauza vibinti chini ya umri pale Bili, hewala. Mnapora wake za watu, hewala.

Sasa, mnaiba na kuharibu mali za raia na kuhatarisha maisha ya wananchi na wageni hapo Arusha, halafu mnasema historia ya kutaka haki? Hivi mnajuwa mnachokifanya? Hakuna mTanzania mwenye akili timamu atae-waunga mkono kwa hili.

Nyie mnafikiri mkikaliwa kimya na Serikali ni kuwa inawaogopa? Sasa mtakiona.

Hovyoooooooooooooooooooooooooooooooooooooo
 
They shall kill our bodies... but never our spirits!!!!! AMANDLAH!!!!!!!!![/SIZE]
 
Labda kama umeanza kufuatilia siasa 2006, hii hali sio mpya na haijavunja bado record ya matukio makubwa zaidi yaliyopata kutokea, na Chadema wanawajibika pia kwa upotevu wa mali za raia wema na usumbufu usio wa lazima uliotokea leo.

We vipi? nani kwa kwambia nia ni kuvunja record? Mali za raia wema zishachukuliwa na mafisadi long back na bado wanajichukulia tu kwa kuwa wewe ni kilaza huwezi jua...
 
Ipo siku tu, yatakwisha kwa kupata katiba mpya ambayo itatuwezesha kuunda serikali inayoheshimu HAKI ZA BINADAMU
 
The end of CCM is coming soon. Let us fight for our rights.
This is unreasonable excessive use of force against the innocents. Shida kubwa ya polisi wetu hawana elimu, ni mambumbu tu, hata sheria za nchi hawazijui, waliowengi wanapata kazi za upolisi kifisadi.
Petendekazo: Polisi wetu wawe na elimu ya kutosha juu ya sheria za nchi wanazozisimamia.Kwa matukio haya ya kipumbavu inaonekana polisi wetu wapo kwaajili ya kujipendekeza kwa bosi wao KIWETE J, ambaye yupo madarakani kwa nguvu za dola na ufisadi. Hii ni aibu kubwa sana kwa nchi. Ni ukiukwaji mkubwa wa Demokrasia nchini. Hakuna utawala wa sheria katika nchii hii. Bali ni utawara wa shari na ufisadi.
 
huo ni mwanzo wa safari wandugu... ukishakuwa mpinzani basi hicho ni kitu cha kawaida. Kuna watu wameshauawa nchi hii na kutiwa kizuizini kwa muda mrefu sababu ya siasa, kuna watu wamelemaa na wengine walivunjwa mikono, sababu ni wapinzani.

Leo hii watu wamesahau yote hayo.... Hii ni kwa sababu ya ukosefu wa kumbukumbu tulionao tunalichukulia kwamba ni suala kubwa sana.. je mwadhani ni halali kukiuka amri ya serikali hata kama ni ovu na hatua isichukuliwe? lazima tukubali kuheshimu utawala na watawala wake huku tukitumia busara za ziada kutatua matatizo tuliyonayo. napenda kuwakumbusha tena Serikali yoyote ile iwayo HAITISHWI bali HUTISHA. Je ikiwa hivyo ndivyo ni wangapi wanabaki nyuma ya Laptop zao kuwahamasisha wapumbavu wachache wafanye ujinga? Na mwisho wa siku wanaumia waliomo na wasiokuwamo.

Kesho mtu aende hospitali ya Mawezi na atajionea majeruhi wangapi watakuwa na pingu! (hali yenyewe ndio hii, kisha mtiwe vilema na hali wenye akili zao wanatanua na kusalimiana na hao mnaowaona kuwa ni adui zao!) Siasa za nchi hii.....:embarrassed:

Hapo umeongea kama umepata utapiamlo wa kisiasa, matatizo ya siasa yanayojitokeza sasa hivi hayatokani na Chadema wala Dr. Slaa, tatizo kubwa ni CCM na utendaji mbovu wa serikali, umasikini unaathiri mamilioni ya watanzania, lishe duni, huduma za afya hakuna, kazi hawana, hivi sasa familia nyingi zinashindwa kumudu hata mlo mmoja kwa siku kutokana na kupanda bei za vyakula, kila kukicha serikali inakumbwa na kashfa za ubadhirifu wa mali za umma, watu wanaonufaika na serikali hii ni wachache sana, jeshi la masikini ni kubwa kumbuka vifaru na AK-47 hazikuwasaidia madikteta kama vile Bokasa, Marcias Nguema, Ferdinad Marcos kubaki madarakani, wananchi wanachotaka ni usawa na haki.
 
Zitto

Wenzio wote wamekamatwa umebaki wewe! sasa niwakati wako wa kusimamia chama .........Tafadhali toa tamko haraka sana
 
Wameshindwa kukamata fikra sahihi, wanakamata watu! Maandiko yanatuambia tusimuogope yule anayeua mwili, bali tumuogope yule anayeweza kuua roho! Je hawa ndata wanaweza kufifisha fikra pevu za viongozi wa cdm? :redfaces:
 
Viongozi wa CCM wanaochochea uvurugaji wa amani wakumbuke kuna mahakama ya kimataifa inawasubiri! Hakika mtajibu mashtaka mbele za haki!
 
Back
Top Bottom