Lowassa ni pasua kichwa

Lowassa ni pasua kichwa

Hivi wanapofika 450 wanaotakiwa hawezi kusimamisha zoezi mpaka awasumbue hao wote? Mbona anaanza kukiuka kanuni kungali mapema hivi? Hiyo ni dalili mbaya. Ni sawa na mtu anayejua uwezo wake wa kula nyama choma ni nusu kilo lakini kwa sababu mwenyeji anampenda hivyo akiweka kilo tano mezani lazima ale zote. Ni ulafi tuu.

Ndio kampeni hizo mkuu! We hujaelewa tu? Wanahisi muda wa kampeni utakua mdogo, ni ujanja tu wanaoutumia kuwalaghai wananchi.
 
Walimtuhumu kwa makosa wasiyokuwa na uhhakika kama ilivyo ESCROW,wakaamua kujirusha kumbe wanajichafua wenyewe kimaadili sasa leo wanaumbuka mmoja baada ya mwingine.
Mh.Lowasa ndio kiongozi pekee asiyekuwa na mchepuko na ndio mwenye familia iliyotulia.
Mkuu anatuhumiwa kwa yule mama aliye mfungilia lema shauri la pingamizi la ubunge.
 
Kajiandikisheni ili wakati utakapofika tufanye maamuzi magumu na muhimu kuisambaratisha ccm
 
Mambo ya Nyerere yameshapitwa na wakati Lowasa ndio rais ajae wa Tanzania
Vivyo hivyo Nyerere alipotutahadharisha kuwa JK alikuwa bado mdogo, ilipofika 2005 tukasema mambo ya Nyerere yameishapitwa na wakati. Kila mbongo aliye na akili timamu ameshuhudia tuliyoambulia katika kipindi cha miaka kumi iliyopita. Sisi tuliishia kuchukua maana ya juu ya neno udogo kiumri kumbe JKN alikuwa anawajua vizuri sana hulka za hawa viumbe. Haya tuendelee na mambo ya Nyerere yamepitwa na wakati...
 
Back
Top Bottom