Maalim Seif: Haturudii Uchaguzi

Maalim Seif: Haturudii Uchaguzi

Kwa taarifa zinavyojionesha uchaguzi uliofanyika ulikuwa na figisu nyingi ikiwemo mawakala wa vituo kutohudhuria kwa baadhi ya vituo na wapiga kura kuzidi idadi waliojiandikisha.

Leo wanadai eti hawawezi kurudia kupiga kura.

Hilo linaonekana kuleta vurugu Zanzibar tumekoma sisi wananchi hatutaki vurugu wafanye wao viongozi.sisi tunaendelea na kazi zetu hatuhitaji uvunjifu wa amani.

Wewe siyo mzanzibar, umevurugwa na umamluki wa ccm.
 
CCM ...huwa mnamatatizo kura za rais wa mungano halal ila rais wa zanzibar haramu..nimeamin kwel ccm ......ni ilelile......
Nyama haramu lakini mchuzi wake halali, kweli CCM ni ile ile lakini namba haisomeki.
 
Katiba hovyo ndio inawatesa ccm. Imagine cuf akashinda then anaingia baraza la mawaziri la jamhuri
 
Kwa taarifa zinavyojionesha uchaguzi uliofanyika ulikuwa na figisu nyingi ikiwemo mawakala wa vituo kutohudhuria kwa baadhi ya vituo na wapiga kura kuzidi idadi waliojiandikisha.

Leo wanadai eti hawawezi kurudia kupiga kura.

Hilo linaonekana kuleta vurugu Zanzibar tumekoma sisi wananchi hatutaki vurugu wafanye wao viongozi.sisi tunaendelea na kazi zetu hatuhitaji uvunjifu wa amani.
Haya, ninyi wananchi endeleeni na shughuli zenu, kwani kuna aliyewazuia? Kama mnadhani mnapingana na 'viongozi wenu' nendeni mkafanye uchaguzi. maalim Seif akiamua kutoshiriki uchaguzi kwa sababu zake za msingi, hakuna anayewazuia kwenda kupiga kura na kuchagua wagombea wa byama vingine watakaoshiriki. Hapo vurugu itatoka wapi?
 
Magufu akikusikia basi utajuta yaani unataka kumuharibia mlo ,

Je mtakubali uchaguzi usimamiwe na UN kuanzia A mpaka Z ,huko Zanzibar tu ! CUF wapo tayari kwa hilo !


Hata Tanzania bara warudie tu.
Hakuna namna.
 
Kwa taarifa zinavyojionesha uchaguzi uliofanyika ulikuwa na figisu nyingi ikiwemo mawakala wa vituo kutohudhuria kwa baadhi ya vituo na wapiga kura kuzidi idadi waliojiandikisha.

Leo wanadai eti hawawezi kurudia kupiga kura.

Hilo linaonekana kuleta vurugu Zanzibar tumekoma sisi wananchi hatutaki vurugu wafanye wao viongozi.sisi tunaendelea na kazi zetu hatuhitaji uvunjifu wa amani.


Kama kweli upos erious tufute uchaguzi wa Muungano, maana hao mawakala unaowaktaa ndio walisimamia kura za muungano pia.
 
Hata Tanzania bara warudie tu.
Hakuna namna.

Kwa taarifa zinavyojionesha uchaguzi uliofanyika ulikuwa na figisu nyingi ikiwemo mawakala wa vituo kutohudhuria kwa baadhi ya vituo na wapiga kura kuzidi idadi waliojiandikisha.

Leo wanadai eti hawawezi kurudia kupiga kura.

Hilo linaonekana kuleta vurugu Zanzibar tumekoma sisi wananchi hatutaki vurugu wafanye wao viongozi.sisi tunaendelea na kazi zetu hatuhitaji uvunjifu wa amani.



