Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,192
- 25,493
Makosa ya ugaidi aliyoshtakiwa Alfred Lwakatare na mwenzake Ludovick Joseph yanaweza kuichafua nchi kimataifa.
Kwa mawazo yangu,makosa ya ugaidi ni makosa 'sensitive' na hivyo kuvuta hisia za mataifa ya nje yakiwemo ya America na Ulaya. Nijuavyo mimi, hii ni mara ya kwanza tangu sheria ya kuzuia ugaidi ilipoundwa na Bunge mwaka 2002 kwa mtanzania kushtakiwa kwa ugaidi hapa nchini. Tanzania tuna magaidi na ugaidi!?
Nionavyo, hata utalii na uwekezaji utapungua kwakuwa watalii na wawekezaji wengi wataiona Tanzania nchi isiyo na usalama sana na hivyo kuwatisha wawekezaji na watalii hao. Mashtaka ya Lwakatare na mwenzake yanaweza kuleta taswira mpya toka ile ya Tanzania yenye amani na utulivu hasa kimataifa.
Tufanye mambo yetu tukiwa tayari kupokea madhara na matokeo ya masuala hayo.
Muhimu: Haya ni maoni na mawazo yangu binafsi kwa mujibu wa Ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,1977(kama inavyorekebishwa mara kwa mara)
Kwa mawazo yangu,makosa ya ugaidi ni makosa 'sensitive' na hivyo kuvuta hisia za mataifa ya nje yakiwemo ya America na Ulaya. Nijuavyo mimi, hii ni mara ya kwanza tangu sheria ya kuzuia ugaidi ilipoundwa na Bunge mwaka 2002 kwa mtanzania kushtakiwa kwa ugaidi hapa nchini. Tanzania tuna magaidi na ugaidi!?
Nionavyo, hata utalii na uwekezaji utapungua kwakuwa watalii na wawekezaji wengi wataiona Tanzania nchi isiyo na usalama sana na hivyo kuwatisha wawekezaji na watalii hao. Mashtaka ya Lwakatare na mwenzake yanaweza kuleta taswira mpya toka ile ya Tanzania yenye amani na utulivu hasa kimataifa.
Tufanye mambo yetu tukiwa tayari kupokea madhara na matokeo ya masuala hayo.
Muhimu: Haya ni maoni na mawazo yangu binafsi kwa mujibu wa Ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,1977(kama inavyorekebishwa mara kwa mara)