Nguno Buchenja
Senior Member
- May 3, 2012
- 149
- 59
Huyu mgombea wa CDM amegeuka mtu wa vurugu, mbona kwenye kura za awali akiwa CCM walimpigia kura wanachama wa CCM mpaka akaongoza kwa kuwaacha mbali wagombea wenzake wa CCM kabla jina lake halijakatwa katika ngazi ya mkoa, na ndipo akaamua kutafuta kuwatumikia wananchi kupitia chama kingine?, Au kuna ajenda nyingine imejificha ambayo haijajulikana. Vurugu zinazotumiwa na kutajwa kwenye kampeni ya Udiwani Makuyuni wilayani Monduli kwamba zinafanywa na CHADEMA mwenye ushahidi awatajie watanzania kwamba zilitokea kijiji gani wilayani Monduli, au ni kutaka kuwatisha wananchi wanaochukuliwa hawajui chochote, kama kipindi kile cha uchaguzi mkuu ambapo mikanda ya picha za vita ya Kimbari nchini Rwanda zilikuwa zinaonyeshwa vijijini kuwatisha wananchi maskini ambao hawana uwezo wa kufuatilia habari kila wakati kutokana na mazingira magumu ya upatikanaji wa mawasiliano wanakoishiambalo si kosa lao bali la mfumo, ambalo limewageuza kichaka cha kujipatia kura kwa kuwatisha kwamba wakichagua mtu mwingine maisha yao yatavurugika, wakati wanojidai wanawajali ndio hao hao wanawageuza ngazi ya wao kuneemeka.
Bado kuna kipindi kigumu kwa sababu wanaoambiwa wasichome visu viongozi(matajiri)wao ndio miili imejaa madonda ya visu vya kunyimwa haki zao.
Bado kuna kipindi kigumu kwa sababu wanaoambiwa wasichome visu viongozi(matajiri)wao ndio miili imejaa madonda ya visu vya kunyimwa haki zao.