Lowassa strikes back!

Lowassa strikes back!

Naona ameamua kutumia TBC1 kutaka kujisafisha wakati huu kuelekea uchaguzi!.
 
Nahisi kama zile tetesi kuwa EL atarudi kwenye kiti chake zinaanza kuniingia akilini.
Kwani kwa kulitambua hilo naona wadau wanaanza kujipendekeza.
 
Sielewi ni kwa nini Mwalimu hakupewa umri mrefu kama wa Mandela. Mungu huyu nae! Yote haya tunayoyashuhudia sasa yasingekuwepo.
 
Huu ni Msemo ambao Ndg Lowasa anadai anautumia na wananchi wake Huko Monduli!!!. Hivi ni kweli Muheshimiwa huyu anataka kuwaambia watanzanioa kuwa wananchi wa monduli ni wajinga kiasi cha kuimba nyimbo kama kasuku tu!! Hata kama unamuimbisha wimbo unaomtukana baba yake ni kweli atauimba tu!!. Watu toka Monduli tunaomba maoni yenu tafadhali!!.
 
Huyo ni mjanja either kuna sehemu ameambiwa atarudishwa ndani ya chama au nyadhifa furaniu atapewa na sasa anataka ajionyeshe kuwa yeye yupo na nina wasi wasi sana na wana CCM wengine wanajipendekeza sana kwa huyo mtu kwakuwa ana jeuri ya pesa anagalieni tu mtakuja jua kitakacho endelea
 
Kwa kweli si kila mwenye uwezo wa kuandika anapaswa kuandika hata mambo hasioyajua...huyu ni mmoja wapo.................1.Anadai hapa kuwa kuna mtu alikuwa anamlazimisha injinia manyanya apitishe memo???????????how mbunge anapitisha memo ya waziri mkuu kwa ujinga wake anadhani manyanya alikuwa ni mtendaji pale tanesco wakati wa tanesco,...........2Hajasikiliza sijui au hajaelewa maelezo kuwa ni kweli alipush mchakato uende kwa haraka kwa kuwa tishio la umeme ni kubwa lilikuwa na anaamini ulikuwa ni wajibu wake

Yaani points zako hazina "leg to stand on" matatizo ya umeme tunayo tangu enzi za mababu zetu....leo yeye lowassa ndo aliona eti tishio la umeme ni kubwa mpaka akaamua kufanya unilateral decision akipuuzia ushauri wa wataalamu...c'mon naona wewe uko kwenye pay list ya EL...the guy hanged himselft on the noose that he prepared....tuna viongozi wengi tu wazuri wa kutuongoza...he was good while he lasted.....apumuzike afanye biashara zake binafsi...he can be a successful businessman....ooh..sorry he IS a successful businessman
 
Huyo ni mjanja either kuna sehemu ameambiwa atarudishwa ndani ya chama au nyadhifa furaniu atapewa na sasa anataka ajionyeshe kuwa yeye yupo na nina wasi wasi sana na wana CCM wengine wanajipendekeza sana kwa huyo mtu kwakuwa ana jeuri ya pesa anagalieni tu mtakuja jua kitakacho endelea
Ni kweli kabisa, make anadai yeye si mtu wa kukaa ofisini na kusubiri mafaili tu, ni mtu wa kufanya maamuzi pasipokuogopa matokeo. Anajaribu kuwaaminisha watanzania kuwa yeye ni mtendaji kwelikweli ili akijakuteuliwa basi watu wasihoji sana. Lakini ukweli uko palepale, huyu bwana ni fisadi, Japo kuna hizi juhudi za kumsafisha ambazo zimekwisha anza.

Lakini ni vyema akatambua kuwa hata kama yeye ni mtendaji sana, si lazima yeye apate nafasi, kuna watu wengi ambao ni watendaji zaidi yake, ni kwamba hawajapata nafasi tu. Na kama yeye si fisadi na ni kiongozi muadilifu, basi atakuwa ni muumini wa uongozi wa kupokezana na hatohangaika kujisafisha ili aendelee kuwa kiongozi katika serikali!!.
 
Huyu jamaa anajiamini kwakuwa ana pesa za wizi na anacontrol kubwa sana kwa serikali na chama pia. Ingekuwa mchovumchovu asingejiaminisha hivi.... Let's see what will come :sick:
 
Thats pople politiks, kusema kile ambacho hakiko moyoni, upendo huo Sita kautoa wapi? Nchi hii bwana....
 
