Maandamano kupinga posho za Wabunge

makoye2009

JF-Expert Member
Jun 12, 2009
2,638
1,218
MAANDAMANO NDIYO DAWA YA KUPINGA ONGEZEKO LA POSHO ZAWABUNGE

Inasikitisha na ni huzuni kubwa kwa jamii ya Watanzaniakusikia kwamba Rais Jakaya Kiwete amebariki na kuridhia ongezeko la Posho kwaWabunge kutoka Tshs .70,000/= mpaka Tshs.200,000/=. Kwa ongezeko hili kilaMbunge sasa ataondoka na kitita cha jumla ya Tshs.330,000/= kwa kila sikuanayokuwepo Bungeni. Hii ni pamoja na kujumlisha Tshs.80,000/=kama posho yakujikimu(perdiem)na Tshs.50,000/= pesa ya mafuta(fuel allowance)inayolipwa kilasiku kwa kila Mbunge aliyeko Bungeni.

Kitendo hiki cha Rais kinaonyesha jinsi Rais Kiweteasivyokuwa na upeo wa kuongoza. Lakini pia kinaonyesha udhaifu wa Serikali yaCCM ambavyo imeshindwa kuongoza nchi hii. Rais Kiwete na Serikali yakewameonyesha DHARAU kubwa sana kwa Watanzania. Kwamba pamoja na malalamiko nakelele za Wananchi na Wanaharakati mbalimbali kupinga posho hizi Kiwete na Serikaliyake wameamua kuridhia ongezeko hilo!

Sasa basi Watanzaniatufanye nini kutokana na kitendo hiki cha dharau, kihuni,kidikteta nakinyonyaji kilichoridhiwa na Rais Kiwete? Jibu nimoja tu: MAANDAMANO.

Haiwezekani kwa namna yoyote ile kudharau na kupuuza maoniya Watanzania ambao ndio wameiweka hii serikali madarakani kwa matumaini kwambaingelikuwa sikivu na kuweza kuwaletea maendeleo Watanzania.
Kuna matukio mengi sana ya kuonyesha kuwa vipato vyaWatanzania walio wengi ni vidogo sana kuanzia Wakulima mpaka Wafanyakazi wataasisi na idara mbalimbali. TUCTA walishaiomba serikali kuongeza Mshahara waKCC (Kima Cha Chini) toka Tshs. 135,000/= mpaka 315,000/kwa mwezi . Badoserikali hii imekataa katakata kwa madai kuwa mshahara huo ni mkubwa sana nahauwezi kulipwa!
Let's use our common sense. Kama kuna mtu anaweza kulipwaTshs. 330,000/= kwa siku kwa maana ya Mbunge,vipi kwa Mfanyakazi anayedaiTshs.315,000/=kwa mwezi siyo kwa siku ishindikane?Kulipa Tshs.330,000/=kwa sikuPESA IPO. Lakini kulipa Tshs.315,000/= kwa mwezi PESA HAIPO!!!!!

Kwa sasa kuna MGOMOWA MADAKTARI nchi nzima wakidai kuboreshewa maslahi yao serikali imekataa kwamaneno kwamba madai yao ni makubwa mno kiasi kwamba seriakli haiwezi kuyamudu. Madaktari bila shaka wamesikia kuwa Rais Kiwete amekubaliWabunge walipwe Tshs 330,000/=kwa siku ilhali madai yao(Madaktari) wanaambiwaserikali haina pesa ya kulipa viwango wanavyodai . Hivi Kiwete na Pinda na serikali yao ya Chama Cha Majambaziwanatarajia nini kutoka kwa Madaktari hawa?
Nahitimisha kwa kusema kuwa sasa ni wakti wa Watanzania KUAMKANA KUPINGA UJINGA HUU WA SERIKALI YA CCM KWA MAANDAMANO MAKUBWA YA NCHI NZIMAMPAKA KIELEWEKE. Naomba Wabunge makini wa CHADEMA waanze kuwasha motohuko Bungeni kuhusiana na Posho hizi za KIFISADI ili Watanzaia wajue kuwawamechoka kuongozwa na Serikali ya majuha!
Nawasilisha.
 
tatizo ni uthubutu wa walio wengi kupinga udhalimu huu na ufedhuli haupo
 
Tulishapata matangangazo mengi ya maandamano huko nyuma sasa hatutaki mnatusumbua . Tukijitokeza hatuoni kitu.
 
Hakuna kitu kibaya kama kusumbua waandamanaji kila tukijitokeza waandaaji mnaingia mitini. Mnacheza na muda wetu. Mimi natangaza rasmi hakuna maandamano.
 
Lakini pia sikubaliana na maandamano ya chama kimoja cha siasa hayana sura ya utaifa.
 
tufanye kama walichofanya wenzetu wa naijeria ndo kitaeleweka vinginevyo ni upuuzi tu!
 
