Kirikou Wa Kwanza
JF-Expert Member
- May 24, 2013
- 3,564
- 1,992
Ni ngumu sana kudhani kwamba Uchaguzi hautarudiwa kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar, Tume hii ina wawakilishi toka CCM na CUF.
Tume ndiyo inatangaza matokeo toka majimbo lalini Tume ndiyo inafanya kazi ya kuandikisha wapiga Kura kabla ya Uchaguzi, hii ina maana gani? Tume ina idadi ya wapiga Kura wote kwa idadi ya Majimbo na vituo vya kupiga Kura.
Endapo itatokea tofauti ya wapiga Kura hasa kama idadi yao itaongezeka Tume itafuta Uchaguzi hiyo ni Haki yake.
Tume imetoa sababu 9 kwa nini imefuta Uchaguzi
1. Makamishna walivua mashati ili kutwangana makonde
9. Idadi ya wapiga Kura ilikua kubwa kuliko waliojiandikisha.
Ktk hali hiyo kinachotakiwa ni tafsiri tu ya Katiba kuhusu majukumu ya ZEC inapotokea hali kama hiyo.
Sababu nyingine vituo vingi vya kupigia kura mawakala walikuwa wa CUF/UKAWA, mawakala wa vyama vingine walinyang'anywa kadi zao za utambulisho hivyo walishindwa kushiriki mchakato wa kusimamia upigaji kura mpaka pale walipopata vitambulisho vyao.