CHADEMA iende kuwekeza nguvu Zanzibar

econonist

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
15,804
21,777
Hakuna wakati muafaka Kama huu kwa chama Cha CHADEMA kwenda kuwekeza nguvu Zanzibar. Sababu zangu kwa ombi Hilo ni zifuatazo.

1. Kwanza, Kwa Sasa harakati za kisiasa Zanzibar zimepoa baada ya Maalim seif Kuondoka duniani. Hivyo kwa Sasa upinzani Zanzibar hauna political figure kama ilivyokuwa kwa Maalim Seif. Akina Ismail jussa ni kama wapo kimya na wameshindwa kuwa key figures.

2. Pili, chama Cha ACT kipo kwenye serikali ya umoja Zanzibar,hivyo kufungwa gavana kutokana na makubaliano. Hii inaipa CHADEMA nafasi ya kujijenga Kama chama kikuu Cha upinzani Zanzibar kisichofungamana na serikali ya Zanzibar ambacho kitakiwa huru kuelezea agenda ya wazazibari bila hofu.

3. Tatu, CHADEMA kujijenga na kuwekeza nguvu Zanzibar kutaifanya kuwa chama Chenye sura ya Muungano. Maana kwa Sasa kinaonekana Kama chama Cha bara pekee. Na hivyo kuleta ushindani wa kisiasa.

4. Nne, CHADEMA watumie kukubalika kwao kwa baadhi ya wapinzani Zanzibar kujijenga. Kwa mfano kwenye uchaguzi wa 2020 wakati wa kampeni za urais CHADEMA, wazanzibar wengi walijitokeza kumsikiliza Mgombea Tundu Lissu na walimwelewa Sana. Hii inammanisha Kuna wazanzibar wanaiamini Sana misimamo ya CHADEMA na wangependa kiwe active kule visiwani.

Nihitimishe kwamba, kwa Sasa Zanzibar inakihitaji chama Cha CHADEMA kuliko wakati wowote, na kikiingia kule ni miaka mitano tu kitakiwa kimejisimika. Aliyeipa nguvu ACT ni Maalim Seif, Sasa hayupo wanategemea zaidi Makamu wa kwanza wa Rais ambaye hajawa influencial Kama Maalim Seif alivyokuwa.
 
Wasije wakajaribu ,Zanzibar kila siku wanaimba wamechoka wanataka inchi yao ,halafu mnavyomtukana Mzanzibari aliebahatika kuukwaa Uraisi wa Tanzania baada ya Nusu karne tangu Muungano utahiriwe na kuwa nchi moja ya Tanzania.
Jingine Chadema ni chama cha kidini tunawaona maaskofu wakubwa kwenye meza kuu,na baadhi ya waislamu walio wanafiki ,hakiwezi kukubalika Zanzibar zaidi ya kukubalika na walevi ,si unajua kanisa halikatazi mvinyo hivyo mtawapata wawili watatu ,ila Mzenji alietulia na kuitambua kuwa yupo katika heka heka za kudai Nchi ,huyo hamumpati.
 
Hakuna wakati muafaka Kama huu kwa chama Cha CHADEMA kwenda kuwekeza nguvu Zanzibar. Sababu zangu kwa ombi Hilo ni zifuatazo.

1. Kwanza, Kwa Sasa harakati za kisiasa Zanzibar zimepoa baada ya Maalim seif Kuondoka duniani. Hivyo kwa Sasa upinzani Zanzibar hauna political figure kama ilivyokuwa kwa Maalim Seif. Akina Ismail jussa ni kama wapo kimya na wameshindwa kuwa key figures.

2. Pili, chama Cha ACT kipo kwenye serikali ya umoja Zanzibar,hivyo kufungwa gavana kutokana na makubaliano. Hii inaipa CHADEMA nafasi ya kujijenga Kama chama kikuu Cha upinzani Zanzibar kisichofungamana na serikali ya Zanzibar ambacho kitakiwa huru kuelezea agenda ya wazazibari bila hofu.

3. Tatu, CHADEMA kujijenga na kuwekeza nguvu Zanzibar kutaifanya kuwa chama Chenye sura ya Muungano. Maana kwa Sasa kinaonekana Kama chama Cha bara pekee. Na hivyo kuleta ushindani wa kisiasa.

4. Nne, CHADEMA watumie kukubalika kwao kwa baadhi ya wapinzani Zanzibar kujijenga. Kwa mfano kwenye uchaguzi wa 2020 wakati wa kampeni za urais CHADEMA, wazanzibar wengi walijitokeza kumsikiliza Mgombea Tundu Lissu na walimwelewa Sana. Hii inammanisha Kuna wazanzibar wanaiamini Sana misimamo ya CHADEMA na wangependa kiwe active kule visiwani.

Nihitimishe kwamba, kwa Sasa Zanzibar inakihitaji chama Cha CHADEMA kuliko wakati wowote, na kikiingia kule ni miaka mitano tu kitakiwa kimejisimika. Aliyeipa nguvu ACT ni Maalim Seif, Sasa hayupo wanategemea zaidi Makamu wa kwanza wa Rais ambaye hajawa influencial Kama Maalim Seif alivyokuwa.
Upo sahihi
 
Wasije wakajaribu ,Zanzibar kila siku wanaimba wamechoka wanataka inchi yao ,halafu mnavyomtukana Mzanzibari aliebahatika kuukwaa Uraisi wa Tanzania baada ya Nusu karne tangu Muungano utahiriwe na kuwa nchi moja ya Tanzania.
Jingine Chadema ni chama cha kidini tunawaona maaskofu wakubwa kwenye meza kuu,na baadhi ya waislamu walio wanafiki ,hakiwezi kukubalika Zanzibar zaidi ya kukubalika na walevi ,si unajua kanisa halikatazi mvinyo hivyo mtawapata wawili watatu ,ila Mzenji alietulia na kuitambua kuwa yupo katika heka heka za kudai Nchi ,huyo hamumpati.
Sio kweli kwani wazemji wote wanampenda Samia kisa tu ni mzenji? Mbona 2015 CCM ilipata 40% za Urais wa muungano au hawakumuona Samia ni mgombea mwenza?

Samia hajawahi pigania Zanzibar huru ila Lissu amefanya hilo time and time again ndio maana 2020 alizoa kura za Bure kabisa Zanzibar hata kumzidi mgombea wa ACT licha ya kuwa CHADEMA Haina hata diwani.
 
Back
Top Bottom