Wanalipwa na Chadema si unaona walitunga kuwa kamati kuu itakuwa Dodoma kukutana na wabunge wa Chadema? Lengo ilikuwa kuwatengenezea ulaji na wao watoke wakapunge upepo wa viyoyozi bungeni Dodoma lengo kuwasaidia Ku Steam out frustration zao kidogo.NIlichojifunza ni kuwa MTU aliyekuwa akikaa viti vya waheshimiwa Leo anakaa viti vya wageni ambavyo hata watoto wa shule hukalia wakienda kutembelea binge nawahurumia sumaye na lowasa wanadhalilisha hadhi ya uwaziri mkuu mstaafu.
Mawazo mgando. Kinachoumiza mioyo yenu ni kuwaona wako upande wa pili wakiijenga siasa ya vyama vingi. Ccm hakuna kinachowakera zaidi kama kumwona mtu, hasam mwenye umaarufu na ushawishi kwa watu, akichukua ”full responsibility" ktk ujenzi wa siasa za upinzani. Mtamtusi, mtamng'ong'a, mtatumia kila lugha mbaya dhidi yake ili tu adharauliwe na jamii. Mnasahau kuwa kila binadamu ana namna jamii inavyom value automatically. Ndiyo maana siasa zetu bado zimejaa visokorokwinyo.
Mara nyingi katika mabunge viongozi wastaafu au viongozi wa vyama vya siasa huudhuria bungeni kwa ajili ya mambo maalum,..Hotuba ya Raisi,Hotuba ya Bajeti, Hotuba ya hali ya Taifa (PM), Hotuba ya hali ya Taifa (KUB). Ukiona viongozi wa vyama vya siasa wanahudhuria kipindi cha maswali na majibu huku wakitumia fursa ya kutambulishwa kama propaganda ujue wamefika mwisho.
mara nyingi kipindi cha maswali na majibu kule kwenye sehemu ya wageni (gallery) hukaa wasaidizi wa mawaziri na wanafunzi wanaojifunza shughuli za bunge. Ninawaeleza washauri wa Lowassa na Sumaye kuwa mmechemka na mmewafanya 'maveterani' wenu kuwa wanasiasa wa rejareja.
Kama leo Lowassa,Sumaye na Ntagazwa (aliwahi kuwa Waziri wa nchi ofisi ya Rais) wanajifunza tena jinsi bunge linavyoendeshwa ni dhahiri wamekwisha. Cha kushangaza hadi wasomi Prof.Safari na Prof.Baregu nao wamefanya makosa makubwa ya kiufundi,tatizo ni picha? au kutokuelewa? au kupotoshwa?
Picha hii hapa chini ni dhahiri itakuonyesha kuwa wamejishusha kiwango,nini wanachojifunza ikiwa wamekaa bungeni miaka takribani 25? . Siku nyingine hudhurieni bungeni mambo makuu ya kimkakati kwa taifa kama Hotuba ya raisi,Bajeti,hotuba ya PM na hotuba ya KUB. Hili lisiachwe lipite ni lazima Mkuu wa Protokali na mambo ya Bunge Chadema, John Mrema awajibishwe...kawafanyia hujuma hawa maveterani,kawashusha,kawapa aibu, kawalinganisha na wanafunzi wa shule ya msingi wanaojifunza bunge.
Hayo mambo unayoyahoji ww n standings za bunge, constitutionally written au mawazo yako binafsi......??? Sina hakika kama ww unaweza kuwa unaifahamu protokali kuliko hao unaowazungumzia na hili n moja ya jambo linaloigharimu sana CCM kila mtu anajifanya anajua mambo na ana uwezo wa kuongea......... Ukoo wa kambale nyinyi, mwili tembo akili kisoda
Ungekuwa na open mind ungeweza kujua mleta mada ni mtu wa tabia gani.
Kwake kila akiamka jambo la kwanza ni Lowassa hili Lowassa lile. Kwake kumtaja ni kama mlo wa kwanza wa siku. Fungua akili mkuu ili utambue mambo
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.