Saint Ivuga
JF-Expert Member
- Aug 21, 2008
- 54,363
- 58,386
Lulu sasa alia kuchafuliwa | ||
MSANII wa filamu za Bongo mwenye umri mdogo na mambo makubwa, Lulu amesema kuwa anaumizwa na vyombo vya habari jinsi vinavyomuandika vibaya. Lulu anasema magazeti humuandika kwa kumchafua na si kumkosoa na hayamsaidii wala kumjenga. Aliongeza kuwa yeye ni binadamu kama wengine hivyo anahitaji heshima na kuwa na uhuru wa kufanya kile anachoamini kitamfurahisha kwa wakati huo. "Mimi si malaika hivyo kuna kipindi napenda kwenda kwenye burudani kama watu wengine lakini nikifika huko ndipo napata mikasa ya kuandikwa vibaya, naomba mnirekebishe si kunichafua zaidi," alisema Lulu. Alifafanua kuwa akiwa kwenye matembezi yake ya kawaida kama kwenye kumbi za starehe na kubadilishana mawazo na marafiki hapendi kufuatiliwa kwa kuwa anahitaji kuwa mtu huru kama wengine |