Lowassa: Tuzo ya amani imewaumbua CCM

Lowassa: Tuzo ya amani imewaumbua CCM

hao watoa tozo nadhanj wamepigwa na upofu. -wangejua jamaa jinsi alivyompeperusha Dr Slaa na Prof Lipumba kutoka ukawa nadhanj wangegairi.
- wangejua jinsi alivyoagiza mamluki kutoka nje ya nchi kuja kudukua kura kwenye database ya tume ya uchaguzi wangegairi
-wangejua mpango aliokuwa ameuandaa wa kutawala nchi akizungukwa na mafisadi wafanyabiashara wangengairi
-wangejua alivyotaka kuchaguliwa kuwa candidate wa ukawa na akakataa asishindanishwe na mtu yoyote wangegairi
-wangejua kuwa alinunua viongozi baadhi wa ukawa ili wamuunge mkono wangegairi
-wangejua Bashir Awale, mkuu wa Stanbic bank aliyekwapua 6 bilion na kampuni ya Kitilya ndie alikuwa mshauri wake wa karibu na mkenya wangegairi.
kuna mengimengi mengi ambayo tumekuja kugundua, yaani Mungu ni mkubwa. mpaka leo hatujui jamaa huyu angeshinda urais nchi hii ingekuwaje.

Kweli wewe ni lumumba buku 7 fc,NADHANJ?ndio lugha ya magamba?
 
....inatia shaka! kwamba taasisi zaidi ya alfu moja kidini, huko bukavu zimeamua kumtunuku tuzo ya amani bwana lowassa ...! inatia shaka, nia ya "hizo taasisi zaidi ya elfu oja", ukitilia ukarimu na uwezo wa bwana lowassa kuhamasisha harambee...lkn pia ni tuzo akishindanishwa na nani? ktk eneo gani? kama ni afrika, GoodluckJonathan wa Nigeria ambae sio tu alikubali kushindwa, na mpinzani wake wa dini ingine, lakini alimpigia na simu kumpongeza kwa ushindi, alishirikishwa? kisha ? hii tuzo si ni afadhali hata "madigirii ya udaktari wa falsafa" ambayo kiongozi wetu mmoja amekuwa akipatiwa kwa heshima! au? kujiliwaza na kujisifu katika up...zi?

Aione uncleben_
 
Last edited by a moderator:
Nani aliwahi kusema Lowassa ni mleta vurugu!? Aache kupindisha mambo. CCM na Watanzania kwa ujumla wetu tunasema Lowassa ni fisadi...Hilo la vurugu anajizushia yeye tu.

Hadi mtasema yoote ya mioyoni mwenu lkn lowasa ndiye rais kipenzi cha watanzania
 
Hapo kwenye red ni swali la muhimu sana, kuna amani gani iliyoonyesha dalili ya kutoweka ambayo lowassa aliilinda ndani ya hiyo miezi miwili?
Na kama toka akiwa sisiemu, kulikuwa na dalili za machafuko yoyote enzi hizo?
Je hao alioshindanishwa nao 'wamepigania' amani ktk maeneo yao kwa muda gani?

Nice reasoning
 
Inategemea Na Taasisi Zenyewe! Isijekuwa Zinaongozwa Na Watu Jamii Ya Gwajima Ambao Hawajui Tofauti Kati Ya Imani Ya Mungu Na Mahaba Ya Kisiasa Na Kimaslahi
 
Mkuu huko nimeshatoka nimewaachia Nyie werevu muendelee kuchanganua hoja ,Acha nihangaike na malofa na wapumbavu wenzangu

Umemjibu vyema.Hata vurugu na Mauaji ya Alphonce Mawazo yamefanywa na vijana wa CCM kwa jina LA Greenguard.Na hata Leo Mwenyekiti wa Kitongoji Mlangali anashikiliwa kwa tuhuma za kujeruhi na kupoteza kwa wanachama wawili wa upinzani, Na nani Ana vurugu???Mara nyingi ukinyoosha kidole basi vile vingi vinakuonyesha mwenyewe.

Hongera kwa kumpa ukweli wake.Aache Malofa na wapumbavu tuendelee na maisha yetu kuna siku watajutia ubaguzi wanaoufanya
 
Aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chadema na kuungwa mkono na Ukawa, Edward Lowassa amesema anashangaa kuona anaambiwa mleta vurugu wakati dunia inamkubali kuwa ni mlinzi wa amani.

Kauli ya Lowassa imekuja ikiwa ni siku moja baada ya taasisi za kidini 1,200 duniani kupitisha jina lake kwa ajili ya kumpatia Tuzo ya Amani.

?Nimepokea kwa unyenyekevu na furaha tuzo ya amani duniani ninayotarajiwa kupewa na taasisi za kidini 1200 duniani,? alisema Lowassa akinukuliwa na msemaji wake, Aboubakar Liongo.

Lowassa alisema tuzo hiyo ni kithibitisho cha uongo wa CCM na Serikali yake kuwa wapinzani ni watu wa vurugu.

Taasisi hizo katika kikao chake huko Bukavu DR Congo, zilitangaza kumpa tuzo hiyo Edward Lowassa kutokana na utulivu aliyouonyesha kabla na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba.

Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili, Amani na Haki za Binadamu Kwa jamii, Mchungaji William Mwamalanga ilisema kiasi wajumbe 1,400 wa mkutano huo kutoka kote duniani walikubaliana kumpa tuzo hiyo Lowassa kati ya wanasiasa 1,000 waliyoshindanishwa ili kumpata kiongozi bora wa Amani mwaka 2015, ambaye anajali na kuangalia maslahi ya jamii badala ya madaraka.

Alisema yeye ni muungwana na ana hofu ya Mungu na hata siku moja hatoweka mbele maslahi binafsi, na ndiyo maana aliwatuliza wananchi waliyokuwa wakimtaka kutoa tamko baada ya matokeo kutangazwa.

?Siko tayari kuingia Ikulu huku mikono yangu ikibubujika damu. Nashukuru taasisi hizo za kidini duniani, zimeliona hilo,? alisisitiza Lowassa.



Chanzo:
Mwananchi

Mzee hana jipya saiv
Amebaki kuwa mtu wa kusubiri misiba,
Vituzo ambavyo vilitakiwa kugombewa na wakina rais wa wasafi

Utashangaa amepewa hadi tuzo ya kilimanjaro music award maana n msanii mzuri tu

poor kibaraka lowasa
Endelea kupewa vtuzo na mabwana wa magharibi
 
Umemjibu vyema.Hata vurugu na Mauaji ya Alphonce Mawazo yamefanywa na vijana wa CCM kwa jina LA Greenguard.Na hata Leo Mwenyekiti wa Kitongoji Mlangali anashikiliwa kwa tuhuma za kujeruhi na kupoteza kwa wanachama wawili wa upinzani, Na nani Ana vurugu???Mara nyingi ukinyoosha kidole basi vile vingi vinakuonyesha mwenyewe.

Hongera kwa kumpa ukweli wake.Aache Malofa na wapumbavu tuendelee na maisha yetu kuna siku watajutia ubaguzi wanaoufanya

Mkuu sikua na namna nyingine ya Kumwelewesha nikaona mimi mpumbavu kushindana na mwerevu haitoleta maana ila labda akirudi kwenye senses zake ataelewa kwanini wameona ni vyema Lowasa kupewa tuzo hizo za amani ,ni logic raisi tu eti hoja yake kwanini wasipewe tuzo wanao suluhisha Migogoro kwenye nchi zenye machafuko ila apewe Lowasa ambaye yupo kwenye nchi isiyo na machafuko ,hivi ni mpaka tusibiri nchi iingie kwenye machafuko ndio tutafute amani ??? Haoni kwamba ilikua busara kwa Lowasa kutong'ang'ania madaraka na kusababisha kuchafuka kwa amani ambayo ndio tunu moja wapo Mungu aliotujalia watanzania
 
Kwa hali ya kawaida ya kihistoria kwa Lowasa kununua nunua watu wa kawaida, viongozi wa kisiasa na wakiroho si ajabu kabisa kutoa posa na baadae kulipa mahari kwako viongozi wa taasisi hizo. Lowasa tunamjua hanauwezo wa kujinadi kwa kutumia Sera tangu mwanzo yeye alianza miaka mingi akijidai baba wa misaada kwa makanisa na Miskiti mbalimbali Tanzania. Tumeliona hilo!!!! Tafta mbinu nyingine siyo Tuzo.
 
Back
Top Bottom