Tulishapata matangangazo mengi ya maandamano huko nyuma sasa hatutaki mnatusumbua . Tukijitokeza hatuoni kitu.
zimekuwa kama verses za bongo flava hazina mashiko, maneno yale yale "mpenzi nakupenda" kwa kila mwimbaji na single zao
 
maandamano ndiyo dawa ya kupinga ongezeko la posho zawabunge

inasikitisha na ni huzuni kubwa kwa jamii ya watanzaniakusikia kwamba rais jakaya kiwete amebariki na kuridhia ongezeko la posho kwawabunge kutoka tshs .70,000/= mpaka tshs.200,000/=. Kwa ongezeko hili kilambunge sasa ataondoka na kitita cha jumla ya tshs.330,000/= kwa kila sikuanayokuwepo bungeni. Hii ni pamoja na kujumlisha tshs.80,000/=kama posho yakujikimu(perdiem)na tshs.50,000/= pesa ya mafuta(fuel allowance)inayolipwa kilasiku kwa kila mbunge aliyeko bungeni.

kitendo hiki cha rais kinaonyesha jinsi rais kiweteasivyokuwa na upeo wa kuongoza. Lakini pia kinaonyesha udhaifu wa serikali yaccm ambavyo imeshindwa kuongoza nchi hii. Rais kiwete na serikali yakewameonyesha dharau kubwa sana kwa watanzania. Kwamba pamoja na malalamiko nakelele za wananchi na wanaharakati mbalimbali kupinga posho hizi kiwete na serikaliyake wameamua kuridhia ongezeko hilo!

sasa basi watanzaniatufanye nini kutokana na kitendo hiki cha dharau, kihuni,kidikteta nakinyonyaji kilichoridhiwa na rais kiwete? Jibu nimoja tu: maandamano.

haiwezekani kwa namna yoyote ile kudharau na kupuuza maoniya watanzania ambao ndio wameiweka hii serikali madarakani kwa matumaini kwambaingelikuwa sikivu na kuweza kuwaletea maendeleo watanzania.
kuna matukio mengi sana ya kuonyesha kuwa vipato vyawatanzania walio wengi ni vidogo sana kuanzia wakulima mpaka wafanyakazi wataasisi na idara mbalimbali. Tucta walishaiomba serikali kuongeza mshahara wakcc (kima cha chini) toka tshs. 135,000/= mpaka 315,000/kwa mwezi . Badoserikali hii imekataa katakata kwa madai kuwa mshahara huo ni mkubwa sana nahauwezi kulipwa!
let's use our common sense. Kama kuna mtu anaweza kulipwatshs. 330,000/= kwa siku kwa maana ya mbunge,vipi kwa mfanyakazi anayedaitshs.315,000/=kwa mwezi siyo kwa siku ishindikane?kulipa tshs.330,000/=kwa sikupesa ipo. Lakini kulipa tshs.315,000/= kwa mwezi pesa haipo!!!!!

kwa sasa kuna mgomowa madaktari nchi nzima wakidai kuboreshewa maslahi yao serikali imekataa kwamaneno kwamba madai yao ni makubwa mno kiasi kwamba seriakli haiwezi kuyamudu. Madaktari bila shaka wamesikia kuwa rais kiwete amekubaliwabunge walipwe tshs 330,000/=kwa siku ilhali madai yao(madaktari) wanaambiwaserikali haina pesa ya kulipa viwango wanavyodai . Hivi kiwete na pinda na serikali yao ya chama cha majambaziwanatarajia nini kutoka kwa madaktari hawa?
nahitimisha kwa kusema kuwa sasa ni wakti wa watanzania kuamkana kupinga ujinga huu wa serikali ya ccm kwa maandamano makubwa ya nchi nzimampaka kieleweke. Naomba wabunge makini wa chadema waanze kuwasha motohuko bungeni kuhusiana na posho hizi za kifisadi ili watanzaia wajue kuwawamechoka kuongozwa na serikali ya majuha!
nawasilisha.

kibali ndo itakuwa tatizo. Lakini hata polisi nadhani hata kama viongozi wao watakataa kuruhusu, nadhani polisi hawatapiga mtu, kwani nao inawahusu sana
 
maandamano sasa basi, silaha haramu ziingizwa hasa mabomu ya kurusha tuilipue bunge. Sasa ni kujitoa mhanga.
 
wako wapi wana jf waliokuwa wanamponda Dr.Ulimboka kwa kitendo chake cha kuongea na vyombo vya habari akitokea mafichoni kuwa si cha kishujaa ila ni woga? naomba sasa wao wawe mstari wa mbele ktk kufanya hayo maandamano ili tujue kuwa wao ndio mashujaa wa ukweli
 
watanzania tumebaki kuwa washadadiaji huku taifa letu linaangamia,na hata watawala wanalielewa ilo ndio maana wanapitisha mambo wanayotaka wao,vijana watanzania wengi hatujitambui na hatuna uthubutu kabisa,tunashindwa kuelewa kua athari hizi zinatugsa sisi moja kwa moja na familia zetu pia,tumebaki kukaa pembeni na kulalamika na kua watumwa wa kushadadia mambo bila kuchukua hatua kuiamsha serikali,hii haitatusaidia kabisa,mbaya zaidi wengine bongo zetu zimeathiriwa vibaya mno hata mambo ya kijinga tunashabaikia na yale ya maana tunayapuuzia,utakuta mtu msomi kabisa anabakia kushadadia siasa kama vile ni simba na yanga,hizi siasa za usimba na yanga zitatufikisha wapi sisi kama taifa?tunashindwa elewa kuwa siasa ni zaidi ya upigaji kelele majukwaani au vijiweni,sias ni maisha.....kwa kweli ili ni taifa linalparaganyika,vijana hatujitambui kabisa.....hii kitu ya wabunge ilitakiwa kupingwa kwa nguvu zote,uwe mfuasi wa tlp,cuf,ccm,udp,cck,cdm au usiwe mfuasi wa chama chochote ili sio jambo la kuliacha na kukaa pembeni kushadadia tu
 
Hizi story za udhalimu wa hii serikali sasa zinatia kichefuchefu..na kila siku ni tuandamane mara tugome mwisho wa siku hakuna cha mgomo wala maandamano...zinachosha sasa!!
 
Masikini, Kikwete! Sikulaumu sana kwa sababu tangu awali ulionesha udhaifu wa kimaamzi, halafu mbaya zaidi washauri wako nao hawakutakii mema wamekuwa wakikupotosha kila mara.
 
Hakuna mwandamanaji Bongo...na hata ukiandamana peke yako au wachache kuonyesha msimamo, waBongo watakuona kichaa na kukudhiaki! Ona yanayotokea kwa madaktari...Bongo ingekuwa nchi ya mwamko, angalau hata ndugu/rafiki au wagonjwa wenye testimonies za dhati jinsi walivyowahi kusaidiwa na madaktari basi wangekuja toa support!
 
Maandamano hayawezekaniki maaana Alshabaab watakuwepo.

Kujitoa muhanga ndio mpango. Lipua V8 zote
 
Maandamano nchi hii ni porojo tu,la msingi kila mtu adai nyongeza ya posho kwenye eneo lake la kazi kama walivyoanza madokta,viongozi hawana uzalendo,pia tatizo ni sisi wananchi kwani zadi ya 75% ya hawa wabunge watarudi tena mjengoni kwanini maandamano yetu tusiyafanye 2015 kwenda kwenye box ka kupigia kura kwa lengo la kuwaondoa ambapo hakuna virungu wala maji ya kuwasha??kwa kufanya hivi watakaoingia watakuwa wamepata somo hivyo watajua umuhimu wa kuwajali wananchi
 
Hakuna mwandamanaji Bongo...na hata ukiandamana peke yako au wachache kuonyesha msimamo, waBongo watakuona kichaa na kukudhiaki! Ona yanayotokea kwa madaktari...Bongo ingekuwa nchi ya mwamko, angalau hata ndugu/rafiki au wagonjwa wenye testimonies za dhati jinsi walivyowahi kusaidiwa na madaktari basi wangekuja toa support!

Na hicho ndicho kinachokatisha tamaa kuhusu watu wetu, hata unapojaribu kuonyesha njia ya kwenda wataiacha serikali na kukugeukia wewe kwa hoja za kijuha oh mdini mara mkabila.....
Watanzania ni umma wa ajabu sana hapa duniani.
Hivi? Sawa vyama vya siasa (upinzani) hatutaki vizungumzie mustakabali wetu kisa "eti vina jichukulia umaarufu (hoja ya kipuuzi sijawahi ona)"
je hizo trade unions ziko wapi??
Maandamano hata ya umma unaojitambua lazima yaongozwe na vyama vya umma.....
Mambo hapa kwetu yanakatisha tamaa sana.
 
Ndugu yangu hakuna maandamano yanayopangwa, labda yenye ruksa na serikali!
 
kibali ndo itakuwa tatizo. Lakini hata polisi nadhani hata kama viongozi wao watakataa kuruhusu, nadhani polisi hawatapiga mtu, kwani nao inawahusu sana

ongeza mshahara wake 1,750,000/=Mimi sielewi tumewachagua wa nini?
 
Nakumbuka Kardinari Policarp Pengo alisema " maandamano sio njia sahihi ya kuwasilisha malalamiko yenu kwa Serikali "

Kazi kwenu.
 
Back
Top Bottom