Lwakatare ataichafua Tanzania

Lwakatare ataichafua Tanzania

Cha msingi haki itendeke. Hayo mambo ya kuichafua nchi hayapaswi kuwa kizingiti cha haki kutendeka.Kwani nchi gani hakuna ugaidi mpaka itunyooshee kidole. Labda Vatican peke yake ndio hakuna ugaidi.
Mnajitaidi sana kujitekenya na kucheka wenyewe huku ukweli wa jambo ili mkiujua, lakini mjue hapa CCM na serikali yake Wanaruka sarakasi huku wamevaa Taulo kitakachotokea ni kukaa UCHI.
 
Mnajitaidi sana kujitekenya na kucheka wenyewe huku ukweli wa jambo ili mkiujua, lakini mjue hapa CCM na serikali yake Wanaruka sarakasi huku wamevaa Taulo kitakachotokea ni kukaa UCHI.

Hakuna lolote ninalojua kuhusu ugaidi....
 
Wakenya bado hawaja take advatage,kwa hili kuchukua Watalii

Hivi nyinyi mnafikiri kila mtu ni poor thinker, ma great thinkers huwa hawakurupuki kutoa maamuzi.
Hivi ni ugaidi gani utamfanya mtalii aogope kuja Tanzania?

Kwanza hii kesi ya Rwakatale kweli ilistahili kuwa ya ugaidi au wamefanya hivyo ili kuikuza issue.

Pili, kama Tanzania haikuchafuka kimataifa kwa matukio mabaya yaliyowahi kutokea nchi hii, ukilinganisha na hili la Rwakatale basi haiwezi kuchafuka.
 
Na kitakachoipa sifa Tanzania ni kuanza kuwashughulikia kikamilifu Wahusika wakuu wa uvunjifu wa Amani kina Lwakatare na chama chake cha Demekrasia Feki!

DEMEKRESIA....!?? sikushangai, ndo matunda ya Mulugo
 
acha kumtaja taja mungu kwa mambo usio na uhakika nayo wala ujuzi nayo,acha sheria ichukue mkondo wake sio kila kitu ni siasa ndo mnaofanya cdm kionekane chama cha kidini

Achana nae gamba huyo
 
mkuu Petro E. Mselewa, kumbe wakati nimeshaanza kukata tamaa kwa idadi kubwa ya Watanzania ambao upeo wao wa kuona unaishia kwenye matumbo yao na anayekwenda zaidi ni matumbo ya familia zao lakini naona nyota kama wewe mnaoweza kuona maslahi kwa picha kubwa ya taifa la Tanzania. Asante sana japo ni wachache watakuelewa bado!
 
Kwa kuwa kiongozi wa Chadema anahusika na ugaidi ndio unataka Mahakama isimhukumu kwa ugaidi aliopanga kuufanya? ili kujipendekeza kwa watalii? hivi ulisoma shule wewe? sheria ya ugaidi ilipitishwa na Bunge na kama kuna magaidi wacha sheria ichukue mkondo wake! mbona Waziri Nchimbi aliposema Zanzibar kuna ugaidi mlifurahia? Zanzibar mnakiri kuna magaidi lakini wa kutoka bara mnataka wafichwe au washtakiwe kama majambazi! uhasidi na chuki ni vitu hatari sana!

Naona umewashwa na pilipili kwa sababu tu unaona utugawe bara na visiwani. Hakuna anayekataa sheria ya ugaidi kufanya kazi yake bali tunataka tujiridhishe kama kweli kulikuwa na upangaji njama ama ni sinema tu. Wewe hushangai kwamba mtu anaachwa huru kabla hajafika mbali anakamatwa kwa jambo lile lile? Kama kila mpango wa mauaji ni ugaidi, je kina Mwangosi na Dr. Ulimboka mbona wahusika wake wanajulikana kwanini hadi leo hakuna aliyesema kuwa ni ugaidi na wala hakuna cha maana kinachoendelea?

Wewe usitoe povu bure, kama ni ugaidi kweli basi kina Mwigulu Nchemba waliokuwa na mkanda wa mipango ya mauaji wangeuleta kwanza kabla ya kurukaruka na mikanda ya humu kwenye mitandao.
 
Na kitakachoipa sifa Tanzania ni kuanza kuwashughulikia kikamilifu Wahusika wakuu wa uvunjifu wa Amani kina Lwakatare na chama chake cha Demekrasia Feki!

Huu ni ushabiki usiokuwa na chembe cha busara ndani yake. Tumia akili acha kukurupuka. siyo lazima uchangie kila mada .

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Unajua kitu kinacholeta shida nchini kwetu kwa sasa ni kuwa CCM ishajua kuwa kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 hawana uwezekano wa kushinda uchaguzi kutokana na kukubalika sana kwa wananchi kwa CDM. Na wao wanaonekana hawako tayari kukabidhi madaraka kwa upinzani. Kwa hiyo wanalazimika kufanya hila za aina yoyote ili wabaki madarakani.

Kwa hiyo wameona mkakati mzuri kwao ni kuwabambikia kesi viongozi wote wakuu wa CDM ili ifikapo 2015 kusiwe na wagombea strong kwenye uchaguzi huo ili wao wapite kiulaini.

Hata hivyo mpango wao huo wanamagamba ushaanza kubackfire kwa kuwa watu waliofanya nao coalition mpango wao huo mwovu ambao ni Jeshi la Polisi na TISS hawakuapangilia uzuri mpango wao na sasa ushaanza kuwatokea puani. Lakini kwa sasa inabidi wawe wapole na wasubiri matokeo kwa kuwa mambo yote hayo wamejitakia wenyewe!!
 
Makosa ya ugaidi aliyoshtakiwa Alfred Lwakatare na mwenzake Ludovick Joseph yanaweza kuichafua nchi kimataifa.

Kwa mawazo yangu,makosa ya ugaidi ni makosa 'sensitive' na hivyo kuvuta hisia za mataifa ya nje yakiwemo ya America na Ulaya. Nijuavyo mimi, hii ni mara ya kwanza tangu sheria ya kuzuia ugaidi ilipoundwa na Bunge mwaka 2002 kwa mtanzania kushtakiwa kwa ugaidi hapa nchini. Tanzania tuna magaidi na ugaidi!?

Nionavyo, hata utalii na uwekezaji utapungua kwakuwa watalii na wawekezaji wengi wataiona Tanzania nchi isiyo na usalama sana na hivyo kuwatisha wawekezaji na watalii hao. Mashtaka ya Lwakatare na mwenzake yanaweza kuleta taswira mpya toka ile ya Tanzania yenye amani na utulivu hasa kimataifa.

Tufanye mambo yetu tukiwa tayari kupokea madhara na matokeo ya masuala hayo.

Muhimu: Haya ni maoni na mawazo yangu binafsi kwa mujibu wa Ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,1977(kama inavyorekebishwa mara kwa mara)
Serikali ya CCM inaona haina cha kupoteza maana haioni dalili za kuendelea kuwepo madarakani na ndio maana haitaki kujua madhara ya matendo yake. Hili unalolisema linaenda sambamba na hatua ya rais kuwaza kwenda kukopa na kuongeza deni la taifa kila siku.

Rais anataka hata CCM itapotoka serikali inayokuja ipate shida ya kulipa hayo madeni wanayokopa ili kuwezesha safari na kufanya matumizi ya kawaida na sio kuzalisha. Lengo la huu ukopaji ni kuwa serikali ya upinzani ikiingia madarakani, ihangaike kulipa madeni badala ya kuwafanyia wananchi maendeleo. Yapo mengi yanayoashiria kutikiwa mabaya kwa serikali ijayo.
 
Makosa ya ugaidi aliyoshtakiwa Alfred Lwakatare na mwenzake Ludovick Joseph yanaweza kuichafua nchi kimataifa.

Kwa mawazo yangu,makosa ya ugaidi ni makosa 'sensitive' na hivyo kuvuta hisia za mataifa ya nje yakiwemo ya America na Ulaya. Nijuavyo mimi, hii ni mara ya kwanza tangu sheria ya kuzuia ugaidi ilipoundwa na Bunge mwaka 2002 kwa mtanzania kushtakiwa kwa ugaidi hapa nchini. Tanzania tuna magaidi na ugaidi!?

Nionavyo, hata utalii na uwekezaji utapungua kwakuwa watalii na wawekezaji wengi wataiona Tanzania nchi isiyo na usalama sana na hivyo kuwatisha wawekezaji na watalii hao. Mashtaka ya Lwakatare na mwenzake yanaweza kuleta taswira mpya toka ile ya Tanzania yenye amani na utulivu hasa kimataifa.

Tufanye mambo yetu tukiwa tayari kupokea madhara na matokeo ya masuala hayo.

Muhimu: Haya ni maoni na mawazo yangu binafsi kwa mujibu wa Ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,1977(kama inavyorekebishwa mara kwa mara)

Tanzania haiwezi kueleweka vibaya kwa kosa la ugaidi kwa sababu Lwakatare ameshitakiwa kwa kosa ambalo hakulitenda wala halikutendeka.watakacho washangaa wa Tanzania ni jinsi walivyo mambumbu wa kutafusiri sheria ya ugaidi.vinginevyo nao wameshatambuwa kuwa huu ni mchongo wa magamba.
 
nyie woote mnaoshabikia kesi ya kuzushi ya lwakatare kumbukeni majaliwa ya mikono yenu kwenda mdomoni yanaletwa na kodi za watanzania ambao kwa mamilioni ni maskini mnazusha kesi ili mpate kula amini nawaambieni ukweli hautacha kuwaumbua. mnatumwa na mafisadi kushabikia ufisadi wa siasa matoleo yake mtayaona tunashukuru mmejenga shuke za kata ambazo watoto wamefeli lakini wanauelewa mkubwa wa mambo likiwemo hili la nyinyi kutumwa kuitafuna na kuwalinda wala chi hii hawa watawatoa madarakani subilini
 
Double standards zinapoanza kutumika ndo utajua kilicho nyuma ya pazia. Hatukuona mtu akilalamika Nchimbi aliposema Tanzania (Zanzibar) kuna ugaidi, wote humu mlishangilia na FBI wameletwa! Leo Lwakatare kwa uzembe wake amefanya hayo aliyoyafanya wala haijatangazwa kwa kiwango kile cha Nchimbi mmeanza kulalamika!Kila jambo lina mwanzo wake, mlipaswa kukemea wakati ule alipoanza so acheni kulalamika. Mnataka asishtakiwe? Ajabu basi maana huko walikosema kuna ugaidi hata kichanga cha gaidi hakijapatikana. Huku magaidi wanakamatwa redy handed, oooh itaitia aibu Tanzania. MUNGU NI MKUBWA.
 
Makosa ya ugaidi aliyoshtakiwa Alfred Lwakatare na mwenzake Ludovick Joseph yanaweza kuichafua nchi kimataifa.

Kwa mawazo yangu,makosa ya ugaidi ni makosa 'sensitive' na hivyo kuvuta hisia za mataifa ya nje yakiwemo ya America na Ulaya. Nijuavyo mimi, hii ni mara ya kwanza tangu sheria ya kuzuia ugaidi ilipoundwa na Bunge mwaka 2002 kwa mtanzania kushtakiwa kwa ugaidi hapa nchini. Tanzania tuna magaidi na ugaidi!?

Nionavyo, hata utalii na uwekezaji utapungua kwakuwa watalii na wawekezaji wengi wataiona Tanzania nchi isiyo na usalama sana na hivyo kuwatisha wawekezaji na watalii hao. Mashtaka ya Lwakatare na mwenzake yanaweza kuleta taswira mpya toka ile ya Tanzania yenye amani na utulivu hasa kimataifa.

Tufanye mambo yetu tukiwa tayari kupokea madhara na matokeo ya masuala hayo.

Muhimu: Haya ni maoni na mawazo yangu binafsi kwa mujibu wa Ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,1977(kama inavyorekebishwa mara kwa mara)

Siyo hilo tu,nina wasiwasi hata intergrity ya viongozi wetu itakuleta maswali kwa hawa donors wetu,na hasa pale haki za msingi za binadamu zitakapohusishwa na hili.
 
Nionavyo, hata utalii na uwekezaji utapungua kwakuwa watalii na wawekezaji wengi wataiona Tanzania nchi isiyo na usalama sana na hivyo kuwatisha wawekezaji na watalii hao. Mashtaka ya Lwakatare na mwenzake yanaweza kuleta taswira mpya toka ile ya Tanzania yenye amani na utulivu hasa kimataifa.

Mkuu binafsi sidhani kama uono wako katika jambo hili upo sahihi.
Suala la Lwakatare halina uhusiano wowote na usalama wa raia wa kigeni.
Bali ni jambo ambalo limekaa kama sio kisiasa basi kibinafsi zaidi.
Halina athari yoyote na usalama wa nchi kwani sio kosa la kihaini.
Ndio maana hata nchi za Magharibi hazijatoa taarifa ya hatari kwa wananchi wao.
 
Back
Top Bottom