Rangi yoyote ile lazima iwe na kitu kinaitwa 'RGB VALUE'. Hii ni ratio ya mchanganyiko wa rangi tatu za msingi. R stands for red, G-green and B- Blue. Pata mwanga hapa http://en.wikipedia.org/wiki/List_of_colors:_A–F
nimekusoma mkuuRay lee black is the absence of color. huo mchanganyiko huleta hali ya kushindwa kuakisi rangi ya aina yoyote ile kutoka kwenye mwanga mweupe. hivyo kinachotokea hapo ni giza a.k.a weusi.
Hapa duniani inakadiriwa kwamba kuna rangi takribani milioni 6 mpaka 7 ambazo zinaweza kuonekana kwa kutumia macho bila msaada wa kifaa chochote kile!
Pia inafahamika kwamba rangi hizo zote zinatokana na mchanganyiko wa rangi tatu za msingi ambazo ni Nyekundu, Kijani, na Kibluu. Mfano rangi ya Chungwa, Udhurungwi, Zambarau n.k hupatikana kwa kuchanganya rangi hizo tatu kwa uwiano flani ili kupata matokeo tarajiwa.
Lakini vile vile mchanganyiko wa mwanga wa rangi tatu za msingi huleta mwanga wa rangi nyeupe, hivyo tunasema mwanga wa rangi nyeupe ni mchanganyiko wa rangi zote duniani, na consequently ukiutawanya mwanga mweupe utaziona rangi hizo zote.
Utaalam/ujuzi huu umekuwa muhimu sana katika ugunduzi wa taa za LED zenye mwanga mweupe na ambao huokoa umeme kwa asilimia 90%! Hapo awali iliwezekana kutengeneza 'light emitting diode' (LED) zenye kutoa mianga yenye rangi nyekundu na kijani, baada ya miaka mingi ya uhangaikaji iliwezekana kutengeneza 'LED' zenye kutoa mwanga wa bluu na hivyo muunganiko wa hizo tatu uliwezesha utengenezaji wa taa za LED nyeupe na kuleta mapinduzi katika teknolojia zenye kuokoa nguvu ya umeme!
Inawezekana mi sio mtaalam kuliko ww,ninachofaham rangi za msingi ni red,blue,yellow...labda unieleweshezaidi
Ahsante kwa ufafanuzi murua kuhusu hilo swala la yellow..Topic kama hizi ni nzuri sana kwani zina mafundisho kwa anaezipita. Ahsante.
Kwa kuweka sawa kidogo na kuongezea utamu ili watu waelewe vyema kuhusu "primary colors":
Hizo rangi tatu ulizozitaka ni kwa ajili ya "display" za elektroniki au (umeme) kitaalam huitwa "additive combination of colors".
Lakini rangi tatu za "primary" za kuchorea au ku print au kufanya "dye" za nguo ni "magenta, yellow an cyan" na kitaalam huitwa "subtractive combination of colors".
Ni kuweka sawa tu ili ufahamu wa watu upanuke.
sikubishii coz wapo wanaosema hivyo pia..so unaweza kuchukua unachoamini ww
BujiBuji, weusi si rangi bali ni 'hali'. Infact hakuna kitu kama rangi nyeusi hapa duniani, kwanini nasema haya?!
Ili rangi iwe rangi inabidi iwe na uwezo wa kutoa mwanga wa rangi husika, mfano utakuta kuna taa zinazotoa mwanga wa bluu, 'orange', kijani n.k, lakini hatakuta taa inayota mwanga mweusi!
Weusi ni hali ya kushindwa ku-reflect/kuakisi rangi yoyote ile kati ya zile rangi milioni takrian 7 zilizopo kwenye mwanga mweupe, na badala yake huzinyonya rangi hizo zote na kuacha hali ya giza kwenye eneo husika, ambapo wewe umeamua kuita ni 'rangi nyeusi', lakini neno sahihi ni 'hali ya weusi'...!
Kitu cha bluu hunyonya rangi zote zilizo kwenye mwanga mweupe na kuakisi/ku-reflect rangi moja tu ambayo ni rangi ya bluu.., hali kadhalika kwa rangi zingine zote.., lakini vitu vyenye hali ya weusi havina uwezo huo!
Hapo umenielewa..Sio rangi, mwanga mweusi unapatikanaje!
Yellow ni rangi ya msingi,haipatikani kwa kumix na rangi yyte
Rejea ufafanuzi wa Faiza Foxy hapo juu..Njano sio rangi ya msingi
Umeshawahi kuona duka linalouza taa nyeusi?Sio rangi, mwanga mweusi unapatikanaje!
Bila Shaka unamzungumzia moudy physics... Mchikichin hiyo aise pale tumepitia wengi