Habarini Wadau,
Leo asubuhi niliamka nikiwa na mood mbaya ila wakati nakunywa chai nikajikuta naanza kucheka sana na kila nikikumbuka najikuta nacheka tu hata kimoyoni.
Ni hivi nina Kaka yangu, ni mtu mzima tu na alishaoa na kuwa na mtoto mmoja na sasa mkewe ni mjamzito hivyo anatarajia mtoto wa pili.
Asubuhi nimempigia simu mama kumjulia hali, baada ya maongezi mafupi akaniambia kwa kilugha
"Hivi wewe huwezi kupiga nyumba rangi?"
Nikamwambia hapana mama, mara akaniambia
"sasa si ukaongee na kaka yako kuhusu huyo mpiga rangi?"
Akaongeza..."Nyie ni watu wazima sasa msinisumbue" akakata simu.
Ikabidi nimpigie kaka kujua kuna nini juu ya mpiga rangi.
Kumbe bana wiki mbili zilizopita alimleta mpiga rangi kwenye nyumba yake kwaajili ya kubadilisha rangi sebuleni kwake.
MAAJABU:
Mke wake (shemeji yangu) ambaye ni mjamzito aliipenda sana harufu ya ile rangi ya ukutani na kila mara alipenda kukaa sebuleni siku nzima tena karibu na ukuta kabla rangi haijakauka.
TATIZO LILIPOANZIA:
Mke wa brother alichukua namba ya simu ya fundi rangi kumbe akawa anamwambia mara kwa mara
"Fundi si uje kurudia rangi koti nyingine jamani" kwani nilikufukuza kwangu? na alikuwa akimkumbusha mara kwa mara na mume wake akaja kuona messages ila hakumuuliza chochote.
Sasa mtoto wake kachafua ukuta kwa kuchora chora ndio kaka kaja juu kuwa mke wake ndio kachafua kwa makusudi ili nyumba ipigwe rangi na fundi yule yule.
Jana alipomtembelea mama jana ndio akamwambia anahisi mke wake anamsaliti kwa kutembea na fundi rangi.
Sasa mama anachosema ni kwamba "Mimba" yake ndio imependa hiyo harufu hivyo kaka aache kulia lia.
Hivi Kweli mimba ya mwanamke inaweza kupenda harufu kali kama hiyo ya rangi na wakati inaletaga hadi mafua?
Najua mwanamke akiwa mjamzito anaweza kupenda harufu ya dagaa ama malimao.
Ila Rangi?