Uchaguzi 2020 Maalim Seif: CCM imeweka mikakati yake ya kumtafutia ushindi Dkt. John Magufuli, Tundu Lissu aje nimpe mikakati ya kushinda kwenye Uchaguzi

Mgombea aliyewahi kushindwa na CCM hiyohiyo mara tano, Leo amekuwa fundi wa kuwapa Mbinu wengine kushughurika na CCM hiyohiyo.

Hivi, mpaka muda huu, bado kunamjinga anaamini CCM itashindwa mwaka huu, Walishindwa kuing'oa 2015 wakiwa na ukawa wenye Vyama zaidi ya vinne na wanasiasa wakongwe na maarufu na wenye uzoefu wa kisiasa mara tatu zaidi yao, waje kuweza leo?

Ujinga kwelikweli!!
 
Maalimu seif safari hii, anashindwa kwa tofauti kubwa kuwahi kutokea katika historia ya uchaguzi zanzibar. Kijana mchapakazi Hussein Ally Hassan Mwinyi ndiye chaguo la kizazi kipya
Siiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiisiem WOYYEEEEEEEEEEEEEEEEEE!! ✌ ✌✌✌✌✌🐸🐸
 
Tatizo hujui kilichopo. Watu wa deep state wanaelewa kila kitu. Kwanza fungua fumbo LA mzimu wa 2015 Kule Zanzibar na kilichojiri. Hivi unaamini Maalim ashiriki tens uchaguzi kwa mazingira Yale Yale? Jiulize kunani? Think big. Kichwa unaambiwa kinatoka ACT.

Lissu nenda kwa Maalim ukachukue mbinu, nenda.


Mkuu Hakuna jipya. Banda ya October 28 utasikia tuliibiwa kura ..mara hatumtambui rais . Ukistuka 2025
 
Mgombea aliyewahi kushindwa na CCM hiyohiyo mara tano, Leo amekuwa fundi wa kuwapa Mbinu wengine kushughurika na CCM hiyohiyo.

Hivi, mpaka muda huu, bado kunamjinga anaamini CCM itashindwa mwaka huu, Walishindwa kuing'oa 2015 wakiwa na ukawa wenye Vyama zaidi ya vinne na wanasiasa wakongwe na maarufu na wenye uzoefu wa kisiasa mara tatu zaidi yao, waje kuweza leo?

Ujinga kwelikweli!!
Alishindwa au aliporwa ushindi?
 
Maalimu seif safari hii, anashindwa kwa tofauti kubwa kuwahi kutokea katika historia ya uchaguzi zanzibar. Kijana mchapakazi Hussein Ally Hassan Mwinyi ndiye chaguo la kizazi kipya
Uwe unaona aibu kuongea urongo 2015 maalimu alishindwa au alishindwa?
Jecha akifanya Nini,tuanzie hapo kwanza kabla hujaendelea
 
maalim seif ni sayari nyengine acha mazoea mara hii hali yenu ni ngumu zaidi pande zote, jiulize swali 1 tu moyoni mwako, kwanini maalim seif ameijua mikakati ya jiwe kupewa ushindi mapema hivi? ni wazi huko juu kumeoza wachawi wanaomtafuna jiwe ni wengi ambao utawaona bega kwa bega pamoja naye lakini nje ya hapo ni nyoka.

Acha wajidanganye kuwa ndiyo wao tu wenye maafisa vipenyo.

Mwaka huu mbona wataula wa chuya?
 
Maalimu seif safari hii, anashindwa kwa tofauti kubwa kuwahi kutokea katika historia ya uchaguzi zanzibar. Kijana mchapakazi Hussein Ally Hassan Mwinyi ndiye chaguo la kizazi kipya

Replace:

"Anashindwa" = "anaibiwa"

"Kibazo kipya"="mamlaka iliyopo"
 
T
Tundu Lissu kura tunakupigia.. na tutazilinda. Mikakati hiyo ya hawa jamaa ya wizi please ujiandae namna ya kukabiliana nayo. Kama kuna ambacho wananchi tunatakiwa kufanya cha ziada tujulishe. Sasa hivi enough is enough. Hatutaki tena kuongozwa kwa masimango na dhulma. Tunakutaka wewe.
Tarehe 28 sio mbali mutacheki picha halafu kama kawaida yenu msingizie kuibiwa sijui mnaibiwaje wakati mume weka mawakala kila kituo, halafu mulivyo na roho mbaya munawashindisha njaa hata chakula hamuwapi.
 
Mgombea aliyewahi kushindwa na CCM hiyohiyo mara tano, Leo amekuwa fundi wa kuwapa Mbinu wengine kushughurika na CCM hiyohiyo.

Hivi, mpaka muda huu, bado kunamjinga anaamini CCM itashindwa mwaka huu, Walishindwa kuing'oa 2015 wakiwa na ukawa wenye Vyama zaidi ya vinne na wanasiasa wakongwe na maarufu na wenye uzoefu wa kisiasa mara tatu zaidi yao, waje kuweza leo?

Ujinga kwelikweli!!
Aliyeporwa USHINDI MARA 5 sio kushindwa 🥰🥰🤣🤣😁
 
Tatizo hujui kilichopo. Watu wa deep state wanaelewa kila kitu. Kwanza fungua fumbo LA mzimu wa 2015 Kule Zanzibar na kilichojiri. Hivi unaamini Maalim ashiriki tens uchaguzi kwa mazingira Yale Yale? Jiulize kunani? Think big. Kichwa unaambiwa kinatoka ACT.

Lissu nenda kwa Maalim ukachukue mbinu, nenda.
Kwanini hawa jamaa wanacheza na akili zenu wakuu. Kama kuna mkakati wa siri, ili ujumbe umfikie Lissu ni lazima aende kwake na ilikuwa lazima amuite kwa mbiu ya mgambo ya hadharani kama hivi.
 
Maalimu seif safari hii, anashindwa kwa tofauti kubwa kuwahi kutokea katika historia ya uchaguzi zanzibar. Kijana mchapakazi Hussein Ally Hassan Mwinyi ndiye chaguo la kizazi kipya
Kijana ambaye hakupata hata kura moja ya wajumbe wa Zanzibar ambao ni wa chama twawala. Aliwekwa ulingoni kwa kusukumizwa kwa kura za wadanganyika! Yakhe wanchoka kuletewa rais kutoka bara. Sasa basi!
 
Hii sio siri. Kujua kama kuna Mikakati na janjajanja za wizi ni jambo moja ila kuizua ni jambo jingine kabisa.

Labda Maalim Seif atashare uzoefu wake wa kuporwa ushindi tangu 1995, ilikuwaje na yeye akashindwa kuzuia/kupindua meza iliyopinduliwa na kajipangaje 2020 hii
Mara zote Maalim Seif alipokuwa akiporwa ushindi wake, yeye alikuwa ana amini kuwa CCM wanapiga kura zaidi ya mara moja tu. Na kwamba akiamini kuwa kura zake zinabaki kama zilivyopigwa. Uchaguzi wa 2015 baada ya Mansour kujiunga na CUF, ndipo alipomtobolea siri zote namna anavyoibiwa. Ilikuwa ni mawakala wake mwenyewe na baadhi ya watu walioko juu kwenye CUF walikuwa wakipewa mpunga wa kutosha kuonesha kuwa kikura wamezidiwa CUF. Watu walilazwa hospitali baada ya Mansour kumuonesha Seif wanafik wake. Ndio maana 2015 ikawa ngumu kwa CCM kutoa mpunga kwa mawakala maana maalim alikaba hadi kivuli, matokeo yakimaliza kuhesabiwa tu yanarushwa ofisi kuu. Unaambiwa Mansour alipokwenda kwenye jimbo lake alimkuta wakala wake anasinzia, alimpa kibao kimoja tu :D

Maalim alishindwa kupinduwa meza kwa sababu CCM wanatumia nguvu ya jeshi. Unaambiwa wafanyakazi wa umma washaambiwa wamepeleka vitambulisho vyao vya kupiga kura. Lengo ni kuwa watie CCM ama kibarua hawana.

Maalim kwa 2020 asipopewa urais, hakuna dalili kama ataweza kugombea tena 2025, hivyo mwaka huu kwa yeye naweza kusema kuwa he has nothing to loose, atategemea wafuasi wake ndio iwe sababu ya yeye kuapishwa. Namaanisha, ile kauli yake ya liwalo na liwe, huenda mwaka huu la kuwa likakuwa kusudi dunia ione udhalimu wa CCM.
 
Kijana ambaye hakupata hata kura moja ya wajumbe wa Zanzibar ambao ni wa chama twawala. Aliwekwa ulingoni kwa kusukumizwa kwa kura za wadanganyika! Yakhe wanchoka kuletewa rais kutoka bara. Sasa basi!
Hili jambo hata CCM wenyewe limewakereketa kwa kweli lakini hawapo tayari kukosa ugali wao. Lakini all in all, Mwinyi ndio chaguo sahihi kwa CCM kuliko hata wale waliochaguliwa na CCM Zanzibar. Japokuwa udhalimu kwenye sanduku utafanyika, lakini nina imani, Mwinyi atakapokuwa rais, kuna possibility kubwa ya kusimamia miradi ya Zanzibar vizuri kuliko wale waliochaguliwa ma CCM Zanzibar. Mfano, barabara ya kujengwa 2020 itajengwa 2020 wakati wale wa CCM Zanzibar, wangesubiri 2025 ndio waijenge. CCM Zanzibar wamekuwa walafi mno sana, wanafikiria matumbo yao tu. wamekuwa watu wa roho mbaya, na wao ndio wanaosababisha CCM Zanzibar kuzidi kuchukiwa. Huko Makunduchi kwenye ngome yao, unaambiwa watu wamewachoka, wanasema mara hii bora wakipe chama kingine tu waone kama watapata mabadiliko.

Binafsi, suala la kuchaguliwa viongozi Zanzibar bara naona ni vyema tu. Ndipo CCM Zanzibar watakapotia akili.
 
Ni enzi hizo si wakati huu! Seif kachoka na kizazi chake pia kimechoka..

Kizazi kinachopiga kura zanzibar wakati huu ni kile kilichozaliwa ndani ya Muungano
Watu wamehasika mara 1000 zaidi saivi jamaa wanatapatapa tu huku Zanzibar wanalazimisha wafanya kazi wapeleke Vitambulisho vya Zanzibar mkaazi, cha mpiga kura na kituo cha kupigia kura.
Hali yao ni ngumu sana ila ng'ombe atakavo lala ndivyo tutakavyomchinja.
 
Mgombea aliyewahi kushindwa na CCM hiyohiyo mara tano, Leo amekuwa fundi wa kuwapa Mbinu wengine kushughurika na CCM hiyohiyo.

Hivi, mpaka muda huu, bado kunamjinga anaamini CCM itashindwa mwaka huu, Walishindwa kuing'oa 2015 wakiwa na ukawa wenye Vyama zaidi ya vinne na wanasiasa wakongwe na maarufu na wenye uzoefu wa kisiasa mara tatu zaidi yao, waje kuweza leo?

Ujinga kwelikweli!!
Nimeshangaa...
 
Back
Top Bottom