Lwakatare Hajawahi Kusimamia Ndoa Yangu

Lwakatare Hajawahi Kusimamia Ndoa Yangu

Ili kuweka kumbukumbu sawa na kusahihisha upotoshaji na uongo wa wapuuzi wanaodanganya watu kuwa huyu ndugu ndiye alifadhili harusi na ndoa yangu.

unajua maana ya ufadhiri wewe? Huoni kama hiyo elf 30 kma ufadhiri?
 
Huyu kijana sijamwelewa anadai chama chao cha CHEDEMA hivi yupo chedema ipi?
 
Mkuu endelea kutujaza na kutuhabarisha mambo ambayo chadema wamepotosha Umma!
 
Ninyi vijana mna matatizo kweli kweli na mnakosa uadilifu. Weka orodha basi ya wote walio kuchangia na kiasi cha mchango wa kila mmoja ili umma uone ulipata kiasi gani na nani alikuwa muhimu sana kwako kwa kukuchangia kiasi kikubwa! Kama Mh Lissu alisema na watu wengine wakaamini, inakuwaje uelekeze umma Lwakatare alikuchangia kiasi gani?!
 
Hii habari haijawa timely,naomba kuuliza mlikkuwa na uhusiano gani kifamilia na Lwakatare, vp uliwahi kuishi kwake? Je una ugomvi nae?

Sent from my BlackBerry using JamiiForums

nakushukuru mkuu .
 
View attachment 187933

Wakuu,

Kumekuwa na madai ya uongo na kupotosha hapa kwa muda mrefu hapa kuwa Lwakatare ndiye alisimamia ndoa yangu. madai haya yalitolewa kwa mara ya kwanza na Tundu Lissu hadharani na tangu hapo mashabiki wa chama chetu cha CHADEMA wameendelea kuamini kuwa ni kweli Lwakatare alikuwa msimamizi wa ndoa yangu.

Napenda leo kusema rasmi kuwa ndugu Lwakatare hajawahi kuwa msimamizi wa ndoa yangu kwa maana ya patron (best man) wala kwa maana ya kuwa mfadhili mkuu. aliyesimamia ndoa yangu ni kijana mwenzangu anaitwa Prosper Mberwa (pichani kulia kwangu, na mke wake Savera (pichani kushoto kwa mke wangu). hawa wengine waliosimama nasi ni ndugu zetu wanafamilia wa pande zote mbili.

Nalizimika kusema kuwa Lwakatare alichangia harusi yangu kama wengine na alichangia SH. ELFU 30. namshukuru kama wote walionichangia.Picha hii ni authentic,ilipigwa Morogoro Hotel, jioni ya siku ya ndoa yangu tarehe 28 july,2012.

sasa wanaosema Lwakatare ndiye aliyesimamia ndoa yangu wanapotosha umma kwa sababu gani? uongo huu wa nini? maana siyo vizuri watu wanaoaminika na jamii kudanganya. "you can fool some people all the time, and you can fool all the people for some time, but you can not fool all the people all the times". sasa baadhi anzeni kuona kuwa watu hawa mnaowaamini sana wakati mwingine hudanganya.


Sisi inatuhusu kitu gani?, Wewe ni mnafiki sana na muuwaji wa Demokrasia nchini kwetu.. Kama unafanya Ugaidi kwa Tsh 50,000/= ya Mwigulu kwanini uone 30,000/= za Rwakatare na Mtanzania wa kawaida ni ndogo? Wewe una akili hapo?
 
maandiko matakatifu yanasema kwamba SIKU YA MWISHO KILA GOTI LITAPIGWA .
 
modes pelekeni huu upuuzi kule jukwa la matangazo madogomadogo
 
sijawahi kuishi kwake. nimewahi kufika kwake mara mbili tu na mara zote sikuwahi kukaa zaidi ya saa mbili. lakini waongo wa chadema wamekuwa wanadanganya humu kuwa nimewahi kuishi kwake. huyu ndugu ni rafiki yangu tu

Ile video uliirekodi kwa masaa mangapi?
 
Wakati yakipotoshwa mliona ni sawaa tena mkashtuka kuwa kumbe ni mtu wake wa karibu namna hii ? Sasa kaja kusawazisha namuuliza kwani wewee ni nani na kwanini utaje kiasi na mambo mengine ya kuhoji kijinga kijinga kwani nyie Watanzania ni nani aliyewaloga ? Lwakatare ni gaidi tu
 
View attachment 187933

Wakuu,

Kumekuwa na madai ya uongo na kupotosha hapa kwa muda mrefu hapa kuwa Lwakatare ndiye alisimamia ndoa yangu. madai haya yalitolewa kwa mara ya kwanza na Tundu Lissu hadharani na tangu hapo mashabiki wa chama chetu cha CHADEMA wameendelea kuamini kuwa ni kweli Lwakatare alikuwa msimamizi wa ndoa yangu.

Napenda leo kusema rasmi kuwa ndugu Lwakatare hajawahi kuwa msimamizi wa ndoa yangu kwa maana ya patron (best man) wala kwa maana ya kuwa mfadhili mkuu. aliyesimamia ndoa yangu ni kijana mwenzangu anaitwa Prosper Mberwa (pichani kulia kwangu, na mke wake Savera (pichani kushoto kwa mke wangu). hawa wengine waliosimama nasi ni ndugu zetu wanafamilia wa pande zote mbili.

Nalizimika kusema kuwa Lwakatare alichangia harusi yangu kama wengine na alichangia SH. ELFU 30. namshukuru kama wote walionichangia.Picha hii ni authentic,ilipigwa Morogoro Hotel, jioni ya siku ya ndoa yangu tarehe 28 july,2012.

sasa wanaosema Lwakatare ndiye aliyesimamia ndoa yangu wanapotosha umma kwa sababu gani? uongo huu wa nini? maana siyo vizuri watu wanaoaminika na jamii kudanganya. "you can fool some people all the time, and you can fool all the people for some time, but you can not fool all the people all the times". sasa baadhi anzeni kuona kuwa watu hawa mnaowaamini sana wakati mwingine hudanganya.
umechanganyikiwa si kidogo wewe!
 
Wewe usitufanye sisi watoto wadogo.Ilipotolewa hii issue ya wewe kuruka ukuta mrefu mpaka watu kushangaa ulikua wapi uje kuongea leo?nani kakutuma?au akili zako huwa za msimu?Kwa nini hivi karibuni umekuwa ukiongea ongea issues za CDM?Kuna nini unakitafuta?
Ulipaswa kukanusha haya siku nyingi lakini sio leo.Usitafute umaarufu, wewe uliishajipaka kinyesi kwa kuonekana msalaiti.Hakuna atakae kuonea huruma.
 
Wewe usitufanye sisi watoto wadogo.Ilipotolewa hii issue ya wewe kuruka ukuta mrefu mpaka watu kushangaa ulikua wapi uje kuongea leo?nani kakutuma?au akili zako huwa za msimu?Kwa nini hivi karibuni umekuwa ukiongea ongea issues za CDM?Kuna nini unakitafuta?
Ulipaswa kukanusha haya siku nyingi lakini sio leo.Usitafute umaarufu, wewe uliishajipaka kinyesi kwa kuonekana msalaiti.Hakuna atakae kuonea huruma.

Hilo la kuruka ukuta nalo lina siku yake.polepole uongo wote utajitenga na wengi mtalazimishwa na facts kubadili mawazo. tufocus kwenye mada.haya mengine yana siku yake,moja baada ya jingine.
 
Wewe kijana una akili finyu na ndogo sana ,hata sijui ni nini unatafuta.
Mods pelekeni hii jukwaa la complains au hoja mchanganyiko, sioni ina uhusiano gani na siasa.
 
Back
Top Bottom