Tangu lini kasoro kwenye baadhi ya maeneo zikasababisha kufutwa kwa uchaguzi nchi nzima bila hata majadiliano?
Mbona hata bara palikua na kasoro nyingi na malalamiko mengi ikiwa ni pamoja na kukamatwa kwa masanduku ya kura zilizopigwa tayari lakini uchaguzi haukurudiwa .
Kama kuna maeneo walikiuka utaratibu mbona zipo hatua na adhabu za kutoa ikiwa ni pamoja na kurudia maeneo husika tu na sio nchi nzima.
Je,haki ya wale waliopiga kura zao kwa uhakika kwenye maeneo yasio na kasoro imepotezwa kwa misingi gani?

Je,ni tume ipi itakayosimamia uchaguzi wa marudio ikiwa hiyo ZEC ikeshindwa?
Kwa nini wajumbe na mwenyekiti wa ZEC wasijiuzulu na kupisha wengine wenye uwezo wa kutenda haki ?
 
Magufu akikusikia basi utajuta yaani unataka kumuharibia mlo ,

Je mtakubali uchaguzi usimamiwe na UN kuanzia A mpaka Z ,huko Zanzibar tu ! CUF wapo tayari kwa hilo !
Zanzibar haitambuliki UN.kazi ya UN ni ushauri tu
 
Kwa taarifa zinavyojionesha uchaguzi uliofanyika ulikuwa na figisu nyingi ikiwemo mawakala wa vituo kutohudhuria kwa baadhi ya vituo na wapiga kura kuzidi idadi waliojiandikisha.

Leo wanadai eti hawawezi kurudia kupiga kura.

Hilo linaonekana kuleta vurugu Zanzibar tumekoma sisi wananchi hatutaki vurugu wafanye wao viongozi.sisi tunaendelea na kazi zetu hatuhitaji uvunjifu wa amani.

Huna toafauti na binadamu aliyeishi zama za mawe ie Zinjathropus! Wagombea ie CCM na CUF hakuna aliyelalamika kwamba uchaguzi ulivurugwa.

Msimamizi wa uchaguzi ie ZEC ambaye ndiye anapaswa kusimamia uchaguzi usivurugike ndiye analalamika kwamba uchaguzi UMEVURUGWA!

Ndiyo maana Moi aliwahi kutudhihaki kwamba Nyerere anaongoza MAITI na hakuna uwezekanao wa MAITI hao kukufuka!
 
Hakuna haja ya kurudia uchaguzi kwa sababu zifuatazo:

=> kura za rais bara zilionekana si haramu ila tu kura za urais zanziba haramu aliyepiga kura atajiuliza ile moja imehesabiwa kwanini hii nyingne ikataliwe? Wakati mpigaji ni huyo huyo!!

=>jana nec imetangaza cuf imepata kura 1.2 milion za wabunge wote, kwa kura hizo imepata wabunge vitimaalum (10) jiulize idadi hiyo ya kura ni tanzania bara tu! Au na visiwani? Na kama nina visiwani si ilitangazwa wamefuta uchaguzi?

=> tusubiri tar 17 novemba kufunguliwa kwa bunge, je wawakilishi wa zanziba hawatakuwepo? Wakiwepo uchaguzi haujafutwa!
 
Baba Mkali utanielewa unavyokusudia kunielewa, lakini mimi najaribu kufikiri kwa maandishi; Uchaguzi maana yake ni kutaka kuwauliza wananchi swali lifuatalo; Ni sera zipi na za chama gani wanazipenda? Wananchi wanalijibu swali hili kupitia sanduku la kura. Kama wakizipenda sera za CUF, watawapigia kwa kura nyingi za ndiyo. Tunapowalazimisha wananchi wakubali hili au lile siyo demokrasia. Hii ni kwa vyama vyote bila kujali ni CCM au ni CUF. Tunapofanya ujanja wowote kinyume cha sauti ya wananchi siyo demokrasi. Kadhalika unapomlazimisha mke wako au mtoto wako au jirani yako akubaliane na sera zako kwa nguvu siyo demokrasia. Sasa hoja yangu ni kuwa kama kweli uchaguzi ule ulikuwa huru na wote waliokipigia kura ya ndiyo CUF, hata tukirudia uchaguzi tena katika mazingira huru na ya haki nina imani watashinda tu. Kama kuna madudu waliyafanya ili washinde yakidhibitiwa hawatashinda watashindwa. Labda hili ndiyo linaloleta shida. Nakumbuka msomi mmoja alisoma Urusi shahada ya pili yaani Masters. Chuo Kikuu cha Dar es Salaam walikataa kumtambua. Yule msomi alisema nipeni mtihani. Akapewa. Waliposahihisha wakasema kweli ana shahada ya pili. Ukiona mtu anawasiwasi juu ya ushindi wake, inatia shaka huenda ushindi wake una walakini kweli. Hii itakuwa inamjenga zaidi mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi Zanzibar Jecha.
Hapo sijatetea chama chochote. Kwa upande wa CCM hali kadhalika, kama wameshindwa kihalali watashindwa tena. La kuvunda halina ubani. Sasa kaka yangu Baba Mkali upo wapi uegemezi wa upande mmoja kwenye hoja hizi? Jaribu somo kwa utulivu, utaelewa.
Kuna makada wawili STDVII na bantulile wanajitahidi kweli kutetea uamauzi wa Jescha lakini hata trained dog can establish Jecha flows...kwa hili ndugu zangu kwa sheria na kanuni Jecha amechemka, wadau wamewajibu kwa hoja thabiti kabisa.

