mwashambwa wakwetu
New Member
- Jul 16, 2015
- 3
- 1
100 digits kwani hapo kwenye post yangu kuna mahali popote nilipomtaja Lowassa?
Nilichosema mimi ni kuwa baadhi ya watia nia martumizi yao kwenye hiyo kuisaka Ikulu ndiko kuna utata mkubwa.
Hebu tujiulize swali moja tu, hivi inwezekanaje mtia nia ambaye chama chake kimemuelekeza atafute wadhamini 450 kutoka mikoa 15, yeye anaenda zoa 'rundo' la wadhamini/wapiga kura wake 800,000 plus kutoka mikoa yote 31?
Hivi alikuwa na maana gani kukiuka kwa makusudi maelekezo ya chama chake?
Tutaendelea kukumbuka maneno ya busara sana aliyowahi kuyatoa Mwalimu Nyerere, aliposema Ikulu kuna biashara gani hadi mtu atumie mabilioni ya pesa zake 'kuinvest' kwenda huko?
Akaendelea kuuliza kama huyo mtu ameyakopa mabilioni hayo[Lowassa ametwambia anapewa na rafiki zake] atawezaje kuyalipa wakati Ikulu hakuna biashara yoyote?
Akamalizia wosia wake muhimu sana kwa Taifa hili kuwa mtu huyo ni wa kumuogopa zaidi ya UKOMA.
mfa maji siku zote haishi kutapatapa,ukishindana na mjinga utaonekana mjinga nawe,ukijibu mashambulizi ya chizi hasa maneno mabaya anayokutamkia we mwenyewe utaonekana chizi;kuna nguvu ya ushindi katika kunyamaza.yesu alipoitwa belzebul means mkuu wa mapepo hakupoteza mda kujisafisha bali kunyamaza na kuendelea na kazi aliyotumwa.endelea kunyamaza mzee el utashinda asubuhi