Mkuu point of correction! Nyerere alijitahidi sana ktk kipindi chake! Kufikia 1975 Tanzania ilikuwa kwa kasi ya ajabu kiuchumi, Viwanda, mashamba na exportation ilikuwa juu... Nyerere alipiganishwa vita na Amin bila ya yeye kujua, baadae nchi washiriki zilianguka kiiuchumu! Tanzania ilipigwa sunction kubwa kuliko ile ya Zimbabwe kwani Nyerere alikataa katakata kukubali Madini, Mafuta na Gesi yetu kuchimbwa kasha sisi kuachiwa mashimo kama kule Niger Delta!!! Shell waliondoka kwenda Sudan ambapo Albashir alivunja mkataba na kuwapa WACHINA... KOSA la NYERERE ni kutuletea Benjamin William Mkapa an Economic Hit Man alieandaliwa mara baada ya JKN kumpeleka USA kuw balozi! BMW alikamatwa na akina Ballali na kuandaliwa vilivyo kuwa EHM! ...Itoshe kusema JKN hakujua kuwa kijana wake alikwisha tekwa muda mrefu kuwa EHM... JKN alikuja kugundua mpango mzima baada ya BWM kuuza NBC! Hapa Mwalimu alikwenda kumuona Clinton na kumueleza masikitiko yake ya kuuzwa kwa Assets za NBC na NMB ambazo zimetapakaa nchi nzima! alimweleza kuwa wanachohitaji ni Credits tu na kama suala ni uwekezaji basi wabinafsishe Operations siyo Fixtures (majengo), mara baada ya kikao hicho (1998) Prof Stieglitz aliekuwa mshauri wa Clinton - uchumi alijiuzulu nafasi yake na kusema kuwa anakubaliana na JKN mwanzo mwisho... Inasemekana JKN aliandaliwa trip ya South Africa then UK ...Sasa tuna muenzi Baba wa Taifa kwa Kukinzana na nadharia zake zote! Hata zile zenye manufaa kwetu!!! Itoshe kusema Watanzania tulikosea sana Kuwa na BENJAMIN WILLIAM MKAPA !!! Huyu ndo chanzo na matatizo yote ya Tanzania ya sasa!!! Amini msiamini JK hapo alipo anatamani muda wake uishe salama kwani anafanyakazi katika mazingira na sera mbovu sana walizotengeneza EHM ambazo haiwezekani kuziondoa overnight ...
Kuna mambo mengi uliyoandika sikubaliani na wewe.
Mwaka 1975 kweli uchumi wa Tanzania ulikuwa mzuri, kwa mwaka ule kutokana na bei ya kahawa kupanda sana baada ya kahawa ya Brazil kuungua kwa baridi 1974. Mwaka 1973 na 1974 uchumi wa Tanzania haukuwa mzuri kabia kutokana na kupanda sana kwa mafuta- Petroleum.
Hata kabla ya vita vya Amini mambo hayakuwa shwari sana. Vitu madukani mara nyingi vilikuwa vinakosekana hasa hasa, unga, mchele, mafuta ya kupikia, sabuni, n.k.
Nyerere aliondoka madarakani akiiacha Tanzania ikiwa hoi kwelikweli kiuchumi. Benki Kuu walikuwa hawana hata dollar millioni moja!
Alipoingia Mwinyi alikuta mambo mazito. Mwanzoni tu nchi nzima ilikuwa haina kabisa mafuta (hiki kilikuwa ni kitu cha kawaida wakati wa JKN). Ilibidi kusaini mkataba na Waarabu kubadilishani kahawa na mafuta. Mwinyi alijaribu kufungua uchumi wa Tanzania lakini walionufaika walikuwa ni wachache sana na kodi hazikulipwa. Tanzania ilibanwa sana na World Bank, IMF, na nchi wafadhili hasa kutokana na deni kubwa lililokuwa linaisonga Tanzania.
Mkapa alipoingia alijitahidi kulipa madeni kusudi angalau nchi ikopesheke. Ukata (Ukapa) uliumiza wengi lakini baada ya hapo madeni yalisamehewa madeni mengi. Migodi mingi ilifunguliwa na mashirika mengi yaliuzwa. Kwenye migodi kwa kweli Watanzania hawakunufaika sana lakini vile vile hili lilitokana na shinikizo la World Bank na IMF waliotaka Tanzania ifuate model ya nchi kama Chile. Uuzaji wa mashirika ulikuwa na matatizo yake lakini binafsi nakubaliana naye 100%. Mashirika na viwanda vilikuwa ni mzigo mkubwa kwa wananchi. NBC ilikuwa ni mzigo mkubwa kwa wananchi. Serikali ilikuwa haipati kodi kutoka NBC. Sana sana NBC ilikuwa mbele kuchangia mikutano ya NEC ya CCM kule KIzota na sherehe nyingin za chama. Afadhali ilikufa! Leo wanalipa kodi na serikali inapata gawio la faida.
Mkapa alifanaya vizuri sana sana katika kuinua uchumi wa Tanzania. Kikwete alipoingia madarakani alikuta mwanga na hewa safi katika uchumi wa Tanzania. Forex Reserves aliyoacha Mkapa ilikuwa kama USD 4 bn na Export zilikuwa juu kuliko alipochukua nchi.
Marais walioingia madrakani wakiwa na wakati mzuri ni Nyerere na Kikwete. Nyerere alichukua nchi ikiwa maskini lakini system zote zilikuwa zinafanya kazi. Kikwete amechukua nchi ikiwa katika hali afadhali kiuchumu kuliko wakata Mwinyi na Mkapa wanaingia madarakani.
Samahani kwa ujumbe mrefu.