Nilikuwa nikifuatilia Mahojiano kati ya Tido Muhando na Waziri mkuuu aliyejiuzuru Ndg E.Lowasa. Nilichokiona nikuwa waziri mkuu alikuwa anajaribu kuwaaminisha watanzania kwamba yeye hakuhusika katika mkataba wa kifisadi wa Richmond!! Pamoja na ushahidi wote uliotolewa juu ya nafasi yake katika huo mkataba. Na akasema kuwa magazeti yaliandika habari nyingi za uongo kumhusu yeye mpaka mwisho watanzania wengi wakawachoka na kuwadharau!!!! Baada ya kugundua ni wazushi!!.Je!? Ni kweli watanzania wanaamini hivyo? Au muheshimiwa ndo anazidi kujichimbia shimo?


ni wazi si yote yanayosemwa yalikuwa ukweli kuhusu mkataba husika kwani ushabiki uliingia lakini kitendo cha mheshimiwa huyo kujiuzulu ni ushahidi kuwa alihusika vinginevyo angesimama na ukweli hadi mwisho lakini yeye akaamua kubwaga manyanga kama alivyotamka mwenyewe ikifuatiliwa na hatua za kujisafisha chamawise.
 
Wakati wengi hatukutarajia Lowasa kuteuliwa kushika nafasi ile ya tatu kwa ukubwa serikalini, Sitta yeye anashangaa kujiuzuru kwake. Kuna unafiki mwingi sana kwenye siasa za Tanzania! Nani aliruhusu na kuiunda Tume ile ya Bunge wakati TAKUKURU walishalimaliza suala lile?
 
Mi ninge furahi hata na Rais wa nchi angeachia ngazi, kwani ameshindwa kutekeleza ahadi alizo toa.
Umasikini umezidi, na hali mbaya imezidi kuonekana wazi wakati tukioneshwa takwimu za kugushi kuwa hali ya uchumi ni nzuri.
 
Hapo ndipo Lowassa anaponyimwa haki yake. Kwanini basi tume iliundwa?. Kwanini tume iliweza kuwaita na kuwatembelea wahusika wote wa nje na ndani ya Tanzania na kumwaacha Lowassa aliyekuwa na ofisi mtaa pili tu toka ofisi ya tume hiyo?.

Jamani, mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni.

Welldone Lowassa, kaza buti mpaka kieleweke.


Jamani kwani Ze Tume recommended for his resignation? or left the whole matter for him to reason and decide? nakumbuka kama alishauriwa KUPIMA maamuzi na uhusika wake kama PM juu ya sakata hilo wala hakushauriwa kujiuzulu!

Mzee wa watu akapima, mizani yake ikamuonesha KUJIUZULu akatwaa uamuzi huo kwa utashi wake wala siyo maelekezo ya Ze tume.
 
amakweli Samuel Sitta Ni MNAFIKI sasa nimeamini.Au ameanza kujipendekeza kwa kuwa inaelekea wazi Edo anaweza kurejea kwa kishindo!!!

ss acha unafiki.........leo kweli SS amekuwa mtu wa kumsikitikia Edo kujiuzulu??
 
Mkuu, siku hizi wanasema. Kidumu chama cha mapinduzi, na kuitika kidumu chama tawala. zile za enzi zetu wameshaacha. Usishangae hiyo ndiyo slogan mpya kwa ajili ya monduli tu.
 
Tido anaweza kumpa Lowassa airtime yote anayotaka! WATANZANIA TUMEAMKA HATUDANGANYIKI TENA. Viongozi wako wengi tu sasa hivi tuna kina Bilal na Shein ...mwendo mdundo. Achana nao CCM Masalia!
 
lowasa hatakiwi kabisa kuilaumua tume kwani hakuna hata sehemu moja tume ilisema ajiuzuru,tume ilimtaka apime mwenyewe na ndo alichokifanya.lowasa ni mtu wa kupiga deal tka zamamni,nyerere mwenyewe anamjua kwahiyo hata kama sio RICHMOND lowasa ni mtu wa deal tu wala asitake kutuambia kuwa yeye ni msafi hana lolote..yaani wakati anapiga deal ya RICHMOND akataka uchomeea deal nyingine ya kununua MVUA thailand,du we uliona wapi mvua inaunuliwa?kama do hivyo mungu hana kazi tena...Dr Msabaha nae mda si mrefu atasema ukweli maana lowasa ameanza kuwatupia mpira watu wengine.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom