Lowassa: Sina shaka na umaarufu wangu .

Lowassa: Sina shaka na umaarufu wangu .

Membe,magufuli,mwakyembe,6 ndo kaburi la ccm
Hili kundi likitoswa kwenye uteuzi wa mgombea urais 2015 linaenda ADC, na hapo ndipo patachimbika. CDM watachukua nchi kiulaini kama wanamsukuma mlevi.
 
Duh!hata wewe........kuna mtu alikuwa anaombewa na kutolewa pepo kanisani na kati kati ya wale waombaji alikuwepo dada mmoja naye akikemea kwa sauti ya juu ndipo yule pepo alimgeukia na kumuuliza hata wewe unanikemea.......nashangazwa na lowasa badala ya kujitakatisha ananyooshea wenzake vidole.....toa boriti kwanza ndani ya jicho lako mzee.
 
Huyu fisadi na yeye sasa ameanza kuweweseka baada ya kusikia kuna makundi mengine ya urais ndani ya ccm yameanza kujipambannua. Atulie anyolewe
Anashangaza sana maana kampeni za udiwani si level yake.
 
binafsi simkubali mtu huyu kama ni dhambi MUNGU anisamehe, lakini inavyoonekana ccm hawana mtu mwingine zaidi yake kama wanabisha wamtaje ( kibaya zaidi wanachoangalia zaidi ni fedha zake ndizo wanazozifikiria )
anangufu kwa kuwa ana mali ambazo sisi wadanganyika hatujawahi hata kuhoji amezipataje.
lakini naamini MUNGU atafanya kitu siamini kama ataendelea kutuacha tunyanyasike.

acha kumtaja mungu kwa roho yako mbaya.we kama hujui kutafuta pesa jinyonge.mnamzushia ufisadi bure mzee wa watu wakati jk ndo alimchafua kwa fitna yake
 
Mamvi simwelewi.alipewa uwaziri mkuu ukamshinda.sasa anataka urais !!!!duh.anjiamini nini?HASARA ALIYOTUPA KWENYE RICHMOND HAIELEZEKI.UCHUMI ULIPATA BLOW KUBWA SANA.
 
Mbona umaarufu wake haukumusaidia Mkwewe Sioyi Sumary kule Arumeru!

Tatizo la Tanzania ukiwa FISADI ukuwa "MAARUFU" badala ya kuwa BEHIND BARS! Maajabu ya Tanzania hayatakaa yaishe kama CCM itaendelea kututawala.

Ati Mwizi anajisifia kuwa celebrity!Shame....!
 
Mnaanza kumponda sasa wakati huwa mnamsifiaaaa kisa eti ni wa Arusha!! Shee!

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Duh!hata wewe........kuna mtu alikuwa anaombewa na kutolewa pepo kanisani na kati kati ya wale waombaji alikuwepo dada mmoja naye akikemea kwa sauti ya juu ndipo yule pepo alimgeukia na kumuuliza hata wewe unanikemea.......nashangazwa na lowasa badala ya kujitakatisha ananyooshea wenzake vidole.....toa boriti kwanza ndani ya jicho lako mzee.
Kwani yeye amechochea vurugu? Yeye ni mwizi tu wa Richmond na hao anaowasema wao ni vurugu sasa kichaa na mwendawazimu lao moja


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
lowassa: Sina shaka na umaarufu wangu .


Jumanne, mei 28, 2013 03:41 na eliya mbonea, monduli
.

Mbunge wa monduli na waziri mkuu mstaafu, edward lowassa, amesema hana shaka na umaarufu wake monduli wala tanzania kwa ujumla. Kauli hiyo aliitoa mjini hapa jana wakati akifungua kampeni za udiwani wa kata ya makuyuni huku akikishangaa chama cha demokrasia na maendeleo (chadema) kwa kupeleka mgombea wake katika kata hiyo.
“eti hawa wanathubutu kujinadi na kujigamba kushinda udiwani monduli ya lowassa wakisema watapata kura kwa asilimia 90 jamani haya ni kweli,” alihoji lowassa na kuongeza:

“ndugu zangu sina shaka na umaarufu wangu monduli wala tanzania.”

katika mkutano huo, aliwaambia wananchi kwamba anahitaji kuona wakikiadhibu chadema kwa kukipa pigo ambalo hawajawahi kulipata mahali popote nchini.

“ndugu zangu atakayewapa kura hawa chadema wana wa makuyuni atakuwa amenichoma kisu mimi, naomba msiwape kura hata moja, naomba muwafundishe adabu,” alisema lowassa.

Akikishambulia chama hicho kwa kutumia helikopta katika kata hiyo, alisema siku zote vita vya kiafrika vinapiganwa kwa kutumia askari wa miguu na si helikopita.

Alisema ccm inatumia askari wa miguu kuhakikisha inashinda vita vyake, hivyo haitatishika na helikopita hiyo.

Alikirushia kombora chama hicho kwa kukitaka kisimame hadharani na kujipapanua kama hakihusiki na vurugu

zinazoendelea nchini.

Alisema kama kweli hakihusiki na vurugu zilizopo nchini basi viongozi hao wanapaswa kujihoji ndani ya nafsi zao kama kweli hawahusiki.

“nawaomba hawa chadema wajihoji ndani ya nafsi zao kama kweli hawahusiki na vurugu hizi, je wanaifanyia nchi yetu mema au mabaya,” alihoji lowassa.

naomba nikusahihishe kidogo, lowassa sio waziri mkuu mstaafu, ni waziri mkuu aliyejiuzulu kutokana na kumiliki kampuni hewa ya richmond, iliyojizolea mamilioni ya shilingi kwa siku.lowassa ni mwizi, fisadi papa.hata aibe matrilioni ya pesa bado hatosheki.lowassa hasafishiki hata kwa blich!
 
lakini kwake yeye diwani akipatikana kutoka CCM Alafu Akanyimwa urais atakua na faida gani?
 
Uwaziri Mkuu ulimshinda sasa analilia uraisi. Uwezo wa kuendesha nchi hawezi kuwa nao hata kidogo ndio sababu anataka kuununua kwa kutumia fedha alizotuibia kwa kupitia kampuni za richmond na mdogo wake dowans.

Umaarufu wake wa kuwa fisadi hauna tija yoyote kwa wananchi wa Tanzania na hata monduli kwenyewe ambako wamasai wanakufa njaa huku yeye akikesha makanisani akifanya kampeni.
 
Back
Top Bottom