Kamwe Lowassa hawezi kuwa kama Zuma kwa sababu nyingi tu na chache kati ya hizo ni hiziz:
1. Hana support yoyote toka kwa wafanyakazi wa nchi hii ambao kwa SA ndiy walikuwa instrumental katika kumnyanyua Zuma;
2. Zuma alikuwa na eloquence ya hali ya juu na alishuka mpaka kwa watu wa kawaida na vijana ambao ndiy walikuwa chachu ya ushindi wake. By the way huyu wa kwetu hapa amewahi hata kufanya mahojiano na vyombo vya habari vya kimataifa kama BBC, Sauti ya Ujerumani au hata VOA? kwa lugha gani?;
3. Mbeki alionekana kama mtu ambaye anajali maslahi ya matajiri na watu weupe na kuwaacha watu weusi na wala wa kima cha chini (kwa hapa kwetu sifa hizi za Mbeki ndizo za Lowassa);
4. Zuma alikuwa na constituency, kwa maana ya kwamba alikuwa ni 'undisputed king' wa wazulu na hao walimpa boost kubwa hasa kwa vile ndilo kabila kubwa kuliko yote. Huyu bwana hapa kwetu hata hao wamasai wenyewe wamem-disown wakidai ni mmeru na hata wangemuunga mkono, hawatoshi kumpa jeuri.
5. Kwa ujumla uungwaji mkono wa huyu bwana umebaki kwa wenye njaa wachache wanaoingia kwenye vikao vya chama na wengine sasa wameanza kumgundua na kuchoshwa na hila zake za hujuma na kiu yake ya kuutaka urais.