Maalim Seif: Haturudii Uchaguzi

Maalim Seif: Haturudii Uchaguzi

Zec haijataja majimbo yaliyoengezeka wapiga kura,na hata kama itataja basi ni kwa jimbo kurejea uchaguzi sio kufuta uchaguzi.
Ujinga naukubali ZEC imetoa sababu 9 siyo 8

(1) wajumbe makamishna kuzichapa ngumi hii inaondoa uwezekano wa kikao busara ya mwenyekiti imetumika

(9)idadi ya waliopiga kura kwenye vituo hasa Pemba ni kubwa/wengi kuliko waliojiandikisha

Kama ni kweli ZEC inahaki ya kufuta uchaguzi pamoja na matokeo yake.

Hoja ije hapo sababu alizotoa mwenyekiti ni za kweli? Siyo kuleta blabla

NB; ZEC ndiyo inaandikisha ina orodha ya majina ya wapiga kura haihitaji degree ktk hilo
 
Hapo ambapo Rais wa zanzibar ni miongoni mwa wajumbe wa baraza la mawaziri ndo panapo waumiza kichwa hapo ndo penye utata ndio maana jamaa hawataki kukabidhi nchi.

Tume ya Warioba iliyaona sana haya matatizo na ika-propose ufumbuzi. Sijui ni kwa nini CCM walishupaza shingo vile na athari zake ndio kama hivyo zinataka kuanza kuonekana. For sure, sioni ni kwa vipi Maalim Seif atavuka bahari kuja bara eti kama member wa baraza la mawaziri. Sioni uwezekano huo kamwe!
 
Rais wa Zanzibar aondolewe kwenye baraza la Muungano kikatiba.Rais atateua baraza lake.hatutaki masumbwi ktk baraza kama ilivyokuwa NEC
 
Hapa patamu nami nilijua tu CCM hawataki maalim ashike zanzibar kuna sehemu KATIBA inamtaka Rais wa jamhuri kushauriana na Rais wa zanzibar hasa katika baadhi ya teuzi na maamzi flan flan, na iyo kuingia baraza la mawaziri😀😀

Tafsiri nyepesi ni kuwa maalim kuwa Rais ni kuwapa UKAWA watch dog ndani ya serikali. Patamu hapa. Lazima maalim awe Rais mwaka huu. Picha inaanza Bruce Lee anakufa. 😀😀:beer:
 
Ni ngumu sana kudhani kwamba Uchaguzi hautarudiwa kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar, Tume hii ina wawakilishi toka CCM na CUF.

Tume ndiyo inatangaza matokeo toka majimbo lalini Tume ndiyo inafanya kazi ya kuandikisha wapiga Kura kabla ya Uchaguzi, hii ina maana gani? Tume ina idadi ya wapiga Kura wote kwa idadi ya Majimbo na vituo vya kupiga Kura.

Endapo itatokea tofauti ya wapiga Kura hasa kama idadi yao itaongezeka Tume itafuta Uchaguzi hiyo ni Haki yake.

Tume imetoa sababu 9 kwa nini imefuta Uchaguzi

1. Makamishna walivua mashati ili kutwangana makonde
9. Idadi ya wapiga Kura ilikua kubwa kuliko waliojiandikisha.

Ktk hali hiyo kinachotakiwa ni tafsiri tu ya Katiba kuhusu majukumu ya ZEC inapotokea hali kama hiyo.

bado mkuu hujaelewa alietoa tamko nilam2 m1 sio tume nzima ndo maana adi sasa tume haina msimamo
 
Maalim Seif anazo nakala za matokeo. Je; ni utaratibu mgombea mmoja wapo kupewa nakala za matokeo? Ilikuwaje yeye akawa nazo wakati ana wawakilishi? Hii haithibitishi kuwa makamishena wa ZEC waligeuka kuwa wawakilishi wa vyama vyao. Pale idadi ya kura zinazidi wapiga kura waliojiandikisha katika daftari la wpiga kura, ZEC ifanye nini aeleze Maalim Seif. Pale kura zimefutwa futwa, inajulikana kuwa kura hizo zitakuwa zimeharibika na hapewi mgomba yeyote, je; hii ikionekana kupunguza kura zake itakuwaje

Mambo hayaendi kama baadhi yenu mnavyofikiri. Seiff wala cuf hawawezi kuwa wajinga wa kuweka ushahidi wao jf. Hizo ni akili za magengeni na vijiwe vya gahwa. Ushahidi kama huo hutolewa mahakamani tu ziwe za nchini kwenu au za kimataifa na ni pale kesi inapofunguliwa na ushahidi kuhitajika. Mahakama nazo hudai ushahidi wa hivyo hivyo kwa upande wa pili na kuoanisha kuanzia uhalali wa makaratasi kama yamechezewa au vinginevyo. Wanaweza kuhitaji kupelekewa hata daftari la wapiga kura kuona walioandikishwa na uhalali wao. Hizo taarifa hubakia kuwa za kimahakama na hazitolewi kwa wasiohusika. Mahakama ina vitengo vingi vya kuthibitisha miandiko, urekebishwaji na hata uhalali wa saini na sauti hivyo maalim hawezi kuweka huo ushahidi kwa ajili ya hadhara akifanya hivyo ataipa serikali majibu kirahisi na huo ushahidi haufai tena mahakamani.Cuf kama cuf na hata ukawa wanao wanasheria wengi sana na hizo taratibu wanazielewa fika.
Hofu yangu ilipo ni kuwa serikali na chama chao cha ccm watalazimisha uchaguzi urudiwe na cuf haitaweza kushinda. Endapo cuf wakisusia uchaguzi vyama vingine vya upinzani vitashiriki na serikali inaweza kuwapa ruzuku kubwa. Kwa vyama hivi vidogo vidogo vitajiongezea majimbo na madiwani na kwa kura za wagombea uraisi wa vyama vyao watajiongezea ruzuku ya kila mwezi. Kwao hawatagomea uchaguzi na ndipo ccm itashinda kwa asili mia 90. Hatari ya maamuzi kama haya ni kuiweka Zanzibar kwenye machafuko makubwa. Kitendo cha m/kiti kufuta uchaguzi wa nchi nzima hakina busara wala hekima kwani jimbo lililozidisha wapiga kura hufutiwa matokeo na sio kufuta uchaguzi wote. Kama walikuwepo wajumbe wa kamati waliopigana wangewajibishwa wao kama wao na sio kuwajibisha wapiga kura. Jecha aelewe angeweza kuteuliwa yeye tu peke yake kama m/kiti lakini katiba iliona umuhimu wa kumwekea makamishna. Uamuzi wowote atakaouchukua ni lazima ukubaliwe na makamishna wenzie. Asijisahau kuwa nae ni kamishna tu ila ni m/kiti wao hivyo uamuzi wake peke yake hauna uhalali popote. VINGINEVYO KUENDELEA KUIMBA DEMOKRASIA NA UTAWALA WA SHERIA HAINA MAANA. HAYO NI MAWAZO YANGU. SIO LAZIMA YAWE NA UKWELI WA KISHERIA.
 
bado mkuu hujaelewa alietoa tamko nilam2 m1 sio tume nzima ndo maana adi sasa tume haina msimamo

Baada ya tamko la mwenyekiti wa tume kikao kilikaa na kuridhia Uchaguzi kurudiwa
 
Hapati urais wa zanzibar hata afanye nini. Zanzibar itabaki mikononi mwa ccm, zanzibar itabaki mikononi mwa tanganyika.Na wakileta za kuleta tunatembeza kipigo. Safari hii hata umakamu haupati. Tunakula samaki mzima hapati hata mifupa.
 
Sijalisoma popote pale. Wajumbe wabkamati ya uchaguzi au kikao cha nini?

Makamishna wa ZEC walikutana na kuamua kuridhia, hakuna namna uchaguzi utarudiwa zitapigwa kelele mwisho zitaisha anayeitisha uchaguzi ni ZEC siyo CCM wala CUF
 
Wakiambiwa KATIBA iliyopo jangaa Lumumba wanakuja juu!




Akifafanua, Fatma alisema kuwapo kwa nafasi ya moja kwa moja ya Rais wa Zanzibar kwenye Baraza la Mawaziri kunaibua mgongano inapotokea mshindi wa upande mmoja akiwa ni wa kutoka chama kingine na hiyo ni sababu mojawapo wanayoamini kuwa imechangia kufutwa kwa uchaguzi na pia kukwaza ukuaji wa demokrasia visiwani humo.

Alisema ni dhahiri hali huwa ngumu kwa baraza la mawaziri linaloundwa na watu wa itikadi ya chama kimoja kuchanganyika na mwingine mwenye itikadi tofauti, hasa katika mazingira ya kuwa na usiri katika baadhi ya mambo na kwamba, hilo huchangia kusuasua kwa maendeleo ya kidemokrasia visiwani Zanzibar.





Baraza la Mawaziri na Serikali

Baraza la Mawaziri Sheria ya 1984 Na.15 ibara 9 Sheria Na.4 ya 1992 ib?Sheria Na.34 ya 1994 ibara 12

54.-(1) Kutakuwa na Baraza la Mawaziri ambalo wajumbe wake watakuwa ni Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Rais wa
Zanzibar
na Mawaziri wote.
 
Yaani CUF wakilegeza msimamo na kulainika ati uchaguzi urudiwe, itakuwa imekula kwao, lazima watashindwa.
Uchaguzi huu ulikuwa mgumu sana kwa CCM kiasi kwamba nguvu kubwa ilitumika Bara na hivyo kutoa nafasi kwa CUF kule Zanzibar. Uchaguzi wa Zanzibar ukirudiwa CCM watapata ushindi hata ule wa bao la mkono maana nguvu zao zote zitapelekwa Zanzibar.

Vv
 
Nami nafikiri Maalim Seif ilimbidi ajibie hizi kesi maana kiukweli zimeleta mitazamo tofauti so kwakuwa yeye anazo zile copy za matokeo ambazo alikusanya atuambie kuwa ZEC ni waongo na haweke bayana juu ya tuhuma za kuzidi wapiga kura

Kura zilizidi ngapi na zilionekana lini wakati walikuwa hawajamaliza kuhesabu kura!!??? acha upotoshaji! mwenye kulalamika ni ZEC au Vyama?? Hapa bara umeyaona yaliyotangazwa mpaka mwisho! data zinasemaje??
 
Hapati urais wa zanzibar hata afanye nini. Zanzibar itabaki mikononi mwa ccm, zanzibar itabaki mikononi mwa tanganyika.Na wakileta za kuleta tunatembeza kipigo. Safari hii hata umakamu haupati. Tunakula samaki mzima hapati hata mifupa.

Punguza munkari, Zanzibar kuna watu, tena wana haki sawa na wewe.

Vv
 
Kutokana na katiba ya sasa kuhusu vipengele vya uchaguzi, Tume,ZEC, hata kama itakamilika jopo zima, hawana mamlaka ya kufuta MATOKEO ya uchaguzi wote. Kwa sababu, in theory, kama process inafatwa kisheria na tume wanawajibika ipasavyo, haifikii hatua ya kufikia mpaka kujua matokeo, ndio ujuwe kama uchaguzi una kasoro. Kwa mfano,

Sababu moja waloitowa ni idadi ya kura zilopigwa ni nyingi kuliko idadi ya walojiandikisha katika daftari la wapiga kura huko Pemba. Tatizo hili lilikuwa litambulike mapema kabla kura HAZIJACHAMBULIWA. Nina maana ya kusema kwamba process ya kwanza ni kuhisabu idadi ya kura zote kwenye kila sanduku against waliopiga kura katika chumba kile kabla hata watu hawajapoteza muda wa kuzichambuwa na ku allocate kila mgombea kura zake. Ikiwa kwenye register inaonesha wapiga kura kwenye chumba hichi ni 350 ndio walohudhuria, na kwwnye sanduku zimo 400, kuna haja gani ya kuhesabu kura hizi. Inaonesha tatizo lipo na hapo hapo taarifa inapelekwa tume na wanachukuwa uamuzi kwa sababu ya kasoro hizi.

The possible scenario ya kuahirisha uchaguzi nchi nzima ni kuwa kasoro kama hii ama nyengine possible kuchelewa vifaa ama security concerns ama kifo cha mgombea itokezee vituo vyote vya kupigia kura katika majimbo yote nchi nzima. Hakuna possible scenario yoyote ya kuweza kusababisha uchaguzi ufutwe, labda kwa kupenda JECHA tu.

Kama walivyotowa mfano Awadh na Karume, kwa hiyo ukifanyika tena akatokea mgombea wa TADEA akasema kashinda, uchaguzi ufutwe? Baada ya hapo ADC watasema wameshinda, basi Shein ataendelea kuwa raisi maisha.

Kasoro zote zilobakia ni makosa ya ZEC wenyewe, kwa sababu masanduku ya kura ni ya kwao na yanalindwa na wao wenyewe wakishirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama. Sasa kama kura zimezidi ndani ya sanduku wanamlaumu nani? Hizo kura zimetiwa saa ngapi na kama wakala wa CCM lets say hayupo, jee ZEC na polisi walikuwa wapi kwenye chumba cha kupigia kura. Jecha awajibike yeye kwanza kabla ya kufanyika lolote. Huu ni zaidi ya ufisadi.

Kwa waliosoma hesabu ni sawa na kusema kuku kutoa maziwa. Probability ya kufutwa matokeo ya uchaguzi nchi nzima is zero.
 
Ni ngumu sana kudhani kwamba Uchaguzi hautarudiwa kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar, Tume hii ina wawakilishi toka CCM na CUF.

Tume ndiyo inatangaza matokeo toka majimbo lalini Tume ndiyo inafanya kazi ya kuandikisha wapiga Kura kabla ya Uchaguzi, hii ina maana gani? Tume ina idadi ya wapiga Kura wote kwa idadi ya Majimbo na vituo vya kupiga Kura.

Endapo itatokea tofauti ya wapiga Kura hasa kama idadi yao itaongezeka Tume itafuta Uchaguzi hiyo ni Haki yake.

Tume imetoa sababu 9 kwa nini imefuta Uchaguzi

1. Makamishna walivua mashati ili kutwangana makonde
9. Idadi ya wapiga Kura ilikua kubwa kuliko waliojiandikisha.

Ktk hali hiyo kinachotakiwa ni tafsiri tu ya Katiba kuhusu majukumu ya ZEC inapotokea hali kama hiyo.



Napenda kutoa nasaha hapo red.
Huyu mwenyekiti wa ZEC ni bora angejifunza kutoka kwa marefarii wa mapambano la Boxing.
Kama makamisha wa ZEC wamechapana makonde basi ni bora angemtangaza bondia aliemshushia makonde ya nguvu mwenzake kuwa ni mshindi! Haiwezekani kufuta pambano lote la boxing. Akifuta pambano hata watazamaji sisi tuliolipa kiingilio basi tutadai chetu. Na kwa maana hio basi ni bora tukaanza kumchapa makonde huyo Alhaji Jecha kwanza.
 
Kama CUF ina uhakika imeshinda, maana yake sera zake zinakubalika na wananchi wa Zanzibar. Huu ndiyo ukweli wa mambo. Ikiwa hivyo ndivyo, hata uchaguzi ukirudiwa mara tano CUF watashinda tu. Kuna sababu gani sasa kkataa kurdia uchaguzi? Hofu inatoka wapi?
Ujinga naukubali ZEC imetoa sababu 9 siyo 8

(1) wajumbe makamishna kuzichapa ngumi hii inaondoa uwezekano wa kikao busara ya mwenyekiti imetumika

(9)idadi ya waliopiga kura kwenye vituo hasa Pemba ni kubwa/wengi kuliko waliojiandikisha

Kama ni kweli ZEC inahaki ya kufuta uchaguzi pamoja na matokeo yake.

Hoja ije hapo sababu alizotoa mwenyekiti ni za kweli? Siyo kuleta blabla

NB; ZEC ndiyo inaandikisha ina orodha ya majina ya wapiga kura haihitaji degree ktk hilo
 
Back
Top Bottom