Maandamano makubwa Songea!

Maandamano makubwa Songea!

polisi wa kibongo ushuzi mtupu..kila wakiona maandamano wao wanayahusisha na siasa,.wanadhani ccm inataka kuondolewa madarakani..stupid low salaried guns bearers..
 
Labda polisi wanatest nchi ikoje baada ya mavituz ya Arusha Mwanza na Mbeya. Wanajaribu kuona maeneo mengine ya nchi yakoje. Ila wasije wakajaribu Dar es salaam kwa sababu hiyo ndo itakua Benguz ya Tanzania.
 
Kwa wale ambao walikuwa hawafuatilii yaliyokuwa yanatokwa Songea ni kwamba mji wa Songea na viunga kwasasa umegubikwa na mauaji ya kutisha sana, kitu ambacho kimekuwa kero kwa wakazi wa mji huu. Tatizo jingine ambalo ni kilio cha muda mrefu ni kukosekana kwa umeme. Ni kitu cha kawaida wakazi wa mji huu kukosa umeme kwa masaa zaidi ya 12. Waweza soma malalamiko zaidi ya wananchi wa songea hapa Facebook Songea Group: Log In | Facebook

Pia habari hizi za mauaji zimeripotiwa na vyombo mbalimbali. Kwa kusoma habari na kuangalia picha za watuhumiwa wa mauaji mjini Songea hapa: JIACHIE
 
Ndugu kwa hiyo

(a) kuchoma kituo cha police si ujanja = Lakini kuua Raia wasio na hatia ni Ujanja.

(b) maana hasara na kwetu sis walipa kodi = lakini kuua Raia wasio na hatia ni FAIDA KWETU WALIPA KODI

(C) Nasisitiza maandamano si kufanya uhalifu otherwise hayatakuwa na credibility = Kuua Raia wasio na hatia kuna Credibility hapo.


Yaani ndugu yangu sipati 😛hoto:😛hoto:😛hoto: hii.

Sijui na wewe ni mmoja wa hao FFU hapo Songea. Kama ndivyo waambie wenzio wanachofanya si jambo zuri. Elewa kuwa unaowaumiza pia wapo ndugu zako. Utajisikiaje ukirudi nyumbani jioni ukaambiwa baba / kaka/ / dada yako amekufa au kajeruhiwa katika fujo hizo?

TAFAKARIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIII


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!

you totally missed my point!
what I meant is, Ubaya haulipwi kwa ubaya, I do not support any killings whatsoever.
 
Tulianzisheni kama senegal

yaani wewe umejifungia ndani tena nyuma ya computer unasema tulianzisheni kama senegal, hebu kuwa wa kwanza wewe toka nje na upaze sauti, hapo hauta ona post yoyote humu, jf tutakawa barabarani wote, HEBU TUACHE UNAFK NA USHABIK. RIP wapambanaji wa kweli songea, ushindi unakuja.
 
MAJAMBAZI++WAUAWA.jpg


Pichani ni miili ya watu wawili wanaodaiwa kuwa majambazi ambao walipigwa na kuchomwa moto hadi kifo katika eneo la Ruhuwiko manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.

Baadhi ya wakazi wa eneo la Ruhuwiko ambao hawakutaka kutaja majina yao walidai kuwa kabla ya tukio hilo watu hao hawakuweza kufahamika majina yao waliwasili eneo hilo majira ya saa tatu asubuhi wakiwa na lengo la kuuwa na kuondoa viungo vya uzazi vya binadamu ambavyo inadaiwa vinauzwa kwa fedha nyingi.


Wananchi hao walidai kuwa watu hao walifika kwa mama mmoja ambao walidai wanamtafuta hatimaye wakiwa wanakunywa katika klabu moja ya pombe za kienyeji inadaiwa wakazi wa eneo hilo waliwatilia mashaka watu hao na kuaanza kuwahoji ambapo inadaiwa baada ya kupata kipigo na kuanza kuchomwa walieleza kwamba wao ni wauaji na walipewa fedha kwa ajili ya kuuwa na kwamba tayari wamekuwa wamefanya matukio kadhaa ya mauaji .

Chanzo cha habari kimebainisha kuwa wauaji hao walidai kuwa wapo 50 na wanatakiwa kuuwa watu zaidi ya 100 wakiwemo wanaume 60 na wanawake 40 kwa kuwaondoa sehemu zao za siri ambazo inadaiwa ni biashara ambayo inawapatia fedha nyingi .

Baada ya wauaji hao ambao walikutwa na shilingi 500,000 kukiri kuwa kazi yao ni kuuwa ndipo wananchi wengi wenye hasira waliamua kuanza kuwapa kipigo kizito kisha kununua petroli na kuanza kuwachoma wakiwa hai .Hadi polisi wanafika katika eneo hilo miili ya watu hao ilikuwa inaendelea kuungua kwa moto.

Uchunguzi umebaini kuwa wakazi wa Ruhuwiko waliamua kuchukua sheria mkononi baada ya matukio ya uharifu na mauaji kujitokeza katika eneo hilo na kwamba hii ni mara ya pili kwa wakazi wa Ruhuwiko kufanya mauaji ya kutisha ambapo miaka 25 iliyopita watu wengine wawili waliodaiwa kuwa ni majambazi sugu waliuwa na kisha miili yao kuchomwa moto.


"Mimi binfasi nimefurahia sana kitendo hiki labda sasa majambazi yataogopa kuendelea kufanya uharifu katika eneo hili,hivi sasa hatuna amani kabisa wizi imekuwa ni jambo la karibu kila siku ,mauaji nayo yanazidi kuendelea ,waharifu wengine wanakamatwa na kuachiwa acha wananchi wajichukulie sheria mkononi'',alisema mama mmoja ambaye hakutaka jina lake kuandikwa.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na polisi bado wanaendelea na uchunguzi.

Chanzo:
http://mtangazaji.blogspot.com/2012/02/sheria-mkononi-wawili-wachomwa-hadi.html
 
Vipi Chadema wapo huko? Hawakawii kusingiziwa!

Songea ni CCM tu, Mbunge wamempitisha wa CCM. Wakati wa kampeni John Komba aliwaimbia ndugu zangu Wangoni ule wimbo wao waliokuwa wanaupenda kwenye kampeni,

"WATU WOTE TIENI, TIENI, TIENI, TIENI KWA MOYO MMOJA, NAMBARI WANI EEE, NAMBARI WANI NI CCM"

Nao wakafanya kweli walifikiri masihala.


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
ebwana tujuzeni mlio jirani ya tukio hapo songea.

wananchi wamechoma matairi mengi barabara zote zinazoingia,wananchi wamechachamaa hawaogopi polisi wala f.f.u na mabomu yao,ofisi ya ccm imebomolewa na baada ya polisi kuuwa raia ndo vurugu zimezidi watu wanatoka majumbani kwenda kuungana na wenzao,shule zimefungwa watoto wamerudishwa nyumbani,polisi pamoja na f.f.u wamezidiwa wanaomba usaidizi wa jeshi,mimi mwanangu hajaonekana naendelea kumtafuta,huo ndo utawala wa ccm,TANZANIA NI NCHI YA AMANI NA UTULIVU.huo ndo utulivu wanaousema?
 
you totally missed my point!
what I meant is, Ubaya haulipwi kwa ubaya, I do not support any killings whatsoever.


Mkuu nimekupata. Kumbe tupo pamoja.

Asante.


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Uletaji wa taarifa wa namna hii na unataka watu wajadili sidhani kama unakubalika kwenye jukwaa makini kama hili.Wewe ndio mleta taarifa sasa unataka nani mwingine atoe taarifa? Sisi hatujui wewe ndio unajua sana unauliza kwetu ili iweje?

Huwezi kuwa na taarifa muhimi kama hii ukakaa kimya na eti kisa huna habari kamili na pia eti jukwaa makini.. kwnai hii habari si makini?????? tuwe wakweli sasa
 
Uletaji wa taarifa wa namna hii na unataka watu wajadili sidhani kama unakubalika kwenye jukwaa makini kama hili.Wewe ndio mleta taarifa sasa unataka nani mwingine atoe taarifa? Sisi hatujui wewe ndio unajua sana unauliza kwetu ili iweje?

Sikutegemea wewe uwe shallow kiasi hiki. Nini mbaya kwa muanzisha mada? JF sio Idara ya Habari (Maelezo) kiasi kila anayeleta habari awajibike kwayo. Huyu ndugu ametengeneza Platform ili kila mwenye habari zaidi aweke na sisi tulio mbali tujue.

Mimi binafsi sioni mbaya
 
yaani wewe umejifungia ndani tena nyuma ya computer unasema tulianzisheni kama senegal, hebu kuwa wa kwanza wewe toka nje na upaze sauti, hapo hauta ona post yoyote humu, jf tutakawa barabarani wote, HEBU TUACHE UNAFK NA USHABIK. RIP wapambanaji wa kweli songea, ushindi unakuja.


sijui uoga huu utatupeleka wapi
 
Polisi wa Mwema haya ndio waliyojifunza ccp moshi......
Wananchi wa songea asubuhi ya leo walikuwa wanaandamana kushinikiza jeshi la polisi lichukue hatua kudhibiti mauaji yanayotokea kila siku mjini hapa. Katika maandamano hayo polisi walianza kuwashambulia wananchi kwa risasi za moto na mabomu ya machozi. mwandishi wa habari hizi amenusurika kupigwa risasi ambayo imempata mtu aliyekuwa jirani yake, ambaye amepoteza maisha hapo hapo. katika mashambulizi hayo mwandishi ameshuhudi watu wawili wamepigwa risasi na kufa hapo hapo. Mpaka na kwenda mtimboni bado risasi za moto zinarindima.


Mwandishi wa TBC akiwa anajihami na risasi za polisi


Mmoja kati ya waliouawa na polisi




Polisi wakifyatua risasi kwa raia


Dimbwi la damu



 
kwa sasa waandamanaji wanaelekea kwenye kituo cha redio cha jogoo fm, kwani kimetumiwa kupotosha taarifa, kaazi kwelikweli.
 
wananchi wamechoma matairi mengi barabara zote zinazoingia,wananchi wamechachamaa hawaogopi polisi wala f.f.u na mabomu yao,ofisi ya ccm imebomolewa na baada ya polisi kuuwa raia ndo vurugu zimezidi watu wanatoka majumbani kwenda kuungana na wenzao,shule zimefungwa watoto wamerudishwa nyumbani,polisi pamoja na f.f.u wamezidiwa wanaomba usaidizi wa jeshi,mimi mwanangu hajaonekana naendelea kumtafuta,huo ndo utawala wa ccm,TANZANIA NI NCHI YA AMANI NA UTULIVU.huo ndo utulivu wanaousema?
nchi yetu hii...halafu utakuta kwenye tv zetu wanaonyesha taarabu na tamthiliya sasa hivi.
 
Back
Top Bottom