VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Ukimtazama na kumsikiliza Edward Ngoyai Lowassa unaweza kunibishia. Ukimtazama na kumsikiliza tena Lowassa utaniamini. Ukimtazama na kumsikiliza Lowassa kwa mara ya tatu, hutatamani kumtazama na hata kumsikiliza mara nyingine. Ni msanii kwelikweli. Lowassa anajipambanua kama dawa ya umaskini wa Tanzania. Ameshindwa vibaya kuuondoa umaskini wa Monduli tu aliyoiongoza kwa miaka 25 kama Mbunge.
Lowassa anapokaririwa akisema kuwa ndani ya CC na NEC hakuna wa kukata jina lake unaweza kumuamini. Anajichora kama mpambanaji na shujaa hasa. Anajichora kama mwenye misuli imara chamani na asiyezuilika. Mtazame tena Lowassa na utabadili mtazamo wako. Lowassa amejaa woga na kutojiamini. Ndiyo maana anashtukiashtukia. Anacheza filamu ya takwimu wakati wenzake wamesharejesha fomu na fomu zimeanza kuchambuliwa! Ameshindwa mapema.
Kulipokuwa na fukuto la ufisadi katika Jengo jipya la UVCCM, Lowassa aliingia kwenye mpambano na Nape Nnauye. Lowassa akiwa Waziri Mwandamizi Serikalini na mmoja wa wanabodi ya Udhamini ya UVCCM,Nape alikuwa kijana mdogo na mchanga ndani ya UVCCM. Nape alimpeleka puta Lowassa na kumlaza macho. Lowassa, kwa sisi wachambuzi,alishindwa na Nape.
Mwaka 2008, Lowassa aliingia tena ulingoni kupambana na Dr.Harrison Mwakyembe akiwa na Kamati yake teule ya Richmond. Hapa Lowassa alipigwa KO na kuishia kulalama na kulialia kutafuta huruma. Akasingizia kuwa Uwaziri Mkuu ndiyo uliolengwa. Angekuwa mpambanaji angepambana. Hata PM Pinda anamzidi. Pinda amebaki imara pamoja na Operesheni Tokomeza, Operesheni Kimbunga na Escrow.
Kwenye uchaguzi mdogo Arumeru Mashariki (baada ya kifo cha Hayati Jeremiah Sumari), Lowassa alipanda tena ulingoni. Safari hii alikuwa kichama zaidi. Aliongoza kampeni za mgombea wa CCM na pia ni mkwewe, Sioyi Sumari. Akiwa katika uwanja wa nyumbani-karibu kabisa na Monduli, Lowassa aligaragazwa na kijana wa miaka 25 toka CHADEMA,Joshua Nassari aka Dogo Janja.
Sitaki kutaja kushindwa kwake kununua mvua za kutengeneza Thailand na hata Shule za Kata. Nataka mumtazame na kumsikiliza tena Lowassa halafu mshuhudie usanii wa mtangaza nia huyu. Chamani, Lowassa ni mwepesi na ameshazoea kushindwa. Hana upekee wowote na atayapokea matokeo yoyote Julai 12.
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam.
Lowassa anapokaririwa akisema kuwa ndani ya CC na NEC hakuna wa kukata jina lake unaweza kumuamini. Anajichora kama mpambanaji na shujaa hasa. Anajichora kama mwenye misuli imara chamani na asiyezuilika. Mtazame tena Lowassa na utabadili mtazamo wako. Lowassa amejaa woga na kutojiamini. Ndiyo maana anashtukiashtukia. Anacheza filamu ya takwimu wakati wenzake wamesharejesha fomu na fomu zimeanza kuchambuliwa! Ameshindwa mapema.
Kulipokuwa na fukuto la ufisadi katika Jengo jipya la UVCCM, Lowassa aliingia kwenye mpambano na Nape Nnauye. Lowassa akiwa Waziri Mwandamizi Serikalini na mmoja wa wanabodi ya Udhamini ya UVCCM,Nape alikuwa kijana mdogo na mchanga ndani ya UVCCM. Nape alimpeleka puta Lowassa na kumlaza macho. Lowassa, kwa sisi wachambuzi,alishindwa na Nape.
Mwaka 2008, Lowassa aliingia tena ulingoni kupambana na Dr.Harrison Mwakyembe akiwa na Kamati yake teule ya Richmond. Hapa Lowassa alipigwa KO na kuishia kulalama na kulialia kutafuta huruma. Akasingizia kuwa Uwaziri Mkuu ndiyo uliolengwa. Angekuwa mpambanaji angepambana. Hata PM Pinda anamzidi. Pinda amebaki imara pamoja na Operesheni Tokomeza, Operesheni Kimbunga na Escrow.
Kwenye uchaguzi mdogo Arumeru Mashariki (baada ya kifo cha Hayati Jeremiah Sumari), Lowassa alipanda tena ulingoni. Safari hii alikuwa kichama zaidi. Aliongoza kampeni za mgombea wa CCM na pia ni mkwewe, Sioyi Sumari. Akiwa katika uwanja wa nyumbani-karibu kabisa na Monduli, Lowassa aligaragazwa na kijana wa miaka 25 toka CHADEMA,Joshua Nassari aka Dogo Janja.
Sitaki kutaja kushindwa kwake kununua mvua za kutengeneza Thailand na hata Shule za Kata. Nataka mumtazame na kumsikiliza tena Lowassa halafu mshuhudie usanii wa mtangaza nia huyu. Chamani, Lowassa ni mwepesi na ameshazoea kushindwa. Hana upekee wowote na atayapokea matokeo yoyote Julai 12.
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam.