Maalim Seif, Hamad Rashid uso kwa uso leo

Maalim Seif, Hamad Rashid uso kwa uso leo

Mkuu (sijui na mimi nitumie Maalim kama Jamaa mmoja hapo juu?) Julius Mtatiro safi sana kwa ufafanuzi huu mujarabu. Viongozi kama ninyi ndio mnatakiwa katika wakati huu wa .com. Unatoa taarifa muafaka kwa wakati muafaka. Hongera.

Ila sasa inaonekana Kamati ya Utendaji ina nguvu nyiiiingi na inaongozwa na Katibu Mkuu. Kwa jinsi ulivyoelezea inaonekana kam Mwenyekiti ni mshauri tu katika masuala ya utendaji kichama? Hii haina maana kwamba Katibu Mkuu ana nguvu zaidi kuliko Mwenyekiti?

Mbona naanza kuhisi kuwa hiyo katiba iliandaliwa kwa kuangalia nani ni Katibu! Ukiacha baadhi ya vyama vya Kikomunisti vyama vingine vya siasa duniani huwa Mwenyekiti ndiye Mkuu wa Chama lakini hapo CUF inakuwa kama kinyume!

Kumbe ndio maana Maalim yeye na Ukatibu tu hataki uenyekiti kwa kuwa mwenyekiti hana meno!!

Pia hili suala la kofia mbili yaani moja ni Katibu Mtendaji wa chama na nyingine Makamo wa Rais hamuoni kama linaleta shida kwa kuwa kuna matamko anatoa tunashindwa kuelewa kama ni matamko ya Chama ama ya SUK?

Ahsante.
Kimbunga nilivyomwelewa Mtatiro ni kuwa Kamati ya utendaji inayoongozwa na katibu mkuu haina mamlaka ya kufukuza mwanachama isipokuwa kutoa mapendekezo na kuyawasilisha kwenye kikao cha Baraza kuu kinachoongozwa na Mwenyekiti wa taifa.
 
kama hamuelewi hiyo ni mbinu ya kuwafanya wajitangaze zaidi kwa umma...wanataka wapate coverage kubwa kwenye media ili watu wazidi kuifahamu na kufatilia habari za CUF. kwa hiyo hapo hakuna kufukuzana wala nini...just popularity strategy!
It is very bad strategy.
 
Tufikirie na gharama za uchaguzi wa mbunge Mwengine kama akitimuliwa ...inamaana tutakuwa na majimbo 2 ya uchaguzi
Wa TZ akili mkichwa....:A S embarassed:
 
Tumemaliza kikao cha kamati ya uteandaji ya taifa salama, updates mzipate kwenye vyombo vya habari leo kwani tulijulisha media saa 9 jioni ya leo.

Kikao cha baraza kuu la uongozi la taifa kimeitishwa, ni kikao cha dharura - kitafanyika tarehe 04 januari 2011 siku ya jumatano katika ukumbi wa mazsons zanzibar.

Ni kikao maalum cha dharura kitakachomaliza sintofahamu hizi ambazo zinaendelea ndani yama na kukuzwa sana na vyombo vya habari.

Siku zote nasisitiza hapa, CUF tuna wabunge 36, kati ya wabunge hao mmoja amehama mstari, chama kitatumia vikao kimaliza hali hiyo na chama kitabakia imara.

Kama nilivyosema awali, kamati ya utendaji ya taifa haina maamuzi juu ya HR na wenzie 13. Ni baraza kuu peke yake ndilo lina maamuzi juu yao.

Narudia tena kusisitiza kuwa hakuna mgogoro ndani ya CUF wala hakuna ugomvi - kuna watu wamehama kwenye mstari na watarudishwa mstarini kwa mujibu wa katiba.

Kinachoikuta CUF leo kinaweza kukuta chama chochote cha siasa.

Kamati ya utendaji ya taifa imemaliza kazi yake, sasa ni kazi ya baraza kuu kukaa, kujua nini kimejiri, kupewa ushahidi na kisa wahusika watasikilizwa na baraza kuu na kisha litatoa maamuzi yanayofaa kwa maslahi ya chama.

Ikumbukwe baraza kuu linaundwa na wajumbe kikanda, kuna wanaotoka kanda ya ziwa, kanda ya kati, nyanda za juu kusini, kanda ya kusini, kanda ya kaskazini, kanda mashariki, kanda ya pemba na kanda ya unguja.

Nataka kurudia tena, masuala haya ya vyama, hata kama magazeti yataandika kwa interest zao kiasi gani, hata kama wadau kadhaa watasema nini, ukweli unabakia kuwa masuala ya kisiasa huamuliwa na au kumalizwa na vikao vya chama. Na CUF itayamaliza vikaoni.
 
Mkuu (sijui na mimi nitumie Maalim kama Jamaa mmoja hapo juu?) Julius Mtatiro safi sana kwa ufafanuzi huu mujarabu. Viongozi kama ninyi ndio mnatakiwa katika wakati huu wa .com. Unatoa taarifa muafaka kwa wakati muafaka. Hongera.

Ila sasa inaonekana Kamati ya Utendaji ina nguvu nyiiiingi na inaongozwa na Katibu Mkuu. Kwa jinsi ulivyoelezea inaonekana kam Mwenyekiti ni mshauri tu katika masuala ya utendaji kichama? Hii haina maana kwamba Katibu Mkuu ana nguvu zaidi kuliko Mwenyekiti?

Mbona naanza kuhisi kuwa hiyo katiba iliandaliwa kwa kuangalia nani ni Katibu! Ukiacha baadhi ya vyama vya Kikomunisti vyama vingine vya siasa duniani huwa Mwenyekiti ndiye Mkuu wa Chama lakini hapo CUF inakuwa kama kinyume!

Kumbe ndio maana Maalim yeye na Ukatibu tu hataki uenyekiti kwa kuwa mwenyekiti hana meno!!

Pia hili suala la kofia mbili yaani moja ni Katibu Mtendaji wa chama na nyingine Makamo wa Rais hamuoni kama linaleta shida kwa kuwa kuna matamko anatoa tunashindwa kuelewa kama ni matamko ya Chama ama ya SUK?

Ahsante.

mzee upo njema ktk hoja ulizo toa
 
Tumemaliza kikao cha kamati ya uteandaji ya taifa salama, updates mzipate kwenye vyombo vya habari leo kwani tulijulisha media saa 9 jioni ya leo.

Kikao cha baraza kuu la uongozi la taifa kimeitishwa, ni kikao cha dharura - kitafanyika tarehe 04 januari 2011 siku ya jumatano katika ukumbi wa mazsons zanzibar.

Ni kikao maalum cha dharura kitakachomaliza sintofahamu hizi ambazo zinaendelea ndani yama na kukuzwa sana na vyombo vya habari.

Siku zote nasisitiza hapa, CUF tuna wabunge 36, kati ya wabunge hao mmoja amehama mstari, chama kitatumia vikao kimaliza hali hiyo na chama kitabakia imara.

Kama nilivyosema awali, kamati ya utendaji ya taifa haina maamuzi juu ya HR na wenzie 13. Ni baraza kuu peke yake ndilo lina maamuzi juu yao.

Narudia tena kusisitiza kuwa hakuna mgogoro ndani ya CUF wala hakuna ugomvi - kuna watu wamehama kwenye mstari na watarudishwa mstarini kwa mujibu wa katiba.

Kinachoikuta CUF leo kinaweza kukuta chama chochote cha siasa.

Kamati ya utendaji ya taifa imemaliza kazi yake, sasa ni kazi ya baraza kuu kukaa, kujua nini kimejiri, kupewa ushahidi na kisa wahusika watasikilizwa na baraza kuu na kisha litatoa maamuzi yanayofaa kwa maslahi ya chama.

Ikumbukwe baraza kuu linaundwa na wajumbe kikanda, kuna wanaotoka kanda ya ziwa, kanda ya kati, nyanda za juu kusini, kanda ya kusini, kanda ya kaskazini, kanda mashariki, kanda ya pemba na kanda ya unguja.

Nataka kurudia tena, masuala haya ya vyama, hata kama magazeti yataandika kwa interest zao kiasi gani, hata kama wadau kadhaa watasema nini, ukweli unabakia kuwa masuala ya kisiasa huamuliwa na au kumalizwa na vikao vya chama. Na CUF itayamaliza vikaoni.
Endelea na propaganda Mtatiro lakini kimsingi unajua maamuzi yalishafikiwa na wale jamaa walipochati kwa email. Ila tatizo kubwa unalokwepa kulisema ni hiyo ndoa yenu ya kihuni na ccm ambayo imeenda hata kinyume na katiba kwa maslahi ya watu wachache. Hiyo dhambi ya usaliti mliyoionesha kwa wananchi imeanza kuwageukia. CUF mmebadilika kutoka kupigania serikali mpaka kushiriki kuendesha mojawapo ya serikali mbili!
 
Huu upuuzi tu, hizo ni garbage tupu sijui vikao vya maadili. Watu wanapohoji uadilifu ama kutaka uongozi ndo mnawaitia upuuzi wa vikao vya maadili.

rudi shule maana hata uelewi anachosema mtatiro. Pumba peleka kwenu
 
Hapana mkuu wangu Profesa hana sababu ya kugombea wenyekiti.. nawapa darasa tu la siasa unajua tena - Kigamboni shule kubwa wanaihitaji wote sichagui mhindi, msukuma wala mkerewe..

Ha ha
Mkuu si unaona profesa wanzeko wanavyokimbizwa pale Tz, si bara wala visiwani, kila chama pale kina maprofesa lakini wanapelekwa puta na ma form six.

Heri ya mwaka mpya,
Nafikiri ni bora kuwaelimisha wale kaka zangu wa Ukarani pale, jinsi bora ya kuzalisha viazi bora na machungwa bora ili wajikwamue na wakifika ktk maisha ya kati, BY DEFAULT watachagua kiongozi bora.

Lakini kujaribu kuelimisha hawa viongozi wa vyama vyote vya siasa ni kupoteza mda na resources zako. Viongozi hawa wanafahamu bayana nini cha kufanya, lakini hawafanyi kwa sababu ya nafasi zao na hali ya watanzania ilivyo ni faida kubwa kwao na wanapenda endelee kuwa hivyo.
 
Endelea na propaganda Mtatiro lakini kimsingi unajua maamuzi yalishafikiwa na wale jamaa walipochati kwa email. Ila tatizo kubwa unalokwepa kulisema ni hiyo ndoa yenu ya kihuni na ccm ambayo imeenda hata kinyume na katiba kwa maslahi ya watu wachache. Hiyo dhambi ya usaliti mliyoionesha kwa wananchi imeanza kuwageukia. CUF mmebadilika kutoka kupigania serikali mpaka kushiriki kuendesha mojawapo ya serikali mbili!

rudi shule ndomana mixn kibao huwelewi unachoongea pumba tupu masaburi bana yana tabu. Ndoa unaipenda sana, ? Cameroon tayari amemaliza una wivu kweli bwana wako cameroon, ana kukameroon hutosheki una kwenda kuchokonoa mengine. Watu wamekufa zanzibar wameamua kukaa meza moja natena wananchi walipiga kura zamaoni kutaka mfumo wa pamoja halafu unaleta masaburi hapa umeona cameroon hayalambi masaburi yako kisawasawa.
 
Si angalau hawa wanaitisha vikao kuna mwana CCM anayeweza kuhoji utendaji wa mwenyekiti au katibu mkuu, thubutu.

Kuitisha kikao wakati unamajibu tayari ni uwendawazimu, ni bora asiyeitisha kabisa. Makamba je? Lowasa na bado huko nasikia wanahoji Rais asiwe mwenyekiti wa chama.

Pamoja ni kweli ya kuwa ccm ni wabovu kupindukia lakini bado wana demokrasia kuliko vyama vyote. Demokrasia ni pamoja na kusema wazi wazi ndani ya chama kama vile wanachama wa ccm wanavyosema magamba wajivue, magamba wanagoma wanaita kikao mziki hauendi wanahaarisha, hizo ni dalili za demokrasia.

Lakini kuitisha kikao ukiwa na majibu mkononi na kutimua wanachama ni dalili za udikteta.
 
Tumemaliza kikao cha kamati ya uteandaji ya taifa salama, updates mzipate kwenye vyombo vya habari leo kwani tulijulisha media saa 9 jioni ya leo.

Kikao cha baraza kuu la uongozi la taifa kimeitishwa, ni kikao cha dharura - kitafanyika tarehe 04 januari 2011 siku ya jumatano katika ukumbi wa mazsons zanzibar.

Ni kikao maalum cha dharura kitakachomaliza sintofahamu hizi ambazo zinaendelea ndani yama na kukuzwa sana na vyombo vya habari.

Siku zote nasisitiza hapa, CUF tuna wabunge 36, kati ya wabunge hao mmoja amehama mstari, chama kitatumia vikao kimaliza hali hiyo na chama kitabakia imara.

Kama nilivyosema awali, kamati ya utendaji ya taifa haina maamuzi juu ya HR na wenzie 13. Ni baraza kuu peke yake ndilo lina maamuzi juu yao.

Narudia tena kusisitiza kuwa hakuna mgogoro ndani ya CUF wala hakuna ugomvi - kuna watu wamehama kwenye mstari na watarudishwa mstarini kwa mujibu wa katiba.

Kinachoikuta CUF leo kinaweza kukuta chama chochote cha siasa.

Kamati ya utendaji ya taifa imemaliza kazi yake, sasa ni kazi ya baraza kuu kukaa, kujua nini kimejiri, kupewa ushahidi na kisa wahusika watasikilizwa na baraza kuu na kisha litatoa maamuzi yanayofaa kwa maslahi ya chama.

Ikumbukwe baraza kuu linaundwa na wajumbe kikanda, kuna wanaotoka kanda ya ziwa, kanda ya kati, nyanda za juu kusini, kanda ya kusini, kanda ya kaskazini, kanda mashariki, kanda ya pemba na kanda ya unguja.

Nataka kurudia tena, masuala haya ya vyama, hata kama magazeti yataandika kwa interest zao kiasi gani, hata kama wadau kadhaa watasema nini, ukweli unabakia kuwa masuala ya kisiasa huamuliwa na au kumalizwa na vikao vya chama. Na CUF itayamaliza vikaoni.

Kila la heri lakini madai ya HR yashughulikiwe msije mka-personalize issue
 
Maamuzi ya kubaki ama kutimuliwa ndani ya Chama Cha Wananchi (CUF), Mbunge wa Wawi kupitia chama hicho, Hamad Rashid Mohammed, sasa yamebakia kwa Katibu Mkuu wake, Maalim Seif Sharif Hamad, ambaye leo anaongoza kikao cha Kamati ya Utendaji kumjadili na wenzake 12.

Kikao hicho ambacho wajumbe wake ni wakurugenzi wote wa idara mbalimbali za chama hicho kitafanyika visiwani Zanzibar kwa siku mbili kabla ya kuamua ama kumtimua uanachama ama kumpa onyo kali kwa barua.

Mwenye taarifa zaidi za kikaoni atujuze.
Ukweli umedhihirika sasa jinsi huyu bwana alivyo na uchu na mbinu mbaya za kujitwalia madaraka ,bila kujali madhara gani yanayoweza tokea kwa hila zake,rejea aliposhirikiana na spika Anna makinda ili kupindisha kanuni ya kambi rasmi ya upinzani bungeni.
yote kisa ilikuwa ni kwa sababu yeye alikuwa amepoteza uongozi wa kambi rasmi bungeni kwa kuwa chama chake CUF kilikuwa kimepokwa ushindi na CDM, na hivyo kupoteza sifa ya kuwa kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani bungeni.
Kwa uchu wa kutaka uongozi wa kamati za bunge na kwa hofu ya CCM kutotaka CDM washike kamati nyeti za bunge basi wakashirikiana kuipinga CDM ili tu RH naye aweze kuwa katika kamati mojawapo ya bunge akiwa anawakilisha CCm B na kwa haya yanayotokea leo si kitu cha ajabu kwake yeye maana ni hulka yake.
(UNAWEZA KUNUNUA SAA LAKINI HUWEZI KUNUNUA WAKATI)
Taartfa rasmi ni kwamba kikao kimeisha na wanasubiri kikao cha NEC mnamo tarehe 4 january2012 hii kwa kuwaita watuhumiwa wote kujitetea mbele ya kikao kuhusu tuhuma zinazowakabili
 
rudi shule ndomana mixn kibao huwelewi unachoongea pumba tupu masaburi bana yana tabu. Ndoa unaipenda sana, ? Cameroon tayari amemaliza una wivu kweli bwana wako cameroon, ana kukameroon hutosheki una kwenda kuchokonoa mengine. Watu wamekufa zanzibar wameamua kukaa meza moja natena wananchi walipiga kura zamaoni kutaka mfumo wa pamoja halafu unaleta masaburi hapa umeona cameroon hayalambi masaburi yako kisawasawa.

Hebu tukumbushe mkuu, hao watu unaokiri walikufa, walikufa wakipigania nini? je walichokuwa wakikipigania hao marehemu kimepatikana? khakiiiiiii! ishapatikana? au mmewachuuza wenzenu wamekufa, leo kufa kwao mnageuza ni term of refence ku-justify madhambi na makosa ya sefu na aliowashikia akili, atokee mtu anipinge, nasema waliuawa na sefu! zingatia matokeo ya kura ya maoni kuwa wazanzibar wengi hawakuona vibaya kutawaliwa na ccm hata kama wao ni cuf, ndiyo sefu kuona ajipe ulaji hapo hapo! kuwa makamu wa raisi ambaye hawezi kuteleza matakwa ya cuf serikalini. wewe unajivunia sefu kuua!!! ili hatimaye awe makamu wa rais!!!!!? waliopata vilema wanafaidika nini kwa misimamo ambayo waliaminishwa wanapigania kuikomboa znz mikononi mwa majizi ccm. Leo wezi ccm ndo ma-best wenu, aibuuuuuuuu.
 

picture-4.jpg

Na Saed Kubenea - Imechapwa 28 December 2011

ALIYEJIAPIZA kumng'oa Maalim Seif Shariff Hamad ndani ya Chama cha Wananchi (CUF), sasa kufukuzwa uanachama, imefahamika.

Hamad Rashid Mohammed, mbunge wa Wawi, kisiwani Pemba, ndiye amekuwa akisema anataka kuchukua nafasi ya katibu mkuu wa CUF kwa madai kwamba Maalim Seif ameshindwa uongozi, amedhoofisha chama na hana fikra mpya.

Taarifa kutoka ndani ya chama hicho zinasema, taratibu za kumchukulia hatua Hamad pamoja na wenzake wanaopanga kumuengua Maalim Seif tayari zimeanza.


Hamad na wenzake wanaweza kuwa wameshafukuzwa kwenye chama hicho kabla ya 5 Februari mwaka kesho.


Habari zinasema maandalizi ya vikao vya kumfukuza Hamad na wenzake yalitarajiwa kuanza jana Jumanne (27 Desemba 2011), ambapo Hamad alitakiwa kuhudhuria kikao cha Kamati ya Nidhamu na Maadili.


Hamad na wenzake wanasema tangu Maalim Seif ateuliwe kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), chama kimedhoofika hasa Tanzania Bara ambako kwa sasa CUF "kinaonekana kama tawi la Chama Cha Mapinduzi (CCM)."


Mawasiliano kati ya viongozi wakuu wa chama hicho ambayo yametawanywa jijini Dar es Salaam kwa wiki mbili sasa yanasema, Hamad hawezi kusalimika.


Mawasiliano hayo kati ya Profesa Ibrahim Lipumba, mwenyekiti wa chama hicho taifa, katibu mkuu Maalim Seif, Julius Mtatiro, naibu katibu mkuu Tanzania Bara na Khamisi Khassani, mkurugenzi wa ulinzi na usalama wa CUF, yanaonyesha Hamad atafukuzwa wakati wowote kuanzia sasa na 5 Februari 2012.


Mbali na Hamad wengine wanaotajwa kuchukuliwa hatua au kufukuzwa, ni pamoja na mjumbe wa Baraza Kuu la Uongozi la Taifa, Khassani Doyo na mbunge wa zamani wa Micheweni, Pemba, Shoka Khamisi Juma.


Kwa mujibu wa mawasiliano hayo, tayari Maalim Seif ameagiza kuitwa kwenye Kamati ya Nidhamu ya chama wale anaowaita, "Hamad na genge lake" ili wahojiwe.


Anasema mara baada ya kazi ya kuwahoji kukamilika, kamati ya maadili iwasilishe taarifa yake kwenye kikao cha Kamati ya Utendaji Taifa (KUT) kinachotarajiwa kufanyika wakati wowote mwishoni mwa mwezi huu kwa ajili ya kuchukua hatua.


Akiandika kwa njia ya imeili kwa Profesa Lipumba, 14 Desemba 2011, saa 10:04 asubuhi, Maalim Seif anasema, "Tayari nimeshauriana na Makamu (Makamu mwenyekiti wa CUF, Khamis Machano Alli) na tumeona kuna haja ya jamaa yako (Hamad Rashid) na genge lake kuitwa katika kamati ya nidhamu na maadili kuhojiwa."


Maalim anasema tayari ushahidi wa kutosha umekusanywa na idara ya usalama dhidi ya Hamad, Doyo na Shoka na kwamba sharti Hamad afukuzwe ndani ya chama hicho.


Anasema, "KUT ichukue uamuzi mgumu wa kuwasimamisha uongozi vinara wao na wengine kupewa karipio," anaeleza Maalim katika mawasiliano yake hayo na Profesa Lipumba.


Anasema, "KUT ifikishe taarifa yake katika kikao cha Februari 2012 mbele ya Baraza Kuu Taifa (BKUT) kwa uamuzi." Anasema iwapo itaonekana kuna haja ya kuitishwa kwa mkutano wa dharula wa baraza kuu basi hilo lifanyike haraka iwezekanavyo.


Akisisitiza umuhimu wa Hamad Rashid na wenzake kufukuzwa ndani ya chama hicho, Maalim anasema amekubaliana na ushauri wa Profesa Lipumba wa kuwadhibiti kinidhamu viongozi hao.


Anasema wanachama walio wengi wa chama hicho "wanatudadisi kwa nini hatuchukui hatua?" Anasema, "Sasa ni kumuacha jamaa yako aendelee kufanya kazi aliyopewa na rafiki yake ya kukivuruga chama au chama kimvuruge yeye!"


Hata hivyo, Maalim Seif hajaeleza katika mawasiliano hayo, huyo anayeitwa "rafiki" wa Hamad Rashid aliyempa kazi ya kuivuruga CUF ni nani.


Bali MwanaHALISI limeona nyaraka iliyoandaliwa na idara ya usalama ya chama hicho, pamoja na baadhi ya mawasiliano kati ya Profesa Lipumba, Maalim Seif, Ismail Jussa, Juluis Mtatiro na Khamis Khassani, zikitaja waziri mkuu Mizengo Pinda na mahali pengine mbunge wa Monduli Edward Lowassa, kuwa ndiyo wanaompa nguvu Hamad kuvuruga CUF.


Akionekana kukerwa na tabia hiyo, Maalim anasema, "…leo jamaa yako (Hamad Rashid) kafikia hadi kukodi wahuni na wavuta bangi wanaokadiriwa kufikia 150 kuwahujumu BGs (kikosi cha ulinzi cha CUF)!"


Anasema, "Ikihitajika hata kikao cha dharura cha BKUT kiitishwe. Sisi tunahisi chama ki-act decisively, hasa dhidi ya jamaa yako. Yeye muono wetu tumfukuze kwenye chama na akiamua kwenda mahakamani na mahakama kutoa maamuzi ya kumpendelea yeye, mwache awe mbunge wa mahakama kama ilivyokuwa kwa akina Asha Ngede na Naila Majid Jidawi."


"Ikishajulikana kuwa si mwanachama tena," anasema Maalim, "atakuwa hana mashiko! Muache aende CCM (Chama Cha Mapinduzi) au CHADEMA (Chama cha Demokrasia na Maendeleo) akawe mgombea mwenza!"


Awali akiandika kwa Profesa Lipumba, Maalim Seif anasema, "Nimefurahi kwa mahojiano yako na DW (kituo cha redio na Tv cha Ujerumani cha Deutsche Welle) kuwa ukatibu mkuu hautafutwi kwa mbinu za kimafia.


Anasema tayari Mtatiro ametahadharisha jeshi la polisi mkoani Tabora juu ya Hamad Rashid na wenzake. Maalim anasema Mtatiro ameeleza mkuu wa polisi wa mkoa wa Tabora (RPC) na mkuu wa polisi wa wilaya ya Urambo kuwa wanaokwenda mkoani mwao kufanya mikutano ya hadhara ndio waliosababisha fujo jijini Dar es Salaam.


Barua ya Mtatiro ya 15 Desemba 2011 kwenda kwa mkuu wa polisi wa mkoa wa Tabora, inatuhumu viongozi wawili waandamizi wa chama hicho, Khassani Doyo na Amir Kirungi, kuzunguka wilaya zote nchini bila kuzijulisha mamlaka za chama zilizowekwa kikatiba na kuhamasisha wanachama wake wakihame chama chao.


Hata hivyo, mpango wa Maalim Seif kutaka kufukuza wenzake kwenye chama unapingwa na mjumbe wa baraza hilo, Abubakari Rakesh. Katika mawasiliano yake na Profesa Lipumba, 14 Novemba 2011, Rakesh anasema ni bora Profesa Lipumba kuingilia kati mgogoro kati ya Hamad Rashid na Maalim Seif kuliko kuendekeza utamaduni wa kufukuzana.


Anasema, "…mimi ni kijana wa chama hiki wa muda mrefu…Maalim Seif ni katibu wangu mkuu na Hamad Rashid ni kiongozi wa chama ninayemheshimu sana...nakushauri uingilie kati mgogoro huu ili viongozi hawa waondoe tofauti zao, vinginevyo chama kinaelekea kubaya."


Rakesh alikuwa anamweleza Profesa Lipumba jinsi anavyosakamwa kutokana na mchango wake alioutoa kwenye mkutano wa baraza kuu uliofanyika kwenye hotel ya Lamada, ambapo pamoja na mambo mengine, aliungana na baadhi ya wajumbe waliokuwa wamemtuhumu Maalim Seif kushindwa kutenda kazi zake Tanzania Bara.


Awali Mtatiro akiandika kwa Profesa Lipumba anasema, Doyo na Kirungi wameelekea mkoani Tabora kwa ziara ya kila wilaya; msisitizo wao uko kwenye jimbo la Urambo Magharibi ambako Kirungi aligombea ubunge kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 na 2010.


Anasema, "Wanakwenda huko kufanya kampeni ya wazi ya mikutano ya hadhara na vikao vya ndani kwa lengo kubwa la kutoa notisi ya siku 30 kwa katibu mkuu (Maalim Seif) na mwenyekiti (Profesa Lipumba) wajiuzulu, vinginevyo ngome ya chama yote ihamie CHADEMA."


Mtatiro anasema, "Tuhuma zao ni kuwa mwenyekiti, japokuwa anatokea Tabora, ameshindwa kabisa kukijenga chama na kuwa amepoteza mwelekeo na eti hata katika uchaguzi wa Igunga mwenzie Mbowe (Freeman Mbowe, mwenyekiti wa taifa wa CHADEMA) alipigana wiki kadhaa, lakini mwenyekiti wetu amekimbilia nje ya nchi."


Pili, Mtatiro anasema, Doyo na Kirungi wanadai kuwa katibu mkuu amepoteza mwelekeo na anaua chama Bara, kwa hivyo lazima waondolewe kwa notisi."


Katika mawasiliano mengine, Maalim anamtuhumu mbunge wa Lindi Mjini (CUF), Salum Barwani kutaka kuhujumu ziara yake mkoani Lindi. Anasema Baruani alishawishi baadhi ya watu wasijitokeze kwenye mapokezi yake kwenye uwanja wa ndege wa Lindi.


Anasema, "Nasikia alipingwa vikali na mkutano ulifanikiwa sana. Bila kumtaja, wakati najibu risala yao niliwaeleza kuwa hakuna mgogoro katika chama, isipokuwa kuna mtu na wenziwe wanachochea ionekane kuna mgogoro, na nikaeleza yaliyotokea…."


Iwapo Hamad atafukuzwa CUF, atakuwa mbunge wa pili wa upinzani kuachia ubunge ndani ya kipindi kisichozidi mwaka mmoja tangu kumalizika uchaguzi mkuu.

Mwingine aliyefukuzwa uwanachama, ni mbunge wa Kigoma Kusini kupitia NCCR- Mageuzi, David Kafulila.


Kwa upande wake, Habibu Mnyaa, mbunge wa Mkanyageni, Pemba anamtuhumu Jussa kwa hatua yake ya kutoshiriki vikao vya Maalim Seif kisiwani Pemba.


Akiandika kwa Profesa Lipumba, Mnyaa anasema kikao hicho kilifanyika kwa usalama na amani na wajumbe walitoa michango yao kwa uwazi na kwa nia ya kujenga chama.


Hata hivyo, Mnyaa anasema, pamoja na kwamba makamu mwenyekiti wa chama chake alihudhuria mikutano iliyoitishwa na Maalim Seif, lakini Jussa hakuhudhuria mkutano hata mmoja ingawa alikuwa kisiwani Pemba wakati huo. Hakueleza sababu.


Lakini taarifa zinasema, baadhi ya viongozi wa CUF wanamtuhumu Jussa kumpotosha Maalim Seif kwa maslahi yake binafsi na kukivuruga chama cho kwa maslahi ya CCM.


Wanatoa mfano wa uchaguzi mkuu uliopita, ambapo Jussa alishindwa kukusanya kura kwenye baadhi ya majimbo na kisha kumshinikiza Maalim Seif kukubali matokeo ya urais hata kabla karatasi za kura hazijapatikana.


Mbunge wa Ole, Rajab Mohamed ambaye katika toleo lililopita alitajwa kama mmoja wa wanaomuunga mkono Hamad, amesema "hahusiki kwa namna yoyote na mpango huo."


Ameliambia gazeti hili kwa njia ya simu juzi kuwa hawezi kushiriki na hajapata kushiriki kikao chochote chenye lengo la kuchafua chama. "Mimi ni mbunge mpya jimboni, ninaheshimu viongozi wangu ngazi zote hivyo siwezi kushiriki vikao haramu," alisema.


Idara ya usalama ya CUF ndiyo iliyosambaza taarifa za kuwamo Rajabu kwenye mpango wa kumng'oa Maalim Seif.



 
safi njia inayotumika ni mujibu wa katiba ya chama, hongera cuf mipango yenu ni madhubuti hamkurupuki tu huo ni uwazi sio leo mwenyekiti au katibu anakurupuka na kufukuza wanachama. Utaratibu wa cuf haupo kabisa ukilinganisha na vyama vya upinzani vingine hii ina pelekea baadhi ya vyama vya upinzani kukichukia chama cha cuf. Na mashabiki chipukizi wa vyama pinzani wengi wao hawazidi miaka thelathini hukichukia na kukitolea dhihaka maskini bila ya kujitambua dhihaka zao hazina msingi ni sawa mnajenga huku mnabomoa. Upinzani hawezi kusonga kwa kukichukia chama cha cuf.hapa kuna watu wasio na busara wataanza kuropoka pumba si muda ndipo mtagundua akili za watu zilivyo matope. Na kwamba mawazo yao ndo sahihi wenzao siyo sahihi.
 
Mkuu (sijui na mimi nitumie Maalim kama Jamaa mmoja hapo juu?) Julius Mtatiro safi sana kwa ufafanuzi huu mujarabu. Viongozi kama ninyi ndio mnatakiwa katika wakati huu wa .com. Unatoa taarifa muafaka kwa wakati muafaka. Hongera.

Ila sasa inaonekana Kamati ya Utendaji ina nguvu nyiiiingi na inaongozwa na Katibu Mkuu. Kwa jinsi ulivyoelezea inaonekana kam Mwenyekiti ni mshauri tu katika masuala ya utendaji kichama? Hii haina maana kwamba Katibu Mkuu ana nguvu zaidi kuliko Mwenyekiti?

Mbona naanza kuhisi kuwa hiyo katiba iliandaliwa kwa kuangalia nani ni Katibu! Ukiacha baadhi ya vyama vya Kikomunisti vyama vingine vya siasa duniani huwa Mwenyekiti ndiye Mkuu wa Chama lakini hapo CUF inakuwa kama kinyume!

Kumbe ndio maana Maalim yeye na Ukatibu tu hataki uenyekiti kwa kuwa mwenyekiti hana meno!!

Pia hili suala la kofia mbili yaani moja ni Katibu Mtendaji wa chama na nyingine Makamo wa Rais hamuoni kama linaleta shida kwa kuwa kuna matamko anatoa tunashindwa kuelewa kama ni matamko ya Chama ama ya SUK?

Ahsante.

nimakosa kufikiria katiba ya chama iliundwa kwa manufaa ya maalim sefi, unafahamu wamepita makatibu wangapi kabla ya maalim seif. Mtatiro ame fafanua vizuri na bado mwenyekiti atabaki ndie mwenye mamlaka yote lakini akishauriana na katibu. Ndomana cuf huwezi weka mwenyekiti akawa mwepesi chama tayari kingekuwa kimesambaratika. Leo fanya tafiti zako ndani ya chama utaambiwa mwenyekiti lipumba bado anafaa tena muhimu. Cuf tayari imezitenganisha kazi za katibu na mwenyekiti lakini mwenyekiti ndio final usipate shida mkuu
 
Aloshutumiwa kukiangusha chama ndiye mwenyekiti wa kikao cha maamuzi ya HR... Jamani hivi kweli wewe Mtatiro huoni hata aibu kuja hapa kujaribu kukisafisha chama wakati mnayafanya madudu waziwazi..ndio maana HR alisema hana imani na kikao hicho halafu kweli mtamwajibisha hata kwa kusema ukweli?.
 
Hili nalo halijakaa kiusahihi,

Maalim seif hana maamuzi juu ya hamad rashid, vikao vya chama ndivyo vina maamuzi juu yake.

Hamad rashid na wenzie walihojiwa na kamati ya nidhamu na maadili(kamati hii ipo kikatiba na inafanya kazi kama kamati ndogo chini ya kamati ya ulinzi na usalama ya chama), baada ya hapo kamati ya ulinzi na usalama italeta taarifa yake katika kamati ya utendaji ya taifa.

Kamati ya utendaji ya taifa itapokea taarifa ya kamati ya ulinzi na usalama, itaijadili na kuamua juu ya mapendekezo yaliyoletwa.
Baada ya kuamua KAMATI YA UTENDAJI YA TAIFA itawasilisha taarifa hiyo kwenye kikao cha baraza kuu la uongozi la taifa.

Kikatiba, kamati ya utendaji ya taifa haina mamlaka ya kumpa adhabu kiongozi kama mbunge, mjumbe wa baraza n.k. Hii ina maana kuwa sisi wajumbe wa kamati ya utendaji ya taifa hatuna mamlaka ya kutoa adhabu yoyote kwa HR na wenzie.

Baraza kuu litakapoketi ndio litaamua nini cha kufanya. Kwa mujibu wa katiba, baraza kuu linaweza kumpa onyo la maandishi kiongozi, karipio kali la maandishi, kumsimamisha, kumvua uongozi au kumfukuza uanachama(mamlaka haya yapo kamati ya utendaji taifa).

Jana tumemaliza kikao late night na leo tunaendelea siku ya pili na tunatarajia kupokea taarifa ya kamati ya ulinzi na usalama ambayo inaweza kuhusisha pia masuala ya HR.

In general kikao hiki cha kamati ya utendaji ya taifa siyo cha dharura, ni kikao cha kawaida cha kikatiba kinachokaa kila baada ya miezi miwili. Kikao cha mwisho kilifanyika mwezi oktoba mwishoni na kingine desemba mwishoni.

Vikao vya baraza kuu hukaa kila baada ya miezi minne kutathmini mwenendo wa chama na kukielekeza chama namna ya kujiendesha.

Vikao vya mkutano mkuu hukutana mara moja katika kila miaka mitano.

Nawajuza haya ili kupata weledi zaidi wa masuala yetu ya kivikao na ki-katiba.

Mdogo wangu Mtatiro, kinachoongelewa na watu hapa ni kitu kinachoitwa 'good governance principles' na 'conflict of interest'. Hata ueleze na kufafanua vipi bado haileti picha nzuri kwa MTUHUMIWA (Seif Shariff) kukalia kiti cha mwenyekiti wakati wa kujadili suala la nidhamu linalomhusu MTUHUMU (Hamad Rashid). Hakuna haki hapo hata iweje.
 
Back
Top Bottom