1.Wachawi wanakamatwa na Mgambo
2.Majeruhi na maiti zinabebwa kwa mikono mitupu
3.Jini anavuka barabara anaangalia kulia na kushoto anaangalia usalama kwanza
4.Risasi inachukua Dakika kumfiki mpigwaji
5.Mtu yupo na demu wake supermarket wanachukua nusu saa nzima wakati movie ina saa moja na nusu
6.Mtu akipigwa ngumi anaangalia pakuangukia kwa usalama wake
7.Milio ya Risasi kama unawasha njiti za kiberiti
8.Kahaba lazima avute sigara
9.Jambazi lazima livae koti refu na miwani meusi
10.Mganga wa kienyeji lazima awe porini,mchafu,halafu anaongea kwa ukali!
11.Kwenye subtitle mgeni anaitwa New People
12.Hospitalini wapo wao tu
13.Jambazi anavua viatu akavamia kwenye nyumba
14.Mtanga na Serengo lazima wawe walinzi
15.Jini lazima awe mwanamke
16.JB anavaa shati moja kwenye movie sita
17.Tukio linaonywshwa lilitokea mwaka 1977 halafu ukutani kuna picha ya Rais wa sasa Magu
18.Familia ya kitajiri lazima waongee kizungu Dadii!!..Mamii!!
19.Tajiri lazima amuoe maskini
20.Gereza ni nyumba ya mtu yenye madirisha ya chuma
21.Kila anayetoa habari za maisha yake ya nyuma lazma anyanyue uso juu
22.Mapenzi yanaanza pale mwanamke anapoalibikiwa na gari afu mwanaume anatokea kusaidia
23.Mlinzi wa getini lazima awe hana akili nzuri
24.Kitu pekee kinachoharibika ni Glass tu
25.jambazi laziwa awe na sura mbaya na awe ananuna muda wote
26.Movie inaanza mtoto mweusi kichwani kipilipili cha nguvu, akiwa mkubwa ni mweupe na nyele za kiarabu
Nalog Off bongo movie
Malizia na ww.