Kilichobaki ni CCM kutumia ubabe na mabavu kurudia uchanguzi. Wote tunajua matokeo ya ubabe na dhulma. Wataiingiza Z'bar katika machafuko yasiyo ya lazima.
 
Ataapishwa trh 5/11/20......25 haaa Ccm noma sana ili iwepo Democratic sssss nilazima Ccm ishinde isipo shinda ujue haki haikutendeka so lazima uludiwe

Hivi Maalim kama kweli alishinda hata uchaguzi ukirudiwa si atashinda tu? asiwe na hofu.
 
Maalim Seif anazo nakala za matokeo. Je; ni utaratibu mgombea mmoja wapo kupewa nakala za matokeo? Ilikuwaje yeye akawa nazo wakati ana wawakilishi? Hii haithibitishi kuwa makamishena wa ZEC waligeuka kuwa wawakilishi wa vyama vyao. Pale idadi ya kura zinazidi wapiga kura waliojiandikisha katika daftari la wpiga kura, ZEC ifanye nini aeleze Maalim Seif. Pale kura zimefutwa futwa, inajulikana kuwa kura hizo zitakuwa zimeharibika na hapewi mgomba yeyote, je; hii ikionekana kupunguza kura zake itakuwaje

Mimi najaribu kusoma comment yako nakosa jibu huyu alikuwa na mawakala na kila chama kina wakala na kila wakala anapewa nakala ambayo ni kopi ya matokeo nyingine inabandikwa sasa yeye mawakala wake wamempatia boss wao so kosa liko wapi ? Na kila nakala imesainiwa na mawakala wote tuwe weledi tuache upole pole humu sawa
 
Nijuavyo mimi nakala za matokeo ziliztiwa saini na mawakala wa pande zote zinawasilishwa kwa Tume ya uchakuzi kama ushahidi kuwa matokeo yale ni halali na yamethibitishwa na pande zote shindani. Washindani wote wanasubiri Tume iyafanyie mchakato ikiwa ni kuhakiki, kuyajumlisha na aadaye kumtangaza mshindi. Nakala za matokeo za mawakala zinaweza kutumika kama kutakuwa na malalamiko yoyote. Sheria iko wazi mwenye mamlaka ya kutanganza mshindi ni Tume na siyo mshindania nafasi katika uchaguzi. Mimi ninavyoona na kwa maoni yangu ni kosa kumpatia matokeo mgombea mmojawapo kabla ya Tume kumtangaza. Msingi wa Maalim Seif kujitangaza mshindi kunatokana na kupewa matokeo kabla ya Tume. Tukiruhusu mgombea kujianga mshindi kuna hatari siku moja Maalim Seif atajiapisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania badala ya kuapishwa na Jaji kama sheria inavyotaka. Jambo hili msilione kwa wepesi kiasi hico mchelea mwana kulia hulia yeye. Hapa kuna uvunjivu wa sheria ulio wazi kabisa. Ikiwa Maalim Seif anagombea tu, hajawa Rais, akiwa Rais itakuwaje? Yeye mwenyewe atavunja sheria, pia atashindwa kuwaambia wasaidizi wafuate sheria. Nchi itakuwa ya vituko kweli kweli.
Lakini huyu huyu Maalim Seif katika kipindi cha utawala wa Abdul Jumbe amewahi kuvujisha siri za serikali mapinduzi ya Zanzibar. Mtu asiye tii sheria, asiyefuata maelekezo ya boss wake, asiyetii hata miongozo anakuwa rais wa namna gani? Kila uchaguzi anang'ang'ania kwenda Ikulu, ameweka nini. Nakumbuka nilipokuwa shule vijana wakorofi walikuwa wakipendwa zaidi na wanafunzi wenzao, isije ikawa na huyu anapendwa kwa ukorofi wake, lakini si kwa kuwaletea maendeleo wazanzibar. Maneno mengi mdomoni siyo mojawapo ya sifa za kiongozi bora
Mimi najaribu kusoma comment yako nakosa jibu huyu alikuwa na mawakala na kila chama kina wakala na kila wakala anapewa nakala ambayo ni kopi ya matokeo nyingine inabandikwa sasa yeye mawakala wake wamempatia boss wao so kosa liko wapi ? Na kila nakala imesainiwa na mawakala wote tuwe weledi tuache upole pole humu sawa
 
Nijuavyo mimi nakala za matokeo ziliztiwa saini na mawakala wa pande zote zinawasilishwa kwa Tume ya uchakuzi kama ushahidi kuwa matokeo yale ni halali na yamethibitishwa na pande zote shindani. Washindani wote wanasubiri Tume iyafanyie mchakato ikiwa ni kuhakiki, kuyajumlisha na aadaye kumtangaza mshindi. Nakala za matokeo za mawakala zinaweza kutumika kama kutakuwa na malalamiko yoyote. Sheria iko wazi mwenye mamlaka ya kutanganza mshindi ni Tume na siyo mshindania nafasi katika uchaguzi. Mimi ninavyoona na kwa maoni yangu ni kosa kumpatia matokeo mgombea mmojawapo kabla ya Tume kumtangaza. Msingi wa Maalim Seif kujitangaza mshindi kunatokana na kupewa matokeo kabla ya Tume. Tukiruhusu mgombea kujianga mshindi kuna hatari siku moja Maalim Seif atajiapisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania badala ya kuapishwa na Jaji kama sheria inavyotaka. Jambo hili msilione kwa wepesi kiasi hico mchelea mwana kulia hulia yeye. Hapa kuna uvunjivu wa sheria ulio wazi kabisa. Ikiwa Maalim Seif anagombea tu, hajawa Rais, akiwa Rais itakuwaje? Yeye mwenyewe atavunja sheria, pia atashindwa kuwaambia wasaidizi wafuate sheria. Nchi itakuwa ya vituko kweli kweli.
Lakini huyu huyu Maalim Seif katika kipindi cha utawala wa Abdul Jumbe amewahi kuvujisha siri za serikali mapinduzi ya Zanzibar. Mtu asiye tii sheria, asiyefuata maelekezo ya boss wake, asiyetii hata miongozo anakuwa rais wa namna gani? Kila uchaguzi anang'ang'ania kwenda Ikulu, ameweka nini. Nakumbuka nilipokuwa shule vijana wakorofi walikuwa wakipendwa zaidi na wanafunzi wenzao, isije ikawa na huyu anapendwa kwa ukorofi wake, lakini si kwa kuwaletea maendeleo wazanzibar. Maneno mengi mdomoni siyo mojawapo ya sifa za kiongozi bora

Bantulile wewe unauwelewa wa mambo mengi ila kwenye hili Ccm wamezoeya kuiba sana na waga hawashindwi je kwa mfano malimu angekuwa anagombea kupitia Ccm je haya yote yange jitokeza?
 
uchaguzi wa zanzibar ni fundisho kubwa kwa serikali ya muungano ,binafsi nimejifunza siasa za zanzibar kidogo
 
Back
Top Bottom