Maalim Seif: Haturudii Uchaguzi

Maalim Seif: Haturudii Uchaguzi

Ni vizuri asusie kurudia uchaguzi.wengine WATAENDELEA na hutasikia vurugu za kijitangazia USHINDI,kuhamishia mabox ya kura maskani,kunyima baadhi ya mawakala vitambulisho na makamishina kutwangana
 
Hadi raha....tunapewa ushindi zanzibar...tunavunja muungano...rais magufuri na makamu wake wanakuwa hawana maana tena..tunarudia uchaguzi kwa tz bara ili kumpata rais wa tanganyika....then ukawa tunachukua tanganyika.... Baada ya hapo wazanzibar wanaomba muungano teno baada ya ukawa kushinda tanganyika
 
Hivi UKAWA bado ipo?
Hadi raha....tunapewa ushindi zanzibar...tunavunja muungano...rais magufuri na makamu wake wanakuwa hawana maana tena..tunarudia uchaguzi kwa tz bara ili kumpata rais wa tanganyika....then ukawa tunachukua tanganyika.... Baada ya hapo wazanzibar wanaomba muungano teno baada ya ukawa kushinda tanganyika
 
Seif si atoe hayo makaratasi ya matokeo watu wajumlishe...............
 
Maalim Seif anazo nakala za matokeo. Je; ni utaratibu mgombea mmoja wapo kupewa nakala za matokeo? Ilikuwaje yeye akawa nazo wakati ana wawakilishi? Hii haithibitishi kuwa makamishena wa ZEC waligeuka kuwa wawakilishi wa vyama vyao. Pale idadi ya kura zinazidi wapiga kura waliojiandikisha katika daftari la wpiga kura, ZEC ifanye nini aeleze Maalim Seif. Pale kura zimefutwa futwa, inajulikana kuwa kura hizo zitakuwa zimeharibika na hapewi mgomba yeyote, je; hii ikionekana kupunguza kura zake itakuwaje
Nami nafikiri Maalim Seif ilimbidi ajibie hizi kesi maana kiukweli zimeleta mitazamo tofauti so kwakuwa yeye anazo zile copy za matokeo ambazo alikusanya atuambie kuwa ZEC ni waongo na haweke bayana juu ya tuhuma za kuzidi wapiga kura
 
Naam tuanzie hapo Maalimu Seif alete majibu, vinginevyo hakuna namna Uchaguzi lazima urudiwe.

STDVII naona na wewe unaleta hoja za Kijinga kabisa hapa. Ngoja nitoe ufafanuzi kidogo.

1/ZEC imetoa sababu 8 za kufuta uchaguzi, sababu zote hizo ni kijinga kabisa, zote zimetolewa majibu na Seif na pia watu mbalimbali.
Kwa kifupi hizo sababu hazina mashiko kabisa. Kwa mfano.

(A)Wajumbe wa ZEC kuvua mashati na kupigana. Hii sio sababu ya kuweza kufuta uchaguzi. Ugomvi wa wajumbe(kama kweli ulikuwepo) kamwe hauwezi kuwa ni kasoro katika uchaguzi.

(B)Mtu kujitangazia ushindi kabla ya matokeo rasmi.(Hii sio sababu ya kuufanya uchaguzi uwe na kasoro, hizo ni siasa tu)

(C)Fujo kutokea katika vituo vya kupigia kura.(Vituo vyote vilikuwa na ulinzi mkubwa sana wa askari wenye silaha, hakuna matukio ya Fujo yaliyoripotiwa na Polisi, vyombo vya habari nk. Sasa ZEC wamepata wapi hizo taarifa?).

(D)Kuwepo kwa watu waliopiga kura ambao majina yao hayakuwemo kwenye Daftari.
(Hili ndio haliwezekani kabisa, ZEC ndio wasimamizi wa kupiga kura, sasa nani aliwaruhusu hao watu wapige kura, kwanini mawakala wasilalamike katika hilo?)

(E)Idadi ya watu waliopiga kura kuzidi idadi ya waliojiandikisha.
(Huu ndio uwongo wa wazi kabisa, ZEC imeambiwa itoe matokeo yote ya vituo ili tukione hicho lakini mpaka sasa wameshindwa, CUF wametoa matokeo yote waliyokusanya kituo kwa kituo, jimbo kwa jimbo, na hiyo kasoro haipo kabisa, mpaka sasa hakuna kituo chochote ambacho vote turnout ilifika zaidi ya Asilimia 90, sasa tume wamepata wapi hayo?)

2/Hakuna kikao chochote cha ZEC kilikaa na kuamua kuufuta uchaguzi wa Zanzibar. Ni mwenyekiti mwenyewe wa ZEC aliibuka na kuufuta uchaguzi, kanuni na sheria za ZEC zinataka maamuzi yoyote ni lazima yaafikiwe kwanza na wajumbe wa ZEC wasiopungua 5 kati ya Wajumbe6. Nani kamtuma Jesha kuufuta uchaguzi wa Zanzibar?

3/ZEC imeundwa kisheria na imepewa mamlaka yake kisheria. Hakuna sheria inayoipa ZEC mamlaka ya kuufuta uchaguzi wote wa Zanzibar kwa kigezo cha kasoro, Fujo nk.
Mpaka sasa ZEC imeshindwa kusema ni sheria gani wameitumia ili kufuta uchaguzi wa Zanzibar.
 
Last edited by a moderator:
Seif si atoe hayo makaratasi ya matokeo watu wajumlishe...............

Nenda mzalendo.net soma post majumuisho ya wana diaspora. Matokeo ya majimbo 31 yaliyotangazwa na ZeC yanakubalina na majumuisho ya cuf.Hamna namna maalim apewe tu ushindi.
 
Nami nafikiri Maalim Seif ilimbidi ajibie hizi kesi maana kiukweli zimeleta mitazamo tofauti so kwakuwa yeye anazo zile copy za matokeo ambazo alikusanya atuambie kuwa ZEC ni waongo na haweke bayana juu ya tuhuma za kuzidi wapiga kura

Kwahiyo idadi ilizidi vituo vyote? au kadhaa? kama ni kadhaa? kwanini uchaguzi ufutwe nchi nzima?

Kuna kifungu kinachosema watu wakivua mashati uchaguzi unafutwa? sio kwamba hao jamaa wanakuwa disqualified na wanafikishwa mahakamani? Mbona Sugu alimdunda mtu ngumi bungeni na kile kikao cha bunge hakikufutwa?
 
Maalim Seif anazo nakala za matokeo. Je; ni utaratibu mgombea mmoja wapo kupewa nakala za matokeo? Ilikuwaje yeye akawa nazo wakati ana wawakilishi? Hii haithibitishi kuwa makamishena wa ZEC waligeuka kuwa wawakilishi wa vyama vyao. Pale idadi ya kura zinazidi wapiga kura waliojiandikisha katika daftari la wpiga kura, ZEC ifanye nini aeleze Maalim Seif. Pale kura zimefutwa futwa, inajulikana kuwa kura hizo zitakuwa zimeharibika na hapewi mgomba yeyote, je; hii ikionekana kupunguza kura zake itakuwaje


sikiliza hii utapata majibu yote


 
Last edited by a moderator:
Maalim Seif anazo nakala za matokeo. Je; ni utaratibu mgombea mmoja wapo kupewa nakala za matokeo? Ilikuwaje yeye akawa nazo wakati ana wawakilishi? Hii haithibitishi kuwa makamishena wa ZEC waligeuka kuwa wawakilishi wa vyama vyao. Pale idadi ya kura zinazidi wapiga kura waliojiandikisha katika daftari la wpiga kura, ZEC ifanye nini aeleze Maalim Seif. Pale kura zimefutwa futwa, inajulikana kuwa kura hizo zitakuwa zimeharibika na hapewi mgomba yeyote, je; hii ikionekana kupunguza kura zake itakuwaje

bantulile ngoja nikujibu hoja kwa hoja.
1/Kila chama kiliweka wakala, na kila wakala anapewa nakala ya matokeo ya kituo alichokisimamia. CUF walikusanya nakala ya Fomu zote kutoka kituo kwa kituo na wakajulimsha na wakatoa matokeo ambayo yanaonyesha wameshinda. CCM pia wamekusanya nakala hizo na wamejumlisha matokeo, lakini wamekwepa kuyatoa matokeo yao. ADC nao wamekufanya na wanakiri aliyeshinda ni Maalim Seif wa CUF.

2/Wajumbe wa ZEC wengi wameteuliwa na vyama vya CCM na CUF, na hilo ni agizo la kisheria, hivyo kimantiki ni mawakala wa vyama vyao. Ajabu ni nini katika hilo?
Wewe na Jesha mlitakaje?
Katika hilo kuna kosa gani kisheria au kikanuni? Kuwa wakala wa Chama maana yake ni nini?

3/ZEC wanasema baadhi ya Fomu zilikuwa zimefutwafutwa na kuandikwa, ni vituo au majimbo yapi hasa?
Sheria inasemaje hasa katika hilo?

4/ZEC wanasema wapiga kura walizidi idadi katika baadhi ya vituo.
Mpaka sasa ZEC wameshindwa kusema ni vituo vipi, vingapi vilikuwa na hilo tatizo.
Matokeo yote yaliyotolewa na CUF hayaonyeshi kabisa kama kuna hizo kasoro.
 
Last edited by a moderator:
STDVII naona na wewe unaleta hoja za Kijinga kabisa hapa. Ngoja nitoe ufafanuzi kidogo.

1/ZEC imetoa sababu 8 za kufuta uchaguzi, sababu zote hizo ni kijinga kabisa, zote zimetolewa majibu na Seif na pia watu mbalimbali.
Kwa kifupi hizo sababu hazina mashiko kabisa. Kwa mfano.

(A)Wajumbe wa ZEC kuvua mashati na kupigana. Hii sio sababu ya kuweza kufuta uchaguzi. Ugomvi wa wajumbe(kama kweli ulikuwepo) kamwe hauwezi kuwa ni kasoro katika uchaguzi.

(B)Mtu kujitangazia ushindi kabla ya matokeo rasmi.(Hii sio sababu ya kuufanya uchaguzi uwe na kasoro, hizo ni siasa tu)

(C)Fujo kutokea katika vituo vya kupigia kura.(Vituo vyote vilikuwa na ulinzi mkubwa sana wa askari wenye silaha, hakuna matukio ya Fujo yaliyoripotiwa na Polisi, vyombo vya habari nk. Sasa ZEC wamepata wapi hizo taarifa?).

(D)Kuwepo kwa watu waliopiga kura ambao majina yao hayakuwemo kwenye Daftari.
(Hili ndio haliwezekani kabisa, ZEC ndio wasimamizi wa kupiga kura, sasa nani aliwaruhusu hao watu wapige kura, kwanini mawakala wasilalamike katika hilo?)

(E)Idadi ya watu waliopiga kura kuzidi idadi ya waliojiandikisha.
(Huu ndio uwongo wa wazi kabisa, ZEC imeambiwa itoe matokeo yote ya vituo ili tukione hicho lakini mpaka sasa wameshindwa, CUF wametoa matokeo yote waliyokusanya kituo kwa kituo, jimbo kwa jimbo, na hiyo kasoro haipo kabisa, mpaka sasa hakuna kituo chochote ambacho vote turnout ilifika zaidi ya Asilimia 90, sasa tume wamepata wapi hayo?)

2/Hakuna kikao chochote cha ZEC kilikaa na kuamua kuufuta uchaguzi wa Zanzibar. Ni mwenyekiti mwenyewe wa ZEC aliibuka na kuufuta uchaguzi, kanuni na sheria za ZEC zinataka maamuzi yoyote ni lazima yaafikiwe kwanza na wajumbe wa ZEC wasiopungua 5 kati ya Wajumbe6. Nani kamtuma Jesha kuufuta uchaguzi wa Zanzibar?

3/ZEC imeundwa kisheria na imepewa mamlaka yake kisheria. Hakuna sheria inayoipa ZEC mamlaka ya kuufuta uchaguzi wote wa Zanzibar kwa kigezo cha kasoro, Fujo nk.
Mpaka sasa ZEC imeshindwa kusema ni sheria gani wameitumia ili kufuta uchaguzi wa Zanzibar.


Ujinga naukubali ZEC imetoa sababu 9 siyo 8

(1) wajumbe makamishna kuzichapa ngumi hii inaondoa uwezekano wa kikao busara ya mwenyekiti imetumika

(9)idadi ya waliopiga kura kwenye vituo hasa Pemba ni kubwa/wengi kuliko waliojiandikisha

Kama ni kweli ZEC inahaki ya kufuta uchaguzi pamoja na matokeo yake.

Hoja ije hapo sababu alizotoa mwenyekiti ni za kweli? Siyo kuleta blabla

NB; ZEC ndiyo inaandikisha ina orodha ya majina ya wapiga kura haihitaji degree ktk hilo
 
Last edited by a moderator:
Hapo ambapo Rais wa zanzibar ni miongoni mwa wajumbe wa baraza la mawaziri ndo panapo waumiza kichwa hapo ndo penye utata ndio maana jamaa hawataki kukabidhi nchi.
 
Back
Top Bottom