Lowassa na siasa za makanisani?

Lowassa na siasa za makanisani?

Hizi ni mbinu zake tu za kutafuta kujisafisha, atangaze basi na kutowania urais mwaka 2015. Huyu ni mtu mwenye tamaa sana ya madaraka. Angekuwa mtu wa kupima na akiongozwa na busara angeweza sema, mimi uwaziri mkuu ulinishinda je urais itakuwaje? kwani kuna ulazima wowote wa yeye kuwa rais? tujiulize watanzania huyu mtu anapigania kuingia ikulu anataka akafanye nini hasa? Jamani mheshimiwa Lowasa kama unapitiaga JF, tafadhali pumzika ufanye shughuli zako zingine urais uwaachie wengine wanaoweza, sisi kuja kusikia tena mambo ya Richmond hatutaki tena, tumechoka. Watanzania tuliwaamini sana nyie ( wewe, rafiki yako Jk na maswaiba wenu) mlichoifanyia Tanzania mnakijua wenyewe. Sisi leo tunataabika, mambo yako hovyohovyo, hatutaki tena mturudishe huko jamani, kundi lenu haliwezi kuongoza nchi hii. waachie wengine.
Huo ushuhuda anaoenda kutoa ni kukufuru tu kama kweli yeye ni Mkristo anajua, kama atatubu kuwa ni kweli aliingilia mchakato wa Richmond na kuitumbukiza nchi kwenye hasara, mimi nitampongeza na watanzania wanaweza kumsamehe.
Ahsanteni wana sana.
 
Jamaa anaweweseka sana na anadhani kwamba kumwaga goodies kwenye nyumba za ibada na hata kwenye taasisi za dini (alifanya hivyo hata kwenye kituo cha kiislam) kutamsaidia. Lowassa ajue tatizo lake la msingi. Kwanza ni mchafu wa maadili na utakaso wake hauwezi kuwa kwenye nyumba za ibada. Pili huyu bwana ni mtu wa visasi na mifano iko mingi. Tatu ni kwamba hata uwezo wake wa kazi, uelewa wake wa issues za uongozi ndani na nje ni mdogo na pengine hiyo ina uhusiano masomo yake huko chuo kikuu.
 
Lowasa akienda kama muumini kuna matatizo gani?kama anautaka urais hii ni haki yake ya kikkatiba wasimzuie wala kumbuguzi kwani anayo haki ka watanzania wengine,ila mwisho wa siku sisi wananchi ndio tutamhukumu kwani hakuna hasie mfahamu eidha kwa sikia au kusoma habari zake,inaboa sana watanzania tunavyoangaika na huyu bwana kana kwamba yeye malaika au mungu mtu,washauli wake wakisiasa wamshauli vizuri kwanii mwisho wa siku isijekuandikwa historia nyingine kwani watanzania sio wale wa miaka ile ya zama ujinga.hawadanganyiki tena wanajua kipi mavi na keki.ushauli wangu kwa watanzania tumwache aangaike anavyoweza ila sisi ndio wenye veto.hasitusumbue kichwa.naomba kuwasilisha
 
Lowasa akienda kama muumini kuna matatizo gani?kama anautaka urais hii ni haki yake ya kikkatiba wasimzuie wala kumbuguzi kwani anayo haki ka watanzania wengine,ila mwisho wa siku sisi wananchi ndio tutamhukumu kwani hakuna hasie mfahamu eidha kwa sikia au kusoma habari zake,inaboa sana watanzania tunavyoangaika na huyu bwana kana kwamba yeye malaika au mungu mtu,washauli wake wakisiasa wamshauli vizuri kwanii mwisho wa siku isijekuandikwa historia nyingine kwani watanzania sio wale wa miaka ile ya zama ujinga.hawadanganyiki tena wanajua kipi mavi nakeki.ushauli wangu kwa watanzania tumwache aangaike anavyoweza ila sisi ndio wenye veto.hasitusumbue kichwa.naomba kuwasilisha

tukiendelea kumuongelea na akapitishwa na CCM basi kura yangu, yako na nyingine nyingi hazitomzuia huyu jamaa.Dola yote na tume ya uchaguzi iko CCM, yeyote atayepitishwa na CCM ana kura mil kadhaa za hapana zitageuzwa ndiyo, haya mawazo ya kujiliwaza eti kura zitafanya kazi kumzuia mtu wa ccm, labda upinzani wapate 80% hii figure itakua ngumu sana kuichakachua
 
unafiki mtupu, walishalishana kiapo na jk cha kuachiana uprezidoo sasa anataka kutupiga changa la macho. Alienda Naigeria kutafuta nini kama si kuwazuru wenzake anaowaona watamsumbua sana 2015 akina mwakyembe, mwandosya na sasa zito kabwe
 
mshahara wa ni mauti,japo lowasa labda anania ya kuungama na kutubu kwa mungu, bado nivigumu kuaminika kwa jamii ya kitanzania mi naona angeachana siasa akawa mchungaji angepata heshima kwa jamii ya watanzania na kwa mungu pia
 
tukiendelea kumuongelea na akapitishwa na CCM basi kura yangu, yako na nyingine nyingi hazitomzuia huyu jamaa.Dola yote na tume ya uchaguzi iko CCM, yeyote atayepitishwa na CCM ana kura mil kadhaa za hapana zitageuzwa ndiyo, haya mawazo ya kujiliwaza eti kura zitafanya kazi kumzuia mtu wa ccm, labda upinzani wapate 80% hii figure itakua ngumu sana kuichakachua

Jamani,kama huyu mtu ni mchafu sana kiasi kila siku lazima tumuongelee,si bora tumuache agombee urais 2015 ili upinzani (Dkt Slaa,Prof Lipumba nk) waje kumshinda ki ulaini?. Akija kugombea mtu msafi upande wa CCM si ndio upinzani tutapata shida kuiondoa CCM. Au kuna agenda nyingine behind?. Tuwekane wazi hapa jamvini. Manake mnaomsema kila siku mwisho mtahalalisha kwake ile methali inayosema:MTI WENYE MATUNDA MATAMU NDIO SIKU ZOTE HUPOPOLEWA MAWE!
 
hapa hakuna harambee wewe kama hufahamu kaa kimya unazani watu hatujui.
Lowasa anawahonga viongozi wa dini ili wamualike aende kujisafisha na kwa mujibu wa maandiko hiyo unayoiita sadaka ni ubatili
wewe usiyeyajua nakupa pole sana na ni mwingoni mwa watu wajinga katika tanzania hii ambao hadi leo wanajua nyerere bado ni raisi
pole sana tena sana kwani unatembea ukiwa uchi ukiwa ujijui kama upo uchi unadhani umevaa


Wewe unamatatizo kama sio ya akili basi,ni agent wa Shetani,werwe ni nani hata uamue nani amchangi Mungu na nani asuimchangie,koma kabisa na ushetani wako huu,unaleta siasa kwa Mungu,MUNGU ANAWAHITAJI WATU WOTE UKIWAMO WEWE HATA KAMA NI MZINZI
 
Habari za uvumi toka Ar zinasema ex mp wa tz awamu ya 4a alionekana jana kanisani kwa Ngurumo akiwa na bible plas tenzi za rohoni.EL alionekana akiwa viti vya mbele pia alisikika zaidi wakati wa mapambio kushinda wenzake.Pambio lenyewe lilimbwa Sitarudi tena Misri naenda kanani.Baadaye alionekana akiongozwa sala ya toba huku akitoa ahadi jpili ijayo atatoa ushuhuda wa kufedheheshwa sana kuaibishwa sana kusemwa sana.na pia atajiunga na kwaya ya wazee na atakuwa mweka hazina.JE MWANA JF HILI LIMEKAAJE
..........upupu huu ndugu hatuwezi kuusemea
 
Kumrudia Mungu hawezi kuzuiwa ila kama anatubu pia awaombe msamaha watanzania kwa yale aliowanyia watanzania.tuwe wakweli na wala tusiwe vibaraka.ukweli unajulikana yote EL aliotufanyia watanzania
 
Mbona Rostam alishawahi kualikwa kwenye harambee kanisani pamoja na yeye kuwa Muislam na isitoshe Fisadi? Acheni chuki binafsi.

Watanzania hakuna akili hata moja, kama mnachagua mtu kwa kuangalia sura, akimwaga hela mtakataaa? hakuna watu nyanya kama watanzania. Mimi na familia yangu tutampa kura hiyo haina ubishi endeleeni na ho mahandsome wenu!
 
*********************
Source: TANZANIA DAIMA
Date=TODAY
Page. 06
*********************

Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa, anatarajiwa kuongoza harambee ya kuchangisha zaidi ya shs. millioni 150 katika Kanisa Katoliki, Parokia ya Nyakato, Jimbo Kuu la Mwanza.

-Akizungumza na Tanzania Daima jana ofisini kwake, Mwenyekiti wa Kamati ya ujenzi wa Kanisa hilo, Pastory Masota, alisema harambee hiyo itafanyika Jumapili wiki hii.

-"Tumemwalika Lowassa kufanikisha harambee yetu, maana ni mtu mwenye mahusiano mazuri na jamii yote. Harambee itakuwa Jumapili wiki hii pale kanisani Nyakato National".

"Ukitaka kufanikisha jambo lazima utafute mtu anayependa ushirikiano na maendeleo kwa ujumla. Lowasa amekubali mwaliko wetu na atakuja" alisema Masota.

Alisema kuwa kanisa hilo lina uwezo wa kuchukua waumini 1,350 kwa wakati mmoja.

Masota alisema harambee itatanguliwa na misa takatifu kuanzia saa 04:30 hadi saa 05:00 asubuhi, na wageni mbalimbali wa Serikali wamealikwa kutoka mikoa yote ya kanda ya Ziwa, Arusha na D’Salaam.

Alisema anaamini siku hiyo kanisa litafanikiwa kutokana na ushawishi unaokubalika wa kiongozi huyo.

Hadi sasa kanisa hilo limetumia zaidi ya shs. Million 170 na kwamba harambee hiyo itafanikisha kukamilisha ujenzi wa kanisa hilo ambalo ni la kwanza kwa ukubwa kujengwa bila bila ufadhili toka nje ya nchi.
 
ni bora kujua unadhambi na ukaungama kwani utasamehewa.
 
Nahisi jamaa ameingia ubia na viongozi wa dini ikiwa ni mkakati wa kujisafisha kuelekea mwaka 2015 maana ni juzi tu alialikwa kwenye hafla fulani na kanisa kanisa la anglikana. Ngoja tusubiri kitakachozungumzwa huko....lakini ni wazi kitendo cha kumualika kinamaanisha jamaa ni mtu safi.
 
Mim ni mkatoriki lakin siungi mkono Lowasa kualikwa kwenye hiyo harambee! Hovyo kabisa hizi dini za siku hizi hakuna kitu,wanawaza hela tu!
 
Back
Top Bottom