Maalim Seif: Muungano lazima ujadiliwe

Maalim Seif: Muungano lazima ujadiliwe

EasyFit

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2011
Posts
1,269
Reaction score
1,082
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, amesema hakuna mambo yaliyoainishwa kuwa ni matakatifu ambayo hayatakiwi kuguswa wakati wa kujadili Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano, hivyo aliwataka Wazanzibari wajiandae kutoa maoni yao juu ya Katiba wanayoitaka, ikiwamo mfumo wa Muungano wenye masilahi kwao.

Alisema kutokana na Rais Jakaya Kikwete kutia saini muswada uliopitishwa na wabunge kuhusu katiba mpya, hatua inayofuata ni kuundwa tume ya kuratibu maoni ya wananchi juu ya katiba hiyo, na wananchi wanapaswa kujiandaa kutoa maoni bila woga, bali la muhimu ni kuhakikisha katika maoni yao hawatoi lugha chafu.

Alisema tume hiyo itakayokuwa na wajumbe wanaotoka Zanzibar na Tanzania Bara, itatoa fursa ya kipekee kwa wananchi wa Tanzania, hivyo itakuwa nafasi ya kipekee kwa Wazanzibari kueleza nini wanataka, likiwamo suala la mfumo au muundo wa Muungano.

“Nyinyi Wazanzibari na ndugu zetu wa Tanzania Bara ndio tuliovaa kiatu (Muungano) na aliyevaa kiatu ndiye anayejua msumari unachomea wapi, au anayelala kwenye kitanda ndiye anayejua kunguni wake,” alisema Maalim Seif.

Hata hivyo, alisema kwamba litakuwa ni jambo la maana zaidi Wazanzibari wakiwa na msimamo mmoja juu ya mambo wanayotaka katika katiba mpya na waweke kando itikadi zao za kisiasa katika jambo hilo.

Alieleza kwamba ni vema wakaendelea na na msimamo kama ule waliouonesha wakati wa kutoa maoni juu ya rasimu ya muswada wa katiba mpya ulioandaliwa mara ya kwanza, kabla ya kuwasilishwa bungeni, ambapo Wazanzibari kwa kauli moja waliupinga na ukarekebishwa.
 
Hofu yangu ni baadhi ya watu kuburuzwa kukidhi matakwa ya kundi linalotaka kauli moja! kanakwamba wanasomeshwa a e i o uuu!
 
.....mpaka hapa tulipofikia, yaani kusainiwa kwa muswada na kuwa sheria, wazanzibari wameshinda, walikuwa wamoja, waliweka mambo walioyaona ni ya msingi kama taifa (zanzibar), tumebaki sisi huku Tanganyika, na akina sendeka wetu, akina rage wetu, (kwa uchache) ambao fikra zao ni posho tu na sio Tanzania ya kesho (mtazamo wangu, mm nawaona hivyo)
 
Tanganyika tutakuwa wamoja siku mkuu wa nchi akiwa mzanzibar na pengine ndipo Tanganyika itazaliwa upya.

That's nature.....

Nje ya hapo tupate kiongozi ambaye hana masilahi ktk mfumo wa sasa
 
hakuna umoja utakao endelea kama CCM hawatakubali kubadilisha sheria ambazo zimemlimit mwananch wa kawaida kuwa huru ktk mchakato mzima wa katiba mpya. na wasipokuwa makini lazima damu imwagige nchi hii.
 
watanganyika kazi yao kugonga meza kama majuha,wako kichama zaidi maskini hawaelewi umuhimu wa katiba tunayotaka kutunga.......go maalim seif go ili wadanganyika wapate akiri waache ushabiki wa kipuuzi.......ili baadae wakizinduka tuzichape!!!!!
 
Hakuna mtu atakayetuzuia kuzungumzia Tanganyika yetu. Tutaizungumzia hata usiku wa manane wakati wao wamelala.
Tunaidai Tanganyika na lazima itapatikana. Haiwezekani tuwe koloni la zanzibar. I say haiwezekani. Ni muda tu ngoja tuone.
 
Siyo muda mrefu Zanzibar itafunguwa minyororo ya mkoloni mweusi
 
Wazanzibar wapo huru kujadili muungano, na kutoa maoni yao katika tume ya katiba mpya, na wao kama serekali (SUK) wanawaunga mkono.

source ITV habari mudamfupi uliopita leo.
 
Wazanzibar wapo huru kujadili muungano, na kutoa maoni yao katika tume ya katiba mpya, na wao kama serekali (SUK) wanawaunga mkono.

source ITV habari mudamfupi uliopita leo.

Naunga mkono hoja.
 
mwache ajimalize mwenyewe huyo mroho wa madaraka na muuaji wa Cuf bara na asiependa kuguswa
 
Kabla yakuvunjika muunano tujikumbushe terms of trade ya viazi vyetu,maharage na mtama wa maka(mpunga) toka Mbeya na Moro then ndo tuvunje nyie chezeeni supply chain tu mbaya zaidi mnamchezea actor kwenye chain.Kiukweli tende sio menu jamani
 
kabla yakuvunjika muunano tujikumbushe terms of trade ya viazi vyetu,maharage na mtama wa maka(mpunga) toka mbeya na moro then ndo tuvunje nyie chezeeni supply chain tu mbaya zaidi mnamchezea actor kwenye chain.kiukweli tende sio menu jamani

kwani kabla ya huo muungano unafikiri watu wakila hayo maharage na viazi na ugali , hivi vinaliwa kwa sababu ya njaa tu ???

Ugali watu hata walikuwa hawali , sembe wakila wafungwa
 
Kwamwewe relax.Inaonekana umepanic.Jambo la msingi nikujadili nakueleweka sentensi yako haieleweki inyooshe ueleweke.Tunakuwekeni mjini then mnataka tuvunje muungano. Embu tuambie sasa kama mnakula kwasababu ya njaa si mtakufa tukiacha kuwalisha?Maana yake ni kwamba bei haitakuwa hii ya sasa mtakuwa mnaimport ambayo huku bara tunaongeza kitu tunaita trade balance kwenu?
 
Yeye ni nani Tanzania hii? Ikiwa Shein ni Wazari yeye ni katibu wa kata? Eti wanajidanganya na ma vyeo hewa tu
 
Back
Top Bottom