Chuma Chakavu
JF-Expert Member
- Apr 16, 2011
- 1,523
- 655
Naomba maelezo kutoka kwa yeyote anaejua:Hapo hata mimi waliniacha hoi. Eti taifa la Israeli limeanzishwa juzi tu. Ina maana vitabu vya dini vinatudanganya? Mjadala uliegemea upande 1 (biased). Walishindwa ku-balance mjadala.
1. Je serikali ya palestina ilikuwa inaongozwa na kiongozi(rais, mfalme,sultani,waziri mkuu n.k) aliyeitwa nani (jina) hapo mnamo mwaka 1948 inaposemekana ndipo taifa la Israel lilipoundwa?
2. Hiyo palestina ilishawahi kutawaliwa kabla? Mkoloni aliitwa nani? (i.e. Nchi iliyoitawala palestina) Na ilipata uhuru mwaka gani?
3. Kwa kuwa inaaminika kuwa israel haikuwepo ila iliivamia ardhi ya palestina, je hawa wayahudi walizuka tu hapa duniani? Je hawana ardhi yao ya asili? Kama ipo ardhi yao ya asili, je ni wapi?
4. Kwenye vitabu vya dini, Biblia na Qur'an vyote vinatambua uwepo wa wana wa israel, je, kwa mujibu wa vitabu hivi, hawa wana waisrael walikuwa wanaishi wapi wakati huo? Hilo eneo/ nchi waliyokuwa wanaishi kipindi hicho, lipo hadi leo hii au lilitoweka halipo tena? Naomba nijibiwe kwanza hayo maswali japo ninayo mengine ya ziada.