Maalim Seif: Muungano lazima ujadiliwe

Kwamwewe relax.Inaonekana umepanic.Jambo la msingi nikujadili nakueleweka sentensi yako haieleweki inyooshe ueleweke.Tunakuwekeni mjini then mnataka tuvunje muungano. Embu tuambie sasa kama mnakula kwasababu ya njaa si mtakufa tukiacha kuwalisha?Maana yake ni kwamba bei haitakuwa hii ya sasa mtakuwa mnaimport ambayo huku bara tunaongeza kitu tunaita trade balance kwenu?

WANAOTULETEA NDIO MWISHO HUTULETEA SEMBE HILI TUSIFE NJAA https://www.jamiiforums.com/habari-na-hoja-mchanganyiko/230825-askofu-mwingine-adakwa-na-unga.html
 
Kabla yakuvunjika muunano tujikumbushe terms of trade ya viazi vyetu,maharage na mtama wa maka(mpunga) toka Mbeya na Moro then ndo tuvunje nyie chezeeni supply chain tu mbaya zaidi mnamchezea actor kwenye chain.Kiukweli tende sio menu jamani

Kwani mnatoa bure? Acha utoto huo.
 
Wazanzibar walitakiwa wapewe uhuru wao kwa nini Zanzibar iendelee kutawaliwa na Tanganyika? Mtanganyika anayetaka kuishi zanzibar, si akaombe uraia wa huko? Kuliko kila kukicha ni mikwaruzano tu ya KIGAIDI isio na tija.
 
Hongera sana maalim Seif kuliweka hilo wazi kabisaaaaaaaa tena mchana kweupeeeeeee.

Laazima Mvungano usasambuliwe kwa kina pasi na khofu
.
 
[h=3][/h]

seif-sharif.jpg



Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (Cuf), Maalim Seif Sharif Hamad, amewahimiza wananchi visiwani Zanzibar kujitokeza kwa wingi katika mikutano ya ukusanyaji wa maoni juu ya Katiba mpya na kkuwa huru kueleza aina ya Muungano wanaoutaka.


Akiwa katika ziara ya siku moja ya kukagua uhai wa chama chake kisiwani Pemba jana, Maalim Seif, alisema fursa ya kutoa maoni mbele ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba ni adimu na itakuwa si jambo la busara kwa wananchi kutoitumia vema kwa maslahi ya Zanzibar.


Aliwaambia wananchi kutoka majimbo ya uchaguzi ya Mgogoni na Micheweni waliokusanyika huko Mapofu Wingwi, mkoa wa Kaskazini Pemba kuwa, katika miaka 48 ya muungano wananchi hawajapata fursa kama hiyo, hivyo wasikubali kuitupa, kwani inaweza isitokee tena katika muda ujao wa uhai wao.


“Kwa mtazamo wangu ajenda kuu kwa Wazanzibari katika mchakato wa kuandika Katika mpya ni muungano, kwa sababu Zanzibar inayo Katiba yake ya mwaka 1984,” alisema Maalim Seif ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar.


Aliwakumbusha wananchi kwamba, Katiba ya Zanzibar inajumuisha mambo mengi yanayogusa maslahi ya Wazanzibari, kama vile haki za binaadamu na mgawanyo wa madaraka.


Mwakilishi wa Mgogoni, Abubakar Khamis Bakary kwa upande wake aliwataka wananchi kuwa na imani na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

Alisema wananchi wawe na imani kwa sababu kisheria tume hiyo itaheshimu maoni yao na kwamba hakuna namna utendaji wa chombo hicho unaweza kuruhusu udanganyifu.

Source: Nipashe
 
Sisi hatutaki Muungano Huu Fake Usituzinguwe Bwana, Wazanzibar Hatutaki Serekali 2 Wala 3 Ni kuvunja tu Muungano Mambo ya Muungano niyenu Wana siasa mukikaa mukila mapencheni huku Wazanzibar tukila hilaki.

Hivi sasa sisi sio wafuasi wa chama ni waumini wa Muamsho vyama vimeshindwa kutuletea tulitakalo Wazanzibar nazani Seif umeona Nguvu ya Uamsho inavyofanya kazi.
 
Sisi hatutaki Muungano Huu Fake Usituzinguwe Bwana, Wazanzibar Hatutaki Serekali 2 Wala 3 Ni kuvunja tu Muungano Mambo ya Muungano niyenu Wana siasa mukikaa mukila mapencheni huku Wazanzibar tukila hilaki.

Hivi sasa sisi sio wafuasi wa chama ni waumini wa Muamsho vyama vimeshindwa kutuletea tulitakalo Wazanzibar nazani Seif umeona Nguvu ya Uamsho inavyofanya kazi.

"Sis"? Shuleni nlifundishwa nisimsemee mtu. Kakke mi pia mzanzibari lakini naona ukisema kuwa eti sio wafuasi wa chama hapo naona utakuwa unajisita, hebu itizame hio picha kisha watizame hao waliopo na mavazi yao kisha ndo utajua kama ni wafuasi wa chama au UAMSHO! Naomba urikodi maneno nnayokwambia na utakuja kuyakumbuka. Ikifika 2015 mtakitokeza kwa wingi kuwapigia kura hao hao ambao unasema kuwa mmechoka nao (vyama vya siasa)
 
Maalim Seif Sharif Hamad anahutubia
mkutano mkubwa wa hadhara kisiwani
Pemba sasa hivi na anasema: "Mimi sitafuni
maneno kwamba ni muumini wa Zanzibar
yenye mamlaka kamili kitaifa na kimataifa
itakayofuatiwa na mashirikiano kati yake na
Tanganyika kupitia Muungano wa Mkataba.
Namshangaa leo anakuja kiongozi wa
Zanzibar anasema tuna bendera na muhuri
na wimbo wa taifa, hayo yanatosha. Hivi
huyu anajua anachokisema au anatumikia
maslahi ya waliomtuma? Una bendera gani
hii ambayo mwisho wake Chumbe? Mimi
nataka niione bendera ya Dola ya Zanzibar
inapepea Umoja wa Mataifa, New York pale.
Nataka tuwe na Paspoti ya Zanzibar,
nikisafiri nitoe Paspoti ya nchi yangu.
Nataka tuwe na Ofisi za Kibalozi za Zanzibar
katika nchi za nje. Leo hata mamlaka ya
kiuchumi hatuna. Tumeamua rasilimali yetu
ya mafuta na gesi asilia yasiwe mambo ya
Muungano, mpaka leo Tanganyika
wamekwamisha, wanatuzuia tusinufaike na
rasilimali zetu tukajenga uchumi wetu.
Wanasema tuna viwango na mfumo mmoja
wa kodi lakini bidhaa zikitoka Zanzibar
wanazitoza ushuru tena. Lengo ni kuua
uchumi wetu ili hatimaye tudhoofike na
tusalimu amri kwao. Yaguju! Wasahau hilo.
Leo hata katika mikutano ya kimataifa,
viongozi wetu wa Zanzibar hawapewi
heshima ya uwakilishi wa nchi yetu. Inafika
mahala hata Naibu Waziri tu wa Bara
anaongoza ujumbe wa Tanzania wakati kuna
Waziri kamili kutoka Zanzibar lakini
haheshimiwi. Tutarejesha mamlaka yetu
kamili. Tuwe na Benki Kuu, tuwe na sarafu
yetu ya Zanzibar, tupange uchumi wetu kwa
maslahi ya watu wetu. Tunataka tuwe na
uanachama katika jumuiya na mashirika
yote ya kimataifa. Tuwe na Waziri wa
Mambo ya Nje wa Zanzibar. Tuwe na uwezo
wa kuingia mikataba na nchi za kigeni. Hayo
ndiyo tunayoyataka. Tukisema hivi hatuna
maana tunataka ugomvi na Tanganyika.
Hapana! Tunataka tuwe majirani wema na
Tanganyika kama tutakavyokuwa na ujirani
mwema na Kenya. Hayo yatafikiwa kupitia
Muungano wa Mkataba wa Madola mawili
huru kamili."
Posted by Ismail Jussa.
 
hapa ndipo ninapoona hadhi ya Urais inaposhuka angekuwapo mtu kama Lowassa au Mkapa tusingemiskia huyu mwenye sura mbili akiongea huu upuuzi!
 
Hawa jamaa walalamishi, duh!!

Nyumba na mashamba walioyarundika huku Dar wangeyauza kwanza kisha waanze kudai Znz yao. Nataka kusema, wanawadanganya maskini wa Unguja na Pemba, hali ya hewa ikibadilika kidogo tu, wote huruka kwa chopa na kujificha Dar.

Madaraka matamu sana.
 
hapa ndipo ninapoona hadhi ya Urais inaposhuka angekuwapo mtu kama Lowassa au Mkapa tusingemiskia huyu mwenye sura mbili akiongea huu upuuzi wakati yupo madarakani!
 
Maalim Seif Sharif Hamad anahutubia
mkutano mkubwa wa hadhara kisiwani
Pemba sasa hivi na anasema: "Mimi sitafuni
maneno kwamba ni muumini wa Zanzibar
yenye mamlaka kamili kitaifa na kimataifa
itakayofuatiwa na mashirikiano kati yake na
Tanganyika kupitia Muungano wa Mkataba.
Namshangaa leo anakuja kiongozi wa
Zanzibar anasema tuna bendera na muhuri
na wimbo wa taifa, hayo yanatosha. Hivi
huyu anajua anachokisema au anatumikia
maslahi ya waliomtuma? Una bendera gani
hii ambayo mwisho wake Chumbe? Mimi
nataka niione bendera ya Dola ya Zanzibar
inapepea Umoja wa Mataifa, New York pale.
Nataka tuwe na Paspoti ya Zanzibar,
nikisafiri nitoe Paspoti ya nchi yangu.
Nataka tuwe na Ofisi za Kibalozi za Zanzibar
katika nchi za nje. Leo hata mamlaka ya
kiuchumi hatuna. Tumeamua rasilimali yetu
ya mafuta na gesi asilia yasiwe mambo ya
Muungano, mpaka leo Tanganyika
wamekwamisha, wanatuzuia tusinufaike na
rasilimali zetu tukajenga uchumi wetu.
Wanasema tuna viwango na mfumo mmoja
wa kodi lakini bidhaa zikitoka Zanzibar
wanazitoza ushuru tena. Lengo ni kuua
uchumi wetu ili hatimaye tudhoofike na
tusalimu amri kwao. Yaguju! Wasahau hilo.
Leo hata katika mikutano ya kimataifa,
viongozi wetu wa Zanzibar hawapewi
heshima ya uwakilishi wa nchi yetu. Inafika
mahala hata Naibu Waziri tu wa Bara
anaongoza ujumbe wa Tanzania wakati kuna
Waziri kamili kutoka Zanzibar lakini
haheshimiwi. Tutarejesha mamlaka yetu
kamili. Tuwe na Benki Kuu, tuwe na sarafu
yetu ya Zanzibar, tupange uchumi wetu kwa
maslahi ya watu wetu. Tunataka tuwe na
uanachama katika jumuiya na mashirika
yote ya kimataifa. Tuwe na Waziri wa
Mambo ya Nje wa Zanzibar. Tuwe na uwezo
wa kuingia mikataba na nchi za kigeni. Hayo
ndiyo tunayoyataka. Tukisema hivi hatuna
maana tunataka ugomvi na Tanganyika.
Hapana! Tunataka tuwe majirani wema na
Tanganyika kama tutakavyokuwa na ujirani
mwema na Kenya. Hayo yatafikiwa kupitia
Muungano wa Mkataba wa Madola mawili
huru kamili."
Posted by Ismail Jussa.

Hii sijaelewa imekaaje, ni Maalimu mwenyewe kasema haya? Au Jussa anamwekea maneno mdomoni? Kama ni yeye basi sisi wadanganyika tuna kila sababu ya kusheherekea ushindi maana siku sii nyingi tutapata uhuru kamili na kuachana na hawa za Zenji,
 
Sultani ndo ameamua kufknguka, huo ndo ukweli anawahutubia wenye chama chao, hapo nafikiri waarabu wa oman na iran wamefurahi kwa uwakilishi mzuri toka kwa jussa na sultan au mtume wa cuf!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom