Lowassa: Sina shaka na umaarufu wangu .

Lowassa: Sina shaka na umaarufu wangu .

Lowasa hana jipya yeye anaamini katika kugawa rushwa, kama wali na pilau! Yeye ajihoji kweli amelitendea haki taifa letu kuhusu rushwa? Hasa Richmond?
 
Lowasa bwana mzee kaanza kupagawa laana ya watoto wanaosomea chini laana ta mama zetu waokosa japo panaldo laana ya richimond imeanza kumtafuna sasa hvi anaropoka lolote mpaka wamasai sasa hawamwamin zaman alikuwa akienda huko wala hataji chadema sasa maji ya shingo anaona ndugu zake wameshaijua chadema sasa yeye anawambia mabaya ya cdm kaishiwa mzee hakujua kula na kipofu we kwa cku nasikia mzee arikuwa anakunja ml.150 wakati kuna shule haina mwalim hata1 mwache atapetape
 
Uwaziri Mkuu ulimshinda sasa analilia uraisi. Uwezo wa kuendesha nchi hawezi kuwa nao hata kidogo ndio sababu anataka kuununua kwa kutumia fedha alizotuibia kwa kupitia kampuni za richmond na mdogo wake dowans.

Umaarufu wake wa kuwa fisadi hauna tija yoyote kwa wananchi wa Tanzania na hata monduli kwenyewe ambako wamasai wanakufa njaa huku yeye akikesha makanisani akifanya kampeni.

Mkataba mmoja tu wa RICHMOND ulimshinda ataiweza Tanzania?Kama ni urais jamani huyu mtu akumbushwe kuwa TFF imeanza upya mchakato wa uchaguzi kwa maelekezo ya FIFA.
 
kwani akichomwa kisu kunani?! wameng'oa meno na kucha na kupiga risasi wangapi ili wao waendelee kuneemeka na familia zao? leo anaona kwake kisu kinauma! ajiulize moyoni mwake kisu alichochoma watanzania kwa muda mrefu kwa kuwaibia mali zao inakuwaje? yeye si mmoja tu, afadhali mmoja akipotea kwa ajili ya wengi kukombolewa, au anafikiri tumesahau mambo yake?
 
Ni vizuri ukawa maarufu baada ya kazi uliyofanya kuonekana, badala ya kutaka umaarufu kabla ya kuifanya hiyo kazi!!!!!
 
acha kumtaja mungu kwa roho yako mbaya.we kama hujui kutafuta pesa jinyonge.mnamzushia ufisadi bure mzee wa watu wakati jk ndo alimchafua kwa fitna yake
ni kazi sana kuukubali ukweli na hasa ikiwa mfereji wako wa maisha unapitia kwake endelea kuvuta pesa mabazo kiukweli hazikusaidii zaidi ya kukuongezea laana kwa kutetea ujinga.
tunatafuta pesa tena halali japo ndogo lakini inastarehe yake na sina muda wa kujipendekeza kwa mtu eti kisa viela vyake vichafu.
 
Ni kweli mkuu, Lowassa maarufu sana! Hata kwa Ufisadi pia ndiyo balaa!
 
hivi lowassa unajua sitakupa tena kura yangu?
utakuwa rais gani mwenye dharau na majigambo ya pesa ambazo umetuibia sisi wenyewe
hapa umenitoka, kweli hata ugombee urais na mgomba nitaweka pata kwenye mgomba.
 
Namkubali Lowassa lakini kwa kauli ya KUSEMA atakayewapa KURA CHADEMA itakuwa anamchoma (yeye) Lowassa kisu HUKO SASA NI KUWATISHA WANANCHI NA KUTAFUTA HURUMA ZA WANA WA MONDULI.
 
Kumbe monduli ni ya lowasa, sikulijua hilo. Naijua monduli ya sokoine tu. Nadhani muda wake wa kuaibika umefika si kaamua kutoka pangoni. Aendelee kutapanya fedha zake za ufisadi halafu asubiri presha na stroke baada ya matokeo. Usicheze na CDM utalungula. Mwenyekiti wenu mwenyewe anaiogopa sembuse nyie
 
Wana JF,

Vetting ya kumpata Rais wa Tanzania kwa mwaka wa 2015 inaanza kuonekana mapema na ilikuwa kama ilivyoonekana kwa Wakenya

Wakenya wengi sana kabla ya uchaguzi walionekana kuwaunga mkono ODM na Raila wao lakini kilichotokea hata sisi ni mashahidi kuwa ule mfumo wa Serikali ukampatia kijiti Bw Kenyatta

Watanzania like wise wanaonekana kumuungana sana mkono Bw Lowassa na hata yeye mwenyewe anaonekana anaupenda sana Urais kuliko kitu chochoote lakini kwa hali ilivyo mfumo utampatia kijiti hicho Bw Membe, Mfumo huo huo ndio utakaomnyamazisha Bw Lowassa kuwa atulie Rais ( mwaka huo ) 2016 afanye kazi zake !

Hiyo ndio hali halisi..... Bw Lowassa hawezi kuwa Rais mwaka 2016 kwani pia kuna minongono huko kwenye viunga vya ofisi za serikali kuwa jamaa anaumwa ugonjwa wa kansa ya kibofu cha mkojo ( hii ni minongono tu ) haijawa confirmed !

The Fixer,

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Lowasa mzee wa makampuni feki..........atakuwa rais wa mabwege
 
Back
Top Bottom