Ahsante kwa taarifa, kwakweli ni masikitiko makubwa kwa wananchi pamoja na hao askari waliopoteza maisha yao.
Hili suala la polisi kutumia mabavu kila mara kwa raia wasiokuwa hata na jiwe ni upumbavu mkubwa sana, na sijui kama haya ndiyo mafundisho wanayokwenda kupata chuoni CCP kwa muda wote wa mwaka mmoja.
Kama wananchi wameandamana hadi kwa mkuu wa mkoa na wanachotaka ni mkuu wa mkoa atoke kuwasikiliza, tatizo lilikuwa wapi hadi FFU wanaamua kupiga risasi za moto hadi kuua raia? kama wameshindwa kuwalinda raia hadi wanauawa kila siku bila msaada wao, huo ubabe wa kuwaua raia wema unatoka wapi? mbona wameshindwa kupambana na hao wauaji?
Kumbe Dr. Mwakyembe hakukosea kwamba jeshi la polisi la Tanzania, ndilo jeshi la polisi pekee duniani linalosubiri kuletewa ushahidi mezani kama vile mahakama zinavyosubiri kuletewa ushahidi ili zifanye kazi. Na hii tabia ya polisi kuwaonea wananchi ipo siku watachoka na wataamua kukabiliana nao bila kujali risasi za moto ama mabomu, ikizuka majimaji ya pili huko wasije kuwalaumu wananchi.