Pasco, asante kwa ufafanuzi, najizuiya kuingia kwenye mjadala huu lakini nashindwa, Pasco, ni kweli toba ni ya moyoni kana imani ilivyo ya moyoni! ila huwezi ukaniibia gari leo halafu ukajifanya husikii nikilalamika nimeibiwa gari, halafu ukaenda Kanisani kutubu... na baada ya kutubu siku inayofuata ukaanza kulitumia gari ulilyoniibia, je hiyo toba ni sawa???? eti Pasco ..... heee, si unaona eee!!
Au labda kwa makosa nimehisi kama jirani yangu umeniibia gari, kumbuka tulikuwa marafiki sana, nikakutuhumu umeniibia halafu ukaaa kimya na uhusiano wangu na wewe haujarudi kwa sababu nimehisi umeniibia..... jee, hutakuwa na hatia kwangu kwa kukaa kimya na mimi kuendelea kukutuhumu? huoni kwamba unasababisha nenendelee kuwa na hisia mbaya juu yako nikamkosea Mwokozi Yesu kwa ajili yako? huoni pia kuwa kwa kutotaka suluhu, kwa wewe tu kufungua kinywa chako na kusema nami tukarudia urafuki wetu, as far hakuna aliye mkamilifu chini ya mbingu tukaendea na urafiki na kuwa wamoja kama Mwokozi alivyo tuombea!!?
Pasco, be frank, alipaswa kutolea ufafanuzi siku nyingi eti atasema sikupewa nafasi ya kujitetea, wakati tangu ajiuzulu ni Miaka 4 sasa, au alitaka tumpe nafasi gani? na alisha sema atalitolea ufafanuzi muda muafaka.... mpaka atakapo tolea ufafanuzi na wanachi wakaridhika WaTZ bado hawana amani na mtu huyu!!!! na mm sina Amani naye hata kidogo.
Pasco hata mini ni wa Kaskazini na ni Mkatoliki pia, lakini kwa staili hii ni bora kutopata Raisi wa namna hii millele kutoka kaskazini! ( na huu Pasco ni ubaguzi kusema hivi) kwani kascazini kuna nini, kwani wengine sio waTZ? acha hizo mkuu!!!