Lowassa strikes back!

Lowassa strikes back!

Binafsi nimebahatika kuona interview ya Pinda na kwa kiasi alijitahidi kutumia lugha ya kidiplomasia has kuhusu msuala ya ndani ya bunge la swala la Kadhi lakini bahati mbaya nilishindwa kuvumilia kuona EL akihojiwa kwani alikuwa amejiamini kupita kiasi na nahisi rage is burning inside him.
Ningependa Mwaikembe au yoyote alikuwa katika kamati ile wafugue kopo tujue yote otherwise mtu huyu atatufanya watu wote tuonekane hatuna akili.
EL amependelea wafugaji kiasi ambacho Kilosa ya Kilimo imekuwa jangwa,hafai huyu.
 
Mtake msitake Lowassa ndiye Rais wetu 2010. Siyo kwamba ninampenda au nina mshaikia Mmasai huyu, La hasha, ila kulingana na Watanzania tulivyo mambumbumbu wa kusema TUTAKAYE PEWA NA CCM 2015 ambaye ni LOWASA tutampa Urais pamoja na UFISADI wake wote.
 
Mtake msitake Lowassa ndiye Rais wetu 2010. Siyo kwamba ninampenda au nina mshaikia Mmasai huyu, La hasha, ila kulingana na Watanzania tulivyo mambumbumbu wa kusema TUTAKAYE PEWA NA CCM 2015 ambaye ni LOWASA tutampa Urais pamoja na UFISADI wake wote.

Wanifanya nianze fikiria nini tatizo la Al Shabaab kule Somalia
 
Siamini kama el ana nafasi tena mioyoni mwa watz 2015 yupo sumaye, shibuda, magufuli, n.k. Ccm wasilogwe kufikiria kumpitisha huyu jamaa kuwania ngazi yoyote ya kitaifa
 
Hivi hii mijamaa shida yao ni nini??

Nashindwa kuielewa hii mijamaa, hivi nafsi zao haziwezi kutulia hadi waitwe wahishimiwa na kupewa madaraka ambayo hata hivo maendeleo HATUYAONI???..these people need the help of psychiatrist. Ndio maana wengine tunachukia siasa kwa sababu ya mijitu kama hii.
 
Nyerere aliwachapa bakora wale wanafunzi wa chuo kikuu ....kina marehemu peter bakilama..et al...waliosemaga ,HERI MKOLONI!!!!!!!

..SASA KAKA UNASEMA HERI ..UK...ITS LIKE SAYING HERI MKOLONI....huwezi kulinganisha uk na tanzania kwa vipimo vyovyote duniani...nitamuelewa mtanzania aliye kwenye nchi ya dunia ya tatu ie zambia ...akisema "heri huku"....

BoB MARLEY alisema.."emanticipate yourself from the mental slavery ...."

MtaNZANIa ukiwa Uk AU marekani huwezi kuwa bora kuliko aliye nyumbani.....hasa kwa wale ambao hata ukitokea msiba au sherehe angalau mara moja kwa mwaka wanashindwa kuja .....na atleast kuja likizo angalau mara moja kila baada ya miaka miwili....kama humudu hata kutuma senti nyumbani au kununua nyumba nyumbani...kusomesha nduguzo home...basi huna sababu ya kuwa ulaya ...na kusema "heri huku"

nawapongeza wana diaspora ambao ..kuwa kwa nje kunaleta faida kwa jamii yao na wanaweza kuwekeza nyumbani........tukiendelea hivyo nasisis tutakuwa na sababu ya kuwa ulaya ...kama wahindi ,wa israel,mexico au hata wakenya....ambao ...wana diaspora wanachangia sana kipato cha nchi.

Bob Hakuishia hapo tu, aliendelea "Non but Ourselvelves can FREE our minds"

Whaat you said is right..........
 
...........................Waziri mkuu ndiyo amefanya haya, Tumondolee Heshima au Tumuwajibishe.
Mh. Spika, Nimetafakari sana, Kwa niaba ya chama Changu, kwa niaba ya Serikali Yangu, Nimeamua kumuandikia Rais barua ya kumuomba niachie Ngazi(makofi) . Nafanya hivyo kwa moyo mweupe kabisa Ili kuonyesha dhana ya uwajibikaji lakini na Kutokukubaliana na utaratibu uliotumika kusema uongo ndani ya Bunge wa Kumsingizia mtu.................................................................................


Hayo yalikua maneno ya EL ................................
 
Kidatu.. unajua madaraka ya waziri mkuu kule Bungeni na nafasi yake? Kama hakutendewa haki alitakiwa kulazimisha haki itendeke kwake badala ya kuweka manyanga chini. Kwani alipigiwa kura ya kutokuwa na imani? Lowassa ni mzungumzaji mzuri angeweza kabisa kujenga hoja na kulaizmisha bunge lipige kura ya kuwa na imani naye au la hakufanya hivyo. Aliamua kuweka manyanga chini.

Lowassa alijionea mwenyewe na kujidhulumu mwenyewe. Jaribio lolote la kuhamisha lawama toka kwa Lowassa litashindwa kabla halijajaribiwa.

Kwanza tume ya Mwakembye haikumtaka Lowasa ajiuzulu, ama awajibishwe, ilimwambia apime uzito wa mambo, yeye kapima kaamua kujiuzulu, sasa nani alimuonea. Tume haikumtaja kama mtuhumiwa, yeye dhamiri yake ilikuwa inamla tu.
 
Hapo ndipo Lowassa anaponyimwa haki yake. Kwanini basi tume iliundwa?. Kwanini tume iliweza kuwaita na kuwatembelea wahusika wote wa nje na ndani ya Tanzania na kumwaacha Lowassa aliyekuwa na ofisi mtaa pili tu toka ofisi ya tume hiyo?.

Jamani, mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni.

Welldone Lowassa, kaza buti mpaka kieleweke.

It was a matter of methodology tu..................findings ni zile zile hata ukibadilisha methodology!
 
Nilikuwa nikifuatilia Mahojiano kati ya Tido Muhando na Waziri mkuuu aliyejiuzuru Ndg E.Lowasa. Nilichokiona nikuwa waziri mkuu alikuwa anajaribu kuwaaminisha watanzania kwamba yeye hakuhusika katika mkataba wa kifisadi wa Richmond!! Pamoja na ushahidi wote uliotolewa juu ya nafasi yake katika huo mkataba. Na akasema kuwa magazeti yaliandika habari nyingi za uongo kumhusu yeye mpaka mwisho watanzania wengi wakawachoka na kuwadharau!!!! Baada ya kugundua ni wazushi!!.Je!? Ni kweli watanzania wanaamini hivyo? Au muheshimiwa ndo anazidi kujichimbia shimo?
 
Wadau huyu mtu alipewa nafasi yakujitetea on the spot lakini aliishia kusema nimeonewa sana namedhalilishwa sana nakadhalika nakadhalika...... Sasa sisi tumueleweje? Huyu jamaa ni msanii kwa kweli. Lets wait! will see.
Hivi ndugu zangu huwa tunakuwa na kumbukumbu ya matukio au tunasikia third party???? au ndiyo kawaida yetu kuponda ponda tu ? Mimi ninakumbuka kuwa ile kamati ya kina Mwakyembe ilitoa taarifa yake bungeni na kutoa mapendekezo yake pale pale. Sasa hiyo nafasi ya kujitetea ilikuwa wapi? Mimi siyo mwanasiasa [i thank god for this]] Naye alisimama na akatoa maoni yake kuwa wahusika wote waliitwa na kuhojiwa na kamati lakini kama mtendaji mkuu hakuitwa kuhojiwa na hapo ndipo alipo sema kuwa kamati haikumtendea haki. Sasa kujitetea ajitetee vipi? Au mlitaka ajitetee baada ya kamati kuhitimisha taarifa yake????? .
Ninajua kwa kusema hivi mtaanza kunibandika label za kitoto lakini mfahamu kuwa JF ni mahala ambapo tunatakiwa tujadili hoja kimantiki na siyo kutumia hisia au chuki binafsi.
 
Hivi ni kipya gani alichosema ambacho hakuwahi kukisema? Kwa kweli sielewi kwa nini hii ni habari.

Lowassa si alishajitetea hapa?
 
Lakini huyo bwana mi naona amechanganyikiwa. Si mzima yule!!
 
Mwongo huyo....Watanzania wengi tunavipongeza vyombo vya habari kwa kutuhabarisha ufisadi wa fisadi yule namba wani Tanzania...big up vyombo vya habari...big up Kamati ya Mwakyenbe...it is too late kutafuta sympath ya watanzania...mwacheni mwizi aitwe mwizi..fisadi aitwe fisadi.
 
• Asema kujiuzulu kwake kulimuumiza

na Kulwa Karedia


amka2.gif

SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliyemaliza muda wake, Samuel Sitta, amesema alishtushwa na kuumizwa na uamuzi wa ghafla wa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, kujiuzulu.
Sitta alitoa kauli hiyo jana baada ya kutakiwa na gazeti hili kueleza ni jambo gani ambalo hatalisahau tangu alipoingia bungeni mwaka 2005 akiwa Spika wa Bunge.
“Moja ya mambo ambayo sitayasahau katika maisha ya uspika wangu ni kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, unajua ni mchapa kazi, alishtua wengi ambao hawakuuamini uamuzi ule,” alisema Sitta.
Kauli ya Sitta imekuja siku moja tu baada ya Lowassa kujitokeza hadharani na kueleza sababu ya yeye kuchukua uamuzi huo.
Akihojiwa na kituo cha Shirika la Habari Tanzania (TBC1) juzi usiku, alisema hulka yake ya kuwa tayari kuchukua maamuzi magumu pasipo kuhofia matokeo mabya ndiyo iliyomsukuma kushughulikia kwa ujasiri tatizo la mgawo wa umeme na sakata la Richmond, ambalo lilisababisha ajiuzulu.
Akizungumza na Tanzania Daima katika mahojiano maalumu kwa njia ya simu kutoka jimboni mwake, Urambo Mashariki, mkoani Tabora jana, Spika Sitta alisema siku hiyo hakuamini macho yake baada ya kuona Lowassa akilitangazia Bunge na taifa kuhusu uamuzi wake huo wa kuachia ngazi.
“Nakwambia tangu nimekuwa Spika wa Bunge mwaka 2005, nimepitia mambo mengi mno, lakini kubwa zaidi ambalo siwezi kulisahau ni siku ile aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, alipochukua uamuzi wa kutangaza kujiuzulu wadhifa wake, nilipatwa na mshangao, nilishtuka na sikuamini,” alisema Spika Sitta.
Lowassa alilazimika kujiuzulu wadhifa huo baada ya kuhusishwa na tuhuma za rushwa katika Kampuni ya kuzalisha umeme wa dharura ya Richmond mwaka 2007.
Spika Sitta alisema yeye aliamini kabisa katika kipindi hicho baada ya kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, sanjari na mtangulizi wake katika wizara hiyo, Dk. Ibrahim Msabaha, kungetosha serikali kuwajibika.
“Mimi siku ile nilipoona wale wadogo (mawaziri), wamewajibika, nilielewa wazi kwamba imetosha, lakini baada ya siku kadhaa zilizofuata, mheshimiwa Lowassa naye akajiuzulu, kwa kweli, niliona ni maamuzi magumu aliyochukua,
sikujisikia raha kabisa… kwa vile mimi nafsi yangu huwa haimtakii mtu mabaya,” alisema Spika Sitta.
Alipoulizwa mbali na tukio hilo, anakumbuka mambo gani mazito zaidi, Spika Sitta alisema ni mijadala motomoto iliyokuwa ikiwasilishwa na wabunge iliyosababisha akabiliane na changamoto nyingi.
“Unajua pale bungeni kila mbunge anastahili yake ya kuongea au kuuliza swali, wakati mwingine anaweza kuanza kwa methali… hapo unatakiwa kuwa makini kweli kuwasilikiza, nawashukuru wote kwa michango yao motomoto,” alisema Spika Sitta.
Alisema hata baada ya Mizengo Pinda kuteuliwa kushika wadhifa wake, waliendelea kushirikiana katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku bila tatizo.
“Baada ya Mheshimiwa Rais kumteua Mizengo Pinda, tumeweza kushirikiana vizuri katika utekelezaji wa majukumu yetu bila tatizo, haya ni mafanikio makubwa,” alisema Spika Sitta.
Kuhusu hali ya kisiasa jimboni mwake, Urambo Mashariki, Sitta alisema ni nzuri na ana matumaini ya kutetea kiti chake bila wasiwasi.
“Hivi sasa niko jimboni nasubiri kesho (leo), kuchukua fomu ya kuwania kiti cha ubunge… hali ya kisiasa ni nzuri, naamini nitatetea kiti changu vizuri, tumuombe Mungu,” alisema Spika Sitta.
Alisema hadi jana amesikia kuna wagombea wengine watano waliotangaza nia na leo wanatarajia kuchukua fomu ili kupambana naye kwenye kinyang’anyiro hicho. “Nasikia kuna wagombea wengine watano, lakini hawaonekani hapa, nitakutana nao huko huko,” alisema Spika Sitta. Kufuatia kujiuzulu kwa Lowassa, mawaziri wengine, Naziri Karamagi na aliyekuwa Waziri wa Afrika Mashariki, Dk. Ibrahim Msabaha nao waliachia ngazi, baada ya kuhusishwa na tuhuma za Kampuni ya Richmond.


h.sep3.gif


juu
blank.gif
 
Ni wakati wa kuelekeaa uchaguzii na wote kwa pamoja wanasukuma gurudumu moja (ccm)...kwa faida yao na familia zao.
 
A Quick question.
Hivi unaposikia neno FISADI kichwani mwako inakuja sura ya nani?
 
kila mtu ilimshutua kwani lowasa alikuwa anaonekana hashikiki,lakini cha muhimu kila mtu alifurahi kwa kuwajibika kwake
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom