KIM KARDASH
JF-Expert Member
- Sep 21, 2011
- 5,139
- 1,150
Kama taratibu hatuzijui tu we tunauliza,
Kikatiba CUF ina vikao vinne. 1. Kamati ya ulinzi na usalama 2. Kamati ya utendaji ya taifa 3. Baraza kuu la uongozi la taifa na 4. Mkutano mkuu wa taifa.
Katika vikao hivi vinne vya kikatiba, mwenyekiti taifa anaongoza vikao vitatu, anaongoza kamati ya ulinzi na usalama kama mwenyekiti wa kamati, anaongoza baraza kuu la uongozi taifa kama mwenyekiti wa baraza hilo na anaongoza mkutano mkuu wa taifa kama mwenyekiti wa kikao hicho.
Katibu mkuu wa CUF anaongoza kamati ya utendaji ya taifa tu. Hii ni kwa sababu taasisi nyingi duniani na zinazofanya kazi kwa uwajibikaji na haki siyo rahisi kukuta wenyeviti wanaongoza vikao vya utendaji au wao ni wajumbe wa vikao hivyo na hili liko wazi.
Haiwezekani lipumba awe mwenyekiti wa kamati ya utendaji ya taifa au awe mjumbe wa kamati hiyo.
Hii ni kwa sababu kwa mamlaka yake kama kiongozi mkuu wa chama hawezi kuwa mtendaji mkuu wa chama.
Advantage tuliyonayo ni kwamba mwenyekiti wetu taifa anabakia akifuatilia masuala yote muhimu ya utendaji na akihoji na kuturudisha kwenye mstari. Na hata tunapokuwa katika vikao vya baraza kuu yeye huongoza wajumbe wa baraza huu kupata ufafanuzi wa mambo muhimu kutoka kwa kamati ya utendaji ya taifa.
Hii ina maana kuwa mwenyekiti wa chama yuko juu ya mambo ya utendaji ya chama, yeye ana-monitor, ana-advise , ana-recheck and re-correct mienendo ya kamati ya utendaji wa taifa.
Hatari ya kuwa na mqenyekiti anayeongoza utendaji katika chama ni kuwa jambo lolote dogo likiharibika, anahusishwa moja kwa moja na hiyo ni hatari kwa taasisi.
Leo pana shutuma kadhaa zimetolewa na baadhi ya viongozi wenzrtu kuwa fedha za chama zimeliwa, au helikopta ilikodiwa kwa bei ya juu n.k.(tuhuma hizi ni za kupikwa tu na hazina uthibitiaho wowote kama nilivyowahi kuthibitisha hapa).
Katika mazingira ya namna hiyo mwenyekiti taifa anapokuwa mtendaji angehusishwa na kila tuhuma ndogo katika chama, jambo amablo siyo sahihi hata kidogo.
Binafsi nadhania utaratibu wetu ni muhimu sana na muhimu ukaendelea.
vipi kuhusu zile barua pepe zenye maelekezo ya jinsi ya ku deal na suala la mpiganaji Hamad Rashid toka kwa maalim Seif kwenda kwa profesa ambaye sio mjumbe wa hicho kikao,nazungumzia barua pepe ambazo mpiganaji Hamad Rashid anadai kuzinyaka kabla ya kikao.what is your reaction kamanda?