********************* Source: TANZANIA DAIMA Date=TODAY Page. 06 ********************* Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa, anatarajiwa kuongoza harambee ya kuchangisha zaidi ya shs. millioni 150 katika Kanisa Katoliki, Parokia ya Nyakato, Jimbo Kuu la Mwanza. -Akizungumza na Tanzania Daima jana ofisini kwake, Mwenyekiti wa Kamati ya ujenzi wa Kanisa hilo, Pastory Masota, alisema harambee hiyo itafanyika Jumapili wiki hii. -"Tumemwalika Lowassa kufanikisha harambee yetu, maana ni mtu mwenye mahusiano mazuri na jamii yote. Harambee itakuwa Jumapili wiki hii pale kanisani Nyakato National". "Ukitaka kufanikisha jambo lazima utafute mtu anayependa ushirikiano na maendeleo kwa ujumla. Lowasa amekubali mwaliko wetu na atakuja" alisema Masota. Alisema kuwa kanisa hilo lina uwezo wa kuchukua waumini 1,350 kwa wakati mmoja. Masota alisema harambee itatanguliwa na misa takatifu kuanzia saa 04:30 hadi saa 05:00 asubuhi, na wageni mbalimbali wa Serikali wamealikwa kutoka mikoa yote ya kanda ya Ziwa, Arusha na DSalaam. Alisema anaamini siku hiyo kanisa litafanikiwa kutokana na ushawishi unaokubalika wa kiongozi huyo. Hadi sasa kanisa hilo limetumia zaidi ya shs. Million 170 na kwamba harambee hiyo itafanikisha kukamilisha ujenzi wa kanisa hilo ambalo ni la kwanza kwa ukubwa kujengwa bila bila ufadhili toka nje ya